< Maombolezo 4 >

1 Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
O jakże zaśniedziało złoto! [Jakże] zmieniło się najczystsze złoto! Rozrzucono kamienie świątyni po rogach wszystkich ulic.
2 Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
Szlachetni synowie Syjonu, cenieni jak czyste złoto, jakże są poczytywani za gliniane naczynia, za dzieło rąk garncarza!
3 Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
[Nawet] smoki dają pierś i karmią swoje młode, [ale] córka mojego ludu stała się okrutna jak strusie na pustyni.
4 Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
Język ssącego przylgnął do podniebienia z powodu pragnienia, dzieci prosiły o chleb, lecz nikt im go nie ułamał.
5 Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
Ci, którzy jadali wyborne potrawy, giną na ulicach. Ci, którzy byli wychowani w szkarłacie, przytulają się do gnoju.
6 Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
Większa jest nieprawość córki mojego ludu niż grzech Sodomy, co została zniszczona w okamgnieniu, a nie dotknęła jej żadna ręka.
7 Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
Jej nazirejczycy byli czystsi niż śnieg, bielsi niż mleko, ich ciała bardziej rumiane niż rubiny, [byli] wyciosani jak szafir.
8 Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
Ale [teraz] ich wygląd jest czarniejszy niż węgiel, nie poznaje się ich na ulicach. Ich skóra przyschła do kości, wyschła i stała się jak drewno.
9 Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
Lepiej jest tym, którzy zostali pobici od miecza, niż tym, co umierają z głodu, gdyż oni giną, będąc przebici brakiem plonów pola.
10 Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
Ręce czułych kobiet gotowały własne dzieci. Były ich pokarmem w czasie klęski córki mojego ludu.
11 Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
Dopełnił PAN swego wzburzenia, wylał swój zapalczywy gniew i rozpalił ogień na Syjonie, który strawił jego fundamenty.
12 Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
Nigdy nie uwierzyliby królowie ziemi i wszyscy mieszkańcy świata, że przeciwnik i wróg mógłby wejść w bramy Jerozolimy.
13 Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
Z powodu grzechów jej proroków i nieprawości jej kapłanów, którzy przelewali krew sprawiedliwych pośród niej;
14 Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
Tułali się [jak] ślepi po ulicach, splugawili się krwią, tak że nie można było dotknąć ich szat.
15 Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”
[Dlatego] wołano na nich: Odstąpcie, nieczyści! Odstąpcie, odstąpcie, nie dotykajcie! Gdy odeszli i tułali się, mówiono wśród pogan: Nie będą już mogli [tam] zamieszkać.
16 Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.
Oblicze PANA rozproszyło ich, już więcej nie spojrzy na nich; nie ma szacunku dla kapłanów ani nie ma litości dla starców.
17 Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.
Aż dotąd nasze oczy słabły z powodu naszej daremnej pomocy. Wypatrywaliśmy czujnie narodu, który nie mógł nas wybawić.
18 Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.
Śledzą nasze kroki tak, że nie możemy chodzić po naszych ulicach. Zbliżył się nasz koniec, wypełniły się nasze dni, nadszedł nasz kres.
19 Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.
Nasi prześladowcy są szybsi niż orły niebieskie; ścigają nas po górach i czyhają na nas na pustyni.
20 Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.
Oddech naszych nozdrzy, pomazaniec PANA, został schwytany w ich doły; o nim mówiliśmy: W jego cieniu będziemy żyć wśród pogan.
21 Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.
Raduj się i wesel, córko Edomu, która mieszkasz w ziemi Us; przejdzie też do ciebie kielich, upijesz się i obnażysz.
22 Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.
Skończyła się twoja kara, o córko Syjonu; [on] nie będzie cię dłużej trzymał na wygnaniu. Nawiedzi twoją nieprawość, córko Edomu, i odkryje twoje grzechy.

< Maombolezo 4 >