< Luka 14 >

1 Ikawa siku moja Yesu alipokuwa amekwenda kula chakula kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo siku ya Sabato, watu walikuwa wakimchunguza kwa bidii.
Jésus était entré dans la maison d'un des principaux Pharisiens, pour y prendre un repas; c'était un jour de sabbat. Aussi chacun l'observait-il,
2 Papo hapo mbele yake palikuwa na mtu mmoja mwenye ugonjwa wa kuvimba mwili.
car il y avait là, devant lui, un homme hydropique.
3 Yesu akawauliza wale Mafarisayo na walimu wa sheria, “Je, ni halali kuponya watu siku ya Sabato au la?”
Jésus s'adressa aux légistes et aux Pharisiens. «Est-il permis, oui ou non, de guérir le jour du sabbat?» leur demanda-t-il. Ils gardèrent le silence.
4 Wakakaa kimya. Hivyo Yesu akamshika yule mgonjwa mkono na kumponya, akamruhusu aende zake.
Alors il toucha de la main l'hydropique, le guérit et le congédia.
5 Kisha akawauliza, “Kama mmoja wenu angekuwa na mtoto au ngʼombe wake aliyetumbukia katika kisima siku ya Sabato, je, hamtamvuta mara moja na kumtoa?”
Puis, s'adressant toujours à eux, il dit: «Lequel d'entre vous, si son fils ou son boeuf vient à tomber dans un puits, un jour de sabbat, ne l'en retire aussitôt?»
6 Nao hawakuwa na la kusema.
A cela ils ne surent que répondre.
7 Alipoona jinsi wageni walivyokuwa wanachagua mahali pa heshima wakati wa kula, akawaambia mfano huu:
Ayant remarqué que les convives choisissaient les premières places, il leur raconta une parabole:
8 “Mtu akikualika arusini, usikae mahali pa mgeni wa heshima kwa kuwa inawezekana amealikwa mtu mheshimiwa kuliko wewe.
«Quand tu seras invité par quelqu'un à des noces, dit-il, ne va pas t'installer à la première place, de peur qu'un personnage plus considérable que toi, se trouvant parmi les invités,
9 Kama mkifanya hivyo yule aliyewaalika ninyi wawili atakuja na kukuambia, ‘Mpishe huyu mtu kiti chako.’ Ndipo kwa aibu utalazimika kukaa katika nafasi ya chini kabisa.
celui qui vous a conviés l'un et l'autre ne vienne te dire: «Donne-lui ta place» et que tu n'aies alors la confusion d'aller occuper la dernière place.
10 Badala yake, unapoalikwa, chagua nafasi ya chini, ili yule mwenyeji wako atakapokuona atakuja na kukuambia, ‘Rafiki yangu, nenda kwenye nafasi iliyo bora zaidi.’ Kwa jinsi hii utakuwa umepewa heshima mbele ya wageni wenzako wote.
Tout au contraire, quand tu seras invité, va te mettre à la dernière place, et alors, quand arrivera celui qui t'a invité, il te dira: «Mon ami, monte plus haut.» Ce sera pour toi un honneur devant tous les convives;
11 Kwa maana kila mtu ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.”
car quiconque s'élève lui-même sera abaissé, et quiconque s'abaisse lui-même sera élevé.»
12 Kisha Yesu akamwambia yule aliyewaalika, “Uandaapo karamu ya chakula cha mchana au cha jioni, usialike rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au majirani zako walio matajiri tu. Ukifanya hivyo, wao nao wanaweza kukualika kwao, nawe ukawa umelipwa kile ulichofanya na kupata thawabu yako.
Il disait aussi à son hôte: «Quand tu donnes à déjeuner ou à dîner, ne convoque ni tes amis, ni tes frères, ni tes parents, ni tes riches voisins, de crainte qu'ils ne t'invitent à leur tour et ne te rendent ce qu'ils auront reçu de toi.
13 Bali ufanyapo karamu, waalike maskini, vilema na vipofu,
Tout au contraire, quand tu fais un festin, appelles-y des pauvres, des infirmes, des estropiés, des aveugles.
14 nawe utabarikiwa kwa sababu hawa hawana uwezo wa kukulipa. Mungu atakulipa wakati wa ufufuo wa wenye haki.”
Heureux seras-tu, parce qu'ils n'ont pas de quoi te rendre ce festin; et il te sera rendu à la résurrection des justes.»
15 Mmoja wa wale waliokuwa pamoja naye mezani aliposikia hivi akamwambia Yesu, “Amebarikiwa mtu yule atakayekula katika karamu ya Ufalme wa Mungu!”
A ces mots, un des convives lui dit: «Heureux qui sera du banquet dans le Royaume de Dieu!» —
16 Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anaandaa karamu kubwa, akaalika watu wengi.
«Un homme, lui dit Jésus, donna un grand dîner, et y convia beaucoup de monde.
17 Wakati wa karamu ulipofika, akamtuma mtumishi wake akawaambie wale walioalikwa, ‘Karibuni, kila kitu ki tayari sasa.’
A l'heure du repas, il envoya son serviteur dire aux invités: «Venez, parce que tout est prêt.»
18 “Lakini wote, kila mmoja, wakaanza kutoa udhuru: Wa kwanza akasema, ‘Nimenunua shamba, lazima niende kuliona. Tafadhali niwie radhi.’
Mais tous, comme de concert, commencèrent à s'excuser.
19 “Mwingine akasema, ‘Ndipo tu nimenunua jozi tano za ngʼombe wa kulimia, nami ninakwenda kuwajaribu, tafadhali niwie radhi.’
«J'ai acheté un champ, dit le premier, il est de toute nécessité que j'aille le voir. Je t'en prie, tiens-moi pour excusé.» — «J'ai acheté cinq paires de boeufs, dit un autre, et je vais les essayer. Je t'en prie, tiens-moi pour excusé.» —
20 Naye mwingine akasema, ‘Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.’
«J'ai pris femme, dit un autre encore, donc je ne puis venir.»
21 “Yule mtumishi akarudi, akampa bwana wake taarifa. Ndipo yule mwenye nyumba akakasirika, akamwagiza yule mtumishi wake, akisema, ‘Nenda upesi kwenye mitaa na vichochoro vya mjini uwalete maskini, vilema, vipofu na viwete.’
Le serviteur revint et raconta cela à son maître. Se mettant en colère, le maître de maison dit alors à son serviteur: «Parcours à la hâte les places publiques et les rues de la ville, et amène ici les pauvres, les infirmes, les aveugles, les estropiés.»
22 “Yule mtumishi akamwambia, ‘Bwana, yale uliyoniagiza nimefanya, lakini bado ipo nafasi.’
Quand le serviteur lui dit: «Seigneur, on a fait ce que tu as ordonné», et il y a encore de la place,
23 “Ndipo yule bwana akamwambia mtumishi wake, ‘Nenda kwenye barabara na vijia vilivyoko nje ya mji na uwalazimishe watu waingie ili nyumba yangu ipate kujaa.
le maître lui répondit: «Va dans les chemins et le long des haies et contrains les gens d'entrer, afin que ma maison soit pleine.
24 Kwa maana nawaambia, hakuna hata mmoja wa wale walioalikwa atakayeionja karamu yangu.’”
Je vous le déclare, en effet, aucun de ces hommes qui étaient «les invités» ne prendra part à mon festin.»
25 Umati mkubwa wa watu ulikuwa ukisafiri pamoja na Yesu, naye akageuka, akawaambia,
Il était suivi de foules immenses; il se tourna vers elles et leur dit:
26 “Mtu yeyote anayekuja kwangu hawezi kuwa mwanafunzi wangu kama hatanipenda mimi zaidi ya baba yake na mama yake, mke wake na watoto wake, ndugu zake na dada zake, naam, hata maisha yake mwenyewe.
«Si quelqu'un vient à moi et ne hait pas et son père et sa mère, et sa femme et ses enfants, et ses frères et ses soeurs, plus encore: sa propre vie, il ne peut être mon disciple.»
27 Yeyote asiyeuchukua msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
«Celui qui ne porte pas sa croix, et ne marche pas à ma suite, ne peut être mon disciple.»
28 “Ni nani miongoni mwenu ambaye kama anataka kujenga nyumba, hakai kwanza chini na kufanya makisio ya gharama aone kama ana fedha za kutosha kukamilisha?
«Quel est celui d'entre vous qui, voulant bâtir une tour, ne réfléchisse d'abord, ne calcule la dépense, ne voie s'il a de quoi l'achever?
29 La sivyo, akiisha kuweka msingi, naye akiwa hana uwezo wa kuikamilisha, wote waionao wataanza kumdhihaki,
Il craindrait, après avoir jeté les fondements, de ne pouvoir achever. Tous ceux qui verraient cela se moqueraient de lui.
30 wakisema, ‘Mtu huyu alianza kujenga lakini hakuweza kukamilisha.’
«Le voilà, diraient-ils, l'homme qui a commencé à bâtir et quia été dans l'impossibilité d'achever!»
31 “Au ni mfalme gani atokaye kwenda kupigana vita na mfalme mwingine, ambaye hakai chini kwanza na kufikiri iwapo akiwa na jeshi la watu 10,000 ataweza kupigana na yule anayekuja na jeshi la watu 20,000?
«Quel est encore le roi, sur le point de faire la guerre à un autre roi, qui ne réfléchisse d'abord, qui n'examine s'il est capable, avec dix mille hommes, de marcher à la rencontre de celui qui s'avance sur lui avec vingt mille?
32 Kama hawezi, basi wakati yule mwingine akiwa bado yuko mbali, yeye hutuma ujumbe wa watu na kuomba masharti ya amani.
S'il en est incapable, alors que l'ennemi est encore loin, il lui envoie une ambassade avec des propositions de paix.»
33 Vivyo hivyo, yeyote miongoni mwenu ambaye hawezi kuacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
«Ainsi donc, quiconque ne renonce pas à tout ce qu'il possède ne peut être mon disciple.»
34 “Chumvi ni nzuri, lakini chumvi ikiwa imepoteza ladha yake, itafanywaje ili iweze kukolea tena?
«Le sel est bon; mais si le sel s'affadit, avec quoi lui rendra-t-on sa saveur?
35 Haifai ardhi wala kwa lundo la mbolea, bali hutupwa nje. “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
Il n'est plus propre à rien, ni pour la terre, ni pour le fumier. On le jette dehors. Que celui qui a des oreilles pour entendre, entende.»

< Luka 14 >