< Luka 17 >

1 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mambo yanayosababisha watu watende dhambi hayana budi kutukia. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha.
He said then to the disciples (of Him; *no*) Impossible it is that the stumbling blocks not to come, (but *N(k)O*) woe [to him] through whom they come!
2 Ingekuwa heri kama mtu huyo angefungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutoswa baharini, kuliko kumsababisha mmojawapo wa hawa wadogo kutenda dhambi.
It is better for him if (a stone of a mill *N(k)O*) is hung around the neck of him and he has been thrown into the sea than that he may cause to stumble little [ones] of these one.
3 Kwa hiyo, jilindeni. “Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu, msamehe.
do take heed to yourselves. If (now *k*) shall sin (against *k*) (you *K*) the brother of you, do rebuke him; and if he shall repent, do forgive him.
4 Kama akikukosea mara saba kwa siku moja na mara saba kwa siku moja akaja kwako akisema, ‘Ninatubu,’ msamehe.”
And if seven times in the day (he shall sin *N(k)O*) against you and seven times (day *k*) shall return (to *N(k)O*) you saying: I repent, you will forgive him.
5 Mitume wake wakamwambia Bwana, “Tuongezee imani.”
And said the apostles to the Lord; do add to us faith!
6 Bwana akawajibu, “Kama mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu, ‘Ngʼoka ukaote baharini,’ nao ungewatii.
Said then the Lord; If (you have *N(k)O*) faith like a grain of mustard, you have spoken then would to the mulberry tree this; do be uprooted and do be planted in the sea, and it have obeyed would you.
7 “Ikiwa mmoja wenu ana mtumishi anayelima shambani au anayechunga kondoo, je, mtumishi huyo arudipo atamwambia, ‘Karibu hapa keti ule chakula?’
Which now of you a servant having plowing or shepherding, the [one] having come in out of the field will say to him; Immediately having come (do recline? *N(k)O*)
8 Je, badala yake, hatamwambia, ‘Niandalie chakula, nile, jifunge unitumikie ninapokula na kunywa; baadaye waweza kula na kunywa?’
But surely he will say to him; do prepare what I may eat, and having girded yourself about do serve me while I may eat and I may drink, and after these things you will eat and will drink you yourself?’
9 Je, huyo mtu atamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza yale aliyoamriwa?
Not is he thankful to the servant (that [one] *k*) because he did the [things] having been commanded (to him not I think? *K*)
10 Vivyo hivyo nanyi mkiisha kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi tu watumishi tusiostahili; tumefanya tu yale tuliyopaswa kufanya.’”
Thus also you yourselves, when you may have done all the [things] having been commanded you, do say that Servants unworthy are we; (for *k*) that which (we were obliged *NK(o)*) to do we have done.
11 Yesu alipokuwa njiani akienda Yerusalemu, alipitia mpakani mwa Samaria na Galilaya.
And it came to pass in the going up (him *ko*) to Jerusalem that He himself was passing through ([the] midst *N(k)O*) of Samaria and Galilee.
12 Alipokuwa akiingia kwenye kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma wakakutana naye. Wakasimama mbali,
And when is entering He into a certain village met with Him ten leprous men, who (stood *NK(O)*) afar off.
13 wakapaza sauti, wakasema, “Yesu, Bwana, tuhurumie!”
And they themselves lifted up [their] voice saying; Jesus Master, do have compassion on us.
14 Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Nao walipokuwa njiani wakienda, wakatakasika.
And having seen [them] He said to them; Having gone do show yourselves to the priests. And it came to pass in the going them, they were cleansed.
15 Mmoja wao alipoona kwamba amepona, akarudi kwa Yesu, akimsifu Mungu kwa sauti kuu.
one then of them having seen that he was healed, turned back with a voice loud glorifying God.
16 Akajitupa miguuni mwa Yesu akamshukuru. Yeye alikuwa Msamaria.
and he fell on [his] face at the feet of Him giving thanks to Him; and he himself was a Samaritan.
17 Yesu akauliza, “Je, hawakutakaswa wote kumi? Wako wapi wale wengine tisa?
Having answered then Jesus said; (surely *NK(o)*) the ten were cleansed? But the nine are where?
18 Hakuna hata mmoja aliyeonekana kurudi ili kumshukuru Mungu isipokuwa huyu mgeni?”
None was there found having returned to give glory to God only except foreigner this?
19 Yesu akamwambia, “Inuka na uende zako, imani yako imekuponya.”
And He said to him; Having risen up do go forth; the faith of you has cured you!
20 Yesu alipoulizwa na Mafarisayo Ufalme wa Mungu utakuja lini, yeye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza kwa bidii,
Having been asked now by the Pharisees when is coming the kingdom of God, He answered to them and said; Not comes the kingdom of God with careful observation,
21 wala watu hawatasema, ‘Huu hapa,’ au ‘Ule kule,’ kwa maana Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.”
nor will they say; Behold here or (behold *ko*) There. Behold for the kingdom of God in the midst of you is.
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Wakati utafika ambapo mtatamani kuiona moja ya siku ya Mwana wa Adamu, lakini hamtaiona.
He said then to the disciples; Will come days when you will desire one of the days of the Son of Man to see and not you will behold [it].
23 Watu watawaambia, ‘Yule kule!’ Au, ‘Huyu hapa!’ Msiwakimbilie.
And they will say to you; Behold there or Behold here. Not may go forth nor may follow.
24 Kwa maana kama vile umeme wa radi umulikavyo katika anga kuanzia mwisho mmoja hadi mwingine, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
As for the lightning (which *ko*) is flashing from the [one end] under (the *no*) sky to the [other end] under [the] sky shines, thus will be (also *k*) the Son of Man in the day of Him.
25 Lakini kwanza itampasa kuteseka katika mambo mengi na kukataliwa na kizazi hiki.
First however it behooves Him many things to suffer and to be rejected by generation this.
26 “Kama ilivyokuwa siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Adamu.
And even as it came to pass in the days (*k*) of Noah, thus will it be also in the days of the Son of man:
27 Watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina. Ndipo gharika ikaja na kuwaangamiza wote.
They were eating, were drinking, were marrying, (were being given in marriage, *N(k)O*) until that day entered Noah into the ark, and came the flood and destroyed (all. *N(k)O*)
28 “Ndivyo ilivyokuwa katika siku za Loti: Watu walikuwa wakila na kunywa, wakinunua na kuuza, wakilima na kujenga.
Likewise (even as *N(k)O*) it came to pass in the days of Lot; they were eating, they were drinking, they were buying, they were selling, they were planting, they were building.
29 Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, ikanyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni ukawaangamiza wote.
in that then day went out Lot from Sodom, it rained fire and brimstone from heaven and destroyed (all; *N(k)O*)
30 “Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Adamu atakapofunuliwa.
According (*no*) (to these *N(k)O*) will it be in that day the Son of Man is revealed.
31 Siku hiyo, mtu yeyote aliye juu ya dari ya nyumba yake, hata vitu vyake vikiwa ndani ya hiyo nyumba, asishuke kuvichukua. Vivyo hivyo mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua chochote.
In that [very] day the [one who] will be on the housetop and the goods of him in the house, not he should come down to take away them; and the [one] in (the *k*) field likewise not he should return to the [things] back.
32 Mkumbukeni mke wa Loti!
do remember the wife of Lot!
33 Mtu yeyote anayejaribu kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayeyapoteza maisha yake atayaokoa.
Who[ever] if shall seek the life of him (to gain *N(K)O*) will lose it, (and *k*) who[ever] (but *no*) (maybe *N(k)O*) (shall lose *NK(o)*) (it *k*) will preserve it.
34 Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa wamelala kitanda kimoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
I say to you; in that night there will be two upon bed one: The one will be taken, and the other will be left.
35 Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa. [
There will be two [women] grinding at the same [place]; (The *no*) one will be taken, (and *k*) (and *no*) the other will be left.
36 Wanaume wawili watakuwa wanafanya kazi pamoja shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.]”
(two in field; one will be taken and another it will be left *K*)
37 Kisha wakamuuliza, “Haya yatatukia wapi Bwana?” Akawaambia, “Pale ulipo mzoga, huko ndiko tai watakapokusanyika.”
And answering they say to Him; Where, Lord? And He said to them; Where the body [is], there (also *no*) the vultures (will be gathered. *N(k)O*)

< Luka 17 >