< Luka 1 >

1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
For as much as many have taken in hand to set forth in order a declaration of those things which are most surely believed among us,
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
Even as they delivered them to us, which from the beginning were eyewitnesses, and ministers of the word;
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
It seemed good to me also, having had perfect understanding of all things from the very first, to write to you in order, most excellent Theophilus,
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
That you might know the certainty of those things, wherein you have been instructed.
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
THERE was in the days of Herod, the king of Judaea, a certain priest named Zacharias, of the course of Abia: and his wife was of the daughters of Aaron, and her name was Elisabeth.
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
And they were both righteous before God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
And they had no child, because that Elisabeth was barren, and they both were now well stricken in years.
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
And it came to pass, that while he executed the priest’s office before God in the order of his course,
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
According to the custom of the priest’s office, his lot was to burn incense when he went into the temple of the Lord.
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
And the whole multitude of the people were praying without at the time of incense.
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
And there appeared to him an angel of the Lord standing on the right side of the altar of incense.
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
And when Zacharias saw him, he was troubled, and fear fell on him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
But the angel said to him, Fear not, Zacharias: for your prayer is heard; and your wife Elisabeth shall bear you a son, and you shall call his name John.
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
And you shall have joy and gladness; and many shall rejoice at his birth.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
For he shall be great in the sight of the Lord, and shall drink neither wine nor strong drink; and he shall be filled with the Holy Ghost, even from his mother’s womb.
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
And many of the children of Israel shall he turn to the Lord their God.
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
And he shall go before him in the spirit and power of Elias, to turn the hearts of the fathers to the children, and the disobedient to the wisdom of the just; to make ready a people prepared for the Lord.
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
And Zacharias said to the angel, Whereby shall I know this? for I am an old man, and my wife well stricken in years.
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
And the angel answering said to him, I am Gabriel, that stand in the presence of God; and am sent to speak to you, and to show you these glad tidings.
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
And, behold, you shall be dumb, and not able to speak, until the day that these things shall be performed, because you believe not my words, which shall be fulfilled in their season.
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
And the people waited for Zacharias, and marveled that he tarried so long in the temple.
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
And when he came out, he could not speak to them: and they perceived that he had seen a vision in the temple: for he beckoned to them, and remained speechless.
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
And it came to pass, that, as soon as the days of his ministration were accomplished, he departed to his own house.
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
And after those days his wife Elisabeth conceived, and hid herself five months, saying,
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
Thus has the Lord dealt with me in the days wherein he looked on me, to take away my reproach among men.
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
And in the sixth month the angel Gabriel was sent from God to a city of Galilee, named Nazareth,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
To a virgin espoused to a man whose name was Joseph, of the house of David; and the virgin’s name was Mary.
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
And the angel came in to her, and said, Hail, you that are highly favored, the Lord is with you: blessed are you among women.
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
And when she saw him, she was troubled at his saying, and cast in her mind what manner of salutation this should be.
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
And the angel said to her, Fear not, Mary: for you have found favor with God.
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
And, behold, you shall conceive in your womb, and bring forth a son, and shall call his name JESUS.
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
He shall be great, and shall be called the Son of the Highest: and the Lord God shall give to him the throne of his father David:
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
And he shall reign over the house of Jacob for ever; and of his kingdom there shall be no end. (aiōn g165)
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
Then said Mary to the angel, How shall this be, seeing I know not a man?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
And the angel answered and said to her, The Holy Ghost shall come on you, and the power of the Highest shall overshadow you: therefore also that holy thing which shall be born of you shall be called the Son of God.
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
And, behold, your cousin Elisabeth, she has also conceived a son in her old age: and this is the sixth month with her, who was called barren.
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
For with God nothing shall be impossible.
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
And Mary said, Behold the handmaid of the Lord; be it to me according to your word. And the angel departed from her.
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
And Mary arose in those days, and went into the hill country with haste, into a city of Juda;
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
And entered into the house of Zacharias, and saluted Elisabeth.
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
And it came to pass, that, when Elisabeth heard the salutation of Mary, the babe leaped in her womb; and Elisabeth was filled with the Holy Ghost:
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
And she spoke out with a loud voice, and said, Blessed are you among women, and blessed is the fruit of your womb.
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
And what is this to me, that the mother of my Lord should come to me?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
For, see, as soon as the voice of your salutation sounded in my ears, the babe leaped in my womb for joy.
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
And blessed is she that believed: for there shall be a performance of those things which were told her from the Lord.
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
And Mary said, My soul does magnify the Lord,
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
And my spirit has rejoiced in God my Savior.
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
For he has regarded the low estate of his handmaiden: for, behold, from now on all generations shall call me blessed.
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
For he that is mighty has done to me great things; and holy is his name.
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
And his mercy is on them that fear him from generation to generation.
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
He has showed strength with his arm; he has scattered the proud in the imagination of their hearts.
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
He has put down the mighty from their seats, and exalted them of low degree.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
He has filled the hungry with good things; and the rich he has sent empty away.
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
He has helped his servant Israel, in remembrance of his mercy;
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
As he spoke to our fathers, to Abraham, and to his seed for ever. (aiōn g165)
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
And Mary stayed with her about three months, and returned to her own house.
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
Now Elisabeth’s full time came that she should be delivered; and she brought forth a son.
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
And her neighbors and her cousins heard how the Lord had showed great mercy on her; and they rejoiced with her.
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
And it came to pass, that on the eighth day they came to circumcise the child; and they called him Zacharias, after the name of his father.
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
And his mother answered and said, Not so; but he shall be called John.
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
And they said to her, There is none of your kindred that is called by this name.
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
And they made signs to his father, how he would have him called.
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
And he asked for a writing table, and wrote, saying, His name is John. And they marveled all.
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
And his mouth was opened immediately, and his tongue loosed, and he spoke, and praised God.
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
And fear came on all that dwelled round about them: and all these sayings were noised abroad throughout all the hill country of Judaea.
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
And all they that heard them laid them up in their hearts, saying, What manner of child shall this be! And the hand of the Lord was with him.
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
And his father Zacharias was filled with the Holy Ghost, and prophesied, saying,
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
Blessed be the Lord God of Israel; for he has visited and redeemed his people,
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
And has raised up an horn of salvation for us in the house of his servant David;
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
As he spoke by the mouth of his holy prophets, which have been since the world began: (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
That we should be saved from our enemies, and from the hand of all that hate us;
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
To perform the mercy promised to our fathers, and to remember his holy covenant;
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
The oath which he swore to our father Abraham,
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
That he would grant to us, that we being delivered out of the hand of our enemies might serve him without fear,
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
In holiness and righteousness before him, all the days of our life.
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
And you, child, shall be called the prophet of the Highest: for you shall go before the face of the Lord to prepare his ways;
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
To give knowledge of salvation to his people by the remission of their sins,
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
Through the tender mercy of our God; whereby the dayspring from on high has visited us,
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
To give light to them that sit in darkness and in the shadow of death, to guide our feet into the way of peace.
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
And the child grew, and waxed strong in spirit, and was in the deserts till the day of his showing to Israel.

< Luka 1 >