< Luka 17 >

1 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mambo yanayosababisha watu watende dhambi hayana budi kutukia. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha.
And he said to his disciples, It is necessary for causes of trouble to come about, but unhappy is he by whom they come.
2 Ingekuwa heri kama mtu huyo angefungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutoswa baharini, kuliko kumsababisha mmojawapo wa hawa wadogo kutenda dhambi.
It would be well for him if a great stone was put round his neck and he was dropped into the sea, before he made trouble for any of these little ones.
3 Kwa hiyo, jilindeni. “Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu, msamehe.
Give attention to yourselves: if your brother does wrong, say a sharp word to him; and if he has sorrow for his sin, let him have forgiveness.
4 Kama akikukosea mara saba kwa siku moja na mara saba kwa siku moja akaja kwako akisema, ‘Ninatubu,’ msamehe.”
And if he does you wrong seven times in a day, and seven times comes to you and says, I have regret for what I have done; let him have forgiveness.
5 Mitume wake wakamwambia Bwana, “Tuongezee imani.”
And the twelve said to the Lord, Make our faith greater.
6 Bwana akawajibu, “Kama mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu, ‘Ngʼoka ukaote baharini,’ nao ungewatii.
And the Lord said, If your faith was only as great as a grain of mustard seed, you might say to this tree, Be rooted up and planted in the sea; and it would be done.
7 “Ikiwa mmoja wenu ana mtumishi anayelima shambani au anayechunga kondoo, je, mtumishi huyo arudipo atamwambia, ‘Karibu hapa keti ule chakula?’
But which of you, having a servant who is ploughing or keeping sheep, will say to him, when he comes in from the field, Come now and be seated and have a meal,
8 Je, badala yake, hatamwambia, ‘Niandalie chakula, nile, jifunge unitumikie ninapokula na kunywa; baadaye waweza kula na kunywa?’
Will he not say, Get a meal for me, and make yourself ready and see to my needs till I have had my food and drink; and after that you may have yours?
9 Je, huyo mtu atamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza yale aliyoamriwa?
Does he give praise to the servant because he did what was ordered?
10 Vivyo hivyo nanyi mkiisha kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi tu watumishi tusiostahili; tumefanya tu yale tuliyopaswa kufanya.’”
In the same way, when you have done all the things which are given you to do, say, There is no profit in us, for we have only done what we were ordered to do.
11 Yesu alipokuwa njiani akienda Yerusalemu, alipitia mpakani mwa Samaria na Galilaya.
And it came about that when they were on the way to Jerusalem he went through Samaria and Galilee.
12 Alipokuwa akiingia kwenye kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma wakakutana naye. Wakasimama mbali,
And when he went into a certain small town he came across ten men who were lepers, and they, keeping themselves at a distance,
13 wakapaza sauti, wakasema, “Yesu, Bwana, tuhurumie!”
Said, in loud voices, Jesus, Master, have mercy on us.
14 Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Nao walipokuwa njiani wakienda, wakatakasika.
And when he saw them he said, Go, and let the priests see you. And, while they were going, they were made clean.
15 Mmoja wao alipoona kwamba amepona, akarudi kwa Yesu, akimsifu Mungu kwa sauti kuu.
And one of them, when he saw that he was clean, turning back, gave praise to God in a loud voice;
16 Akajitupa miguuni mwa Yesu akamshukuru. Yeye alikuwa Msamaria.
And, falling down on his face at the feet of Jesus, he gave the credit to him; and he was a man of Samaria.
17 Yesu akauliza, “Je, hawakutakaswa wote kumi? Wako wapi wale wengine tisa?
And Jesus said, Were there not ten men who were made clean? where are the nine?
18 Hakuna hata mmoja aliyeonekana kurudi ili kumshukuru Mungu isipokuwa huyu mgeni?”
Have not any of them come back to give glory to God, but only this one from a strange land?
19 Yesu akamwambia, “Inuka na uende zako, imani yako imekuponya.”
And he said to him, Get up, and go on your way; your faith has made you well.
20 Yesu alipoulizwa na Mafarisayo Ufalme wa Mungu utakuja lini, yeye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza kwa bidii,
And when the Pharisees put questions to him about when the kingdom of God would come, he gave them an answer and said, The kingdom of God will not come through observation:
21 wala watu hawatasema, ‘Huu hapa,’ au ‘Ule kule,’ kwa maana Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.”
And men will not say, See, it is here! or, There! for the kingdom of God is among you.
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Wakati utafika ambapo mtatamani kuiona moja ya siku ya Mwana wa Adamu, lakini hamtaiona.
And he said to his disciples, The time will come when you will have a great desire to see one of the days of the Son of man, but you will not see it.
23 Watu watawaambia, ‘Yule kule!’ Au, ‘Huyu hapa!’ Msiwakimbilie.
And if they say to you, See, it is there! or, It is here! do not go away, or go after them.
24 Kwa maana kama vile umeme wa radi umulikavyo katika anga kuanzia mwisho mmoja hadi mwingine, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
For as in a thunderstorm the bright light is seen from one end of the sky to the other, so will the Son of man be when his time comes.
25 Lakini kwanza itampasa kuteseka katika mambo mengi na kukataliwa na kizazi hiki.
But first, he will have to undergo much and be put on one side by this generation.
26 “Kama ilivyokuwa siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Adamu.
And as it was in the days of Noah, so will it be in the day of the Son of man.
27 Watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina. Ndipo gharika ikaja na kuwaangamiza wote.
They were feasting and taking wives and getting married, till the day of the overflowing of the waters, when Noah went into the ark, and they all came to destruction.
28 “Ndivyo ilivyokuwa katika siku za Loti: Watu walikuwa wakila na kunywa, wakinunua na kuuza, wakilima na kujenga.
In the same way, in the days of Lot; they were feasting and trading, they were planting and building;
29 Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, ikanyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni ukawaangamiza wote.
But on the day when Lot went out of Sodom, fire came down from heaven and destruction came on them all.
30 “Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Adamu atakapofunuliwa.
So will it be in the day of the revelation of the Son of man.
31 Siku hiyo, mtu yeyote aliye juu ya dari ya nyumba yake, hata vitu vyake vikiwa ndani ya hiyo nyumba, asishuke kuvichukua. Vivyo hivyo mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua chochote.
On that day, if anyone is on the roof of the house, and his goods are in the house, let him not go down to take them away; and let him who is in the field not go back to his house.
32 Mkumbukeni mke wa Loti!
Keep in mind Lot's wife.
33 Mtu yeyote anayejaribu kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayeyapoteza maisha yake atayaokoa.
If anyone makes an attempt to keep his life, it will be taken from him, but if anyone gives up his life, he will keep it.
34 Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa wamelala kitanda kimoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
I say to you, In that night there will be two men sleeping in one bed, and one will be taken away and the other let go.
35 Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa. [
Two women will be crushing grain together; one will be taken away and the other let go.
36 Wanaume wawili watakuwa wanafanya kazi pamoja shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.]”
37 Kisha wakamuuliza, “Haya yatatukia wapi Bwana?” Akawaambia, “Pale ulipo mzoga, huko ndiko tai watakapokusanyika.”
And they, answering him, said, Where, Lord? And he said to them, Where the body is, there will the eagles come together.

< Luka 17 >