< Luka 17 >

1 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mambo yanayosababisha watu watende dhambi hayana budi kutukia. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha.
Or il dit à ses disciples: « Il est inévitable qu'il arrive des scandales, néanmoins malheur à celui par lequel ils arrivent;
2 Ingekuwa heri kama mtu huyo angefungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutoswa baharini, kuliko kumsababisha mmojawapo wa hawa wadogo kutenda dhambi.
il lui est plus avantageux qu'on lui mette au col une pierre meulière, et qu'on le précipite dans la mer, que de scandaliser un seul de ces petits.
3 Kwa hiyo, jilindeni. “Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu, msamehe.
Prenez garde à vous-mêmes: Si ton frère a péché, reprends-le, et s'il se repent, pardonne-lui;
4 Kama akikukosea mara saba kwa siku moja na mara saba kwa siku moja akaja kwako akisema, ‘Ninatubu,’ msamehe.”
et si, sept fois le jour, il a péché contre toi, et que sept fois il revienne vers toi, en disant: « Je me repens, » tu lui pardonneras. »
5 Mitume wake wakamwambia Bwana, “Tuongezee imani.”
Et les apôtres dirent au seigneur: « Mets en nous plus de foi. »
6 Bwana akawajibu, “Kama mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu, ‘Ngʼoka ukaote baharini,’ nao ungewatii.
Mais le seigneur dit: « Si vous aviez de la foi, gros comme un grain de moutarde, vous diriez à ce mûrier-ci: « Déracine-toi, et plante-toi dans la mer; » et il vous obéirait.
7 “Ikiwa mmoja wenu ana mtumishi anayelima shambani au anayechunga kondoo, je, mtumishi huyo arudipo atamwambia, ‘Karibu hapa keti ule chakula?’
Mais lequel de vous, ayant un esclave qui conduit la charrue ou paît les troupeaux, lui dira, à son retour des champs: « Viens vite te mettre à table? »
8 Je, badala yake, hatamwambia, ‘Niandalie chakula, nile, jifunge unitumikie ninapokula na kunywa; baadaye waweza kula na kunywa?’
Est-ce qu'au contraire il ne lui dira pas: « Prépare-moi à manger, et ceins-toi pour me servir jusques à ce que j'aie mangé et bu, et après cela, toi, tu mangeras et tu boiras? »
9 Je, huyo mtu atamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza yale aliyoamriwa?
Est-ce qu'il sait gré à l'esclave de ce qu'il a fait ce qui lui était prescrit?
10 Vivyo hivyo nanyi mkiisha kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi tu watumishi tusiostahili; tumefanya tu yale tuliyopaswa kufanya.’”
De même vous aussi, quand vous aurez fait tout ce qui vous a été prescrit, dites: Nous sommes des esclaves inutiles, c'est ce que nous devions faire que nous avons fait. »
11 Yesu alipokuwa njiani akienda Yerusalemu, alipitia mpakani mwa Samaria na Galilaya.
Et il advint, pendant le voyage vers Jérusalem, qu'il passait entre la Samarie et la Galilée.
12 Alipokuwa akiingia kwenye kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma wakakutana naye. Wakasimama mbali,
Et comme il entrait dans un village, vinrent à sa rencontre dix hommes lépreux, qui se levèrent de loin,
13 wakapaza sauti, wakasema, “Yesu, Bwana, tuhurumie!”
et ils haussèrent la voix en disant: « Jésus, maître, aie pitié de nous! »
14 Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Nao walipokuwa njiani wakienda, wakatakasika.
Ce que voyant, il leur dit: « Allez vous montrer aux prêtres. » Et il advint, pendant qu'ils s'y rendaient, qu'ils furent guéris.
15 Mmoja wao alipoona kwamba amepona, akarudi kwa Yesu, akimsifu Mungu kwa sauti kuu.
Or l'un d'entre eux voyant qu'il avait été guéri revint glorifiant Dieu à haute voix,
16 Akajitupa miguuni mwa Yesu akamshukuru. Yeye alikuwa Msamaria.
et il tomba la face contre terre à ses pieds en lui rendant grâces; et c'était un Samaritain.
17 Yesu akauliza, “Je, hawakutakaswa wote kumi? Wako wapi wale wengine tisa?
Mais Jésus prenant la parole dit: « Les dix n'ont-ils pas été guéris? Mais les neuf où sont-ils?
18 Hakuna hata mmoja aliyeonekana kurudi ili kumshukuru Mungu isipokuwa huyu mgeni?”
On ne les a pas vus revenir pour donner gloire à Dieu, sauf cet étranger. »
19 Yesu akamwambia, “Inuka na uende zako, imani yako imekuponya.”
Et il lui dit: « Lève-toi, va-t-en. »
20 Yesu alipoulizwa na Mafarisayo Ufalme wa Mungu utakuja lini, yeye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza kwa bidii,
Or ayant été interrogé par les pharisiens sur l'époque de la venue du royaume de Dieu, il leur répliqua: « Le royaume de Dieu ne vient pas de manière à être épié,
21 wala watu hawatasema, ‘Huu hapa,’ au ‘Ule kule,’ kwa maana Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.”
et l'on ne dira point: « Le voici ici, ou là. » Car voici, le royaume de Dieu est au milieu de vous. »
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Wakati utafika ambapo mtatamani kuiona moja ya siku ya Mwana wa Adamu, lakini hamtaiona.
Mais il dit aux disciples: « Des jours viendront, où vous désirerez voir un des jours du fils de l'homme, et vous ne le verrez pas;
23 Watu watawaambia, ‘Yule kule!’ Au, ‘Huyu hapa!’ Msiwakimbilie.
et on vous dira: « Le voici ici, ou le voilà là; » n'y courez pas,
24 Kwa maana kama vile umeme wa radi umulikavyo katika anga kuanzia mwisho mmoja hadi mwingine, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
car, comme l'éclair flamboyant brille de l'une des extrémités du ciel jusques à l'autre extrémité du ciel, il en sera de même du fils de l'homme;
25 Lakini kwanza itampasa kuteseka katika mambo mengi na kukataliwa na kizazi hiki.
mais il faut d'abord qu'il souffre beaucoup, et qu'il soit rejeté par cette génération.
26 “Kama ilivyokuwa siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Adamu.
Et comme il est advenu du temps de Noé, de même adviendra-t-il aussi du temps du fils de l'homme;
27 Watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina. Ndipo gharika ikaja na kuwaangamiza wote.
on mangeait, on buvait, les hommes prenaient des femmes et on donnait aux femmes des maris, jusques au jour où Noé entra dans l'arche; et le déluge survint et les fit tous périr.
28 “Ndivyo ilivyokuwa katika siku za Loti: Watu walikuwa wakila na kunywa, wakinunua na kuuza, wakilima na kujenga.
De même, comme il advint du temps de Lot, on mangeait, on buvait, on achetait, on vendait, on plantait, on bâtissait,
29 Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, ikanyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni ukawaangamiza wote.
mais le jour où Lot sortit de Sodome, il tomba du ciel une pluie de feu et de soufre et elle les fit tous périr,
30 “Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Adamu atakapofunuliwa.
de même en sera-t-il le jour où le fils de l'homme sera révélé.
31 Siku hiyo, mtu yeyote aliye juu ya dari ya nyumba yake, hata vitu vyake vikiwa ndani ya hiyo nyumba, asishuke kuvichukua. Vivyo hivyo mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua chochote.
En ce jour-là, que celui qui sera sur le toit, et dont les ustensiles sont dans la maison, ne descende point pour les prendre, et que celui qui est aux champs ne revienne pas non plus en arrière:
32 Mkumbukeni mke wa Loti!
souvenez-vous de la femme de Lot.
33 Mtu yeyote anayejaribu kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayeyapoteza maisha yake atayaokoa.
Mais celui qui aura cherché à rester en possession de sa vie la perdra, tandis que celui qui l'aura perdue la conservera.
34 Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa wamelala kitanda kimoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
Je vous le déclare, cette nuit-là deux personnes seront sur un lit, l'une sera prise et l'autre sera laissée.
35 Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa. [
Deux femmes moudront ensemble, l'une sera prise, mais l'autre sera laissée. »
36 Wanaume wawili watakuwa wanafanya kazi pamoja shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.]”
[Deux hommes seront dans la campagne, l'un sera pris et l'autre sera laissé.]
37 Kisha wakamuuliza, “Haya yatatukia wapi Bwana?” Akawaambia, “Pale ulipo mzoga, huko ndiko tai watakapokusanyika.”
Et prenant la parole ils lui dirent: « Où, Seigneur? » Mais il leur dit: « Là où est le corps, c'est là aussi que se rassembleront les aigles. »

< Luka 17 >