< Waamuzi 3 >

1 Haya ndiyo mataifa Bwana aliyoyaacha ili kuwajaribu Waisraeli wote ambao hawakujua vita vyovyote vya Kanaani
A oto narody, które PAN pozostawił, aby przez nie doświadczyć Izraela, czyli tych wszystkich, którzy nie zaznali żadnych wojen o Kanaan;
2 (alifanya hivi ili tu kuwafundisha wazao wa Waisraeli ambao hawakuwa wamejua vita hapo awali):
Aby pokolenia synów Izraela [ich] doświadczyły, aby nauczyły się sztuki wojennej, te, które jej przedtem nie zaznały:
3 wafalme watano wa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, Wahivi waishio katika milima ya Lebanoni kuanzia Mlima wa Baal-Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
Pięciu książąt filistyńskich oraz wszyscy Kananejczycy, Sydończycy i Chiwwici mieszkający na górze Libanu, od góry Baal-Hermon aż do wejścia do Chamat.
4 Waliachwa ili kuwajaribu Waisraeli kuona kama wangetii amri za Bwana, alizokuwa amewapa baba zao kwa mkono wa Mose.
Oni pozostali, aby przez nich doświadczyć Izraela; by poznać, czy będą posłuszni przykazaniom PANA, które dał ich ojcom przez Mojżesza.
5 Waisraeli wakaishi miongoni mwa Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Tak więc synowie Izraela mieszkali pośród Kananejczyków, Chetytów, Amorytów, Peryzzytów, Chiwwitów i Jebusytów.
6 Wakawaoa binti zao, nao wakawatoa binti zao waolewe na wana wa hayo mataifa, na kuitumikia miungu yao.
I brali sobie ich córki za żony, a swe córki dawali ich synom i służyli ich bogom.
7 Waisraeli wakafanya maovu machoni pa Bwana, wakamsahau Bwana Mungu wao na kutumikia Mabaali na Maashera.
I synowie Izraela czynili to, co złe w oczach PANA: zapomnieli o PANU, swym Bogu, i służyli Baalom i gajom.
8 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli, hivyo akawauza na kuwatia mikononi mwa Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu-Naharaimu ambaye Israeli walikuwa chini yake wakimtumikia kwa muda wa miaka minane.
Wtedy zapłonął gniew PANA przeciw Izraelowi i wydał ich w ręce Kuszan-Riszataima, króla Mezopotamii. I synowie Izraela służyli Kuszan-Risztaimowi przez osiem lat.
9 Waisraeli walipomlilia Bwana, yeye akawainulia mwokozi, Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu, ambaye aliwaokoa.
A gdy synowie Izraela wołali do PANA, PAN wzbudził synom Izraela wybawcę, który ich wybawił – Otniela, syna Keneza, młodszego brata Kaleba.
10 Roho wa Bwana akaja juu yake, hivyo akawa mwamuzi wa Israeli, akaenda vitani. Bwana akamtia Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu mikononi mwa Othnieli, naye akamshinda.
Zstąpił na niego Duch PANA i sądził Izraela; a [gdy] wyruszył na wojnę, PAN wydał w jego ręce Kuszan-Riszataima, króla Mezopotamii, i jego ręka wzmocniła się nad Kuszan-Riszataimem.
11 Hivyo nchi ikawa na amani kwa muda wa miaka arobaini, mpaka Othnieli mwana wa Kenazi alipofariki.
I ziemia zaznała pokoju przez czterdzieści lat, aż umarł Otniel, syn Keneza.
12 Waisraeli wakafanya maovu mbele za Bwana tena, kwa kuwa walifanya maovu hayo Bwana akamtia nguvu Egloni mfalme wa Moabu dhidi ya Israeli.
Potem synowie Izraela znowu czynili to, co złe w oczach PANA. I PAN wzmocnił przeciw Izraelowi Eglona, króla Moabu, bo czynili to, co złe w oczach PANA.
13 Egloni akawataka Waamoni na Waamaleki waungane naye, akaja kuishambulia Israeli, nao wakatwaa Mji wa Mitende
Ten zgromadził przy sobie synów Ammona i Amaleka, wyruszył i pobił Izraela, i zajął miasto palm.
14 Waisraeli wakawa chini ya Egloni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka kumi na minane.
Tak więc synowie Izraela służyli Eglonowi, królowi Moabu, przez osiemnaście lat.
15 Waisraeli wakamlilia tena Bwana, naye akawapa mwokozi: Ehudi, mtu wa shoto, mwana wa Gera, Mbenyamini. Waisraeli wakatuma kwa Egloni mfalme wa Moabu ushuru kwa mkono wa Ehudi.
A gdy synowie Izraela wołali do PANA, PAN wzbudził im wybawcę – Ehuda, syna Gery, Beniaminitę, człowieka leworęcznego. I synowie Izraela posłali przez niego dar Eglonowi, królowi Moabu.
16 Basi Ehudi alikuwa ametengeneza upanga wenye ukatao kuwili, urefu wake ni kama dhiraa moja, akaufunga upanga huo ndani ya nguo yake kwenye paja lake la mkono wa kuume.
I Ehud sporządził sobie miecz o dwóch ostrzach, długości jednego łokcia, i przypasał go sobie pod szatą do prawego biodra.
17 Akamkabidhi ushuru Egloni mfalme wa Moabu, ambaye alikuwa mtu mnene sana.
I przyniósł dar Eglonowi, królowi Moabu. Eglon zaś był człowiekiem bardzo otyłym.
18 Baada ya Ehudi kumkabidhi ule ushuru, wale watu waliokuwa wameubeba huo ushuru aliwaruhusu waende zao.
A gdy oddał dar, odprawił ludzi, którzy dar przynieśli;
19 Yeye mwenyewe akafuatana nao hadi kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe karibu na Gilgali, ndipo yeye akarudi, akafika kwa Egloni na kusema, “Ee Mfalme, ninao ujumbe wa siri kwa ajili yako.” Mfalme akasema, “Nyamazeni kimya!” Nao wale waliomhudumia wote wakamwacha, wakatoka nje.
A sam wrócił z kamiennych gór, które były w Gilgal, i powiedział: Mam do ciebie tajną sprawę, o królu. A ten odpowiedział: Cisza! I wyszli od niego wszyscy, którzy przed nim stali.
20 Ndipo Ehudi akamsogelea alipokuwa ameketi peke yake kwenye chumba cha juu cha jumba lake la kifalme la majira ya kiangazi, na kusema, “Ninao ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili yako.” Mfalme alipokuwa anainuka kutoka kwenye kiti chake,
Wtedy Ehud podszedł do niego. On zaś siedział w letniej komnacie, którą miał tylko dla siebie. I Ehud powiedział: Mam dla ciebie słowo od Boga. A [ten] powstał z tronu.
21 Ehudi akaunyoosha mkono wake wa kushoto na kuufuta ule upanga aliokuwa ameufunga kwenye paja lake la kulia, akamdunga Mfalme Egloni tumboni mwake.
Wtedy Ehud wyciągnął lewą rękę, dobył miecz ze swego prawego biodra i wbił go w jego brzuch.
22 Hata mpini nao ukazama tumboni pamoja na upanga wenyewe, nao upanga ukatokea mgongoni mwake. Ehudi hakuuchomoa huo upanga, nayo mafuta yakashikamana juu ya upanga.
A rękojeść weszła razem z ostrzem i tłuszcz zamknął się za ostrzem tak, że nie mógł wyjąć miecza z jego brzucha; i wyszły z niego nieczystości.
23 Ehudi akatoka nje barazani; akamfungia milango ya chumba cha juu na kuifunga kwa funguo.
Potem Ehud wyszedł przez przedsionek, zamknął za sobą drzwi komnaty i zasunął rygle.
24 Baada ya kuondoka, watumishi wakaja na kukuta milango ya chumba cha juu imefungwa kwa funguo. Wakasema, “Bila shaka amejipumzisha kwenye chumba cha ndani cha nyumba yake ya majira ya kiangazi.”
A gdy wyszedł, przyszli słudzy i kiedy zobaczyli, że drzwi komnaty były zamknięte, powiedzieli: Z pewnością król odpoczywa w letniej komnacie.
25 Wakangoja hata wakawa na fadhaa, basi wakati hakufungua milango ya chumba, wakachukua funguo na kuifungua. Tazama wakaona bwana wao amelala sakafuni, amekufa.
I czekali długo, aż poczuli się zawstydzeni. Widząc, że on nie otwiera drzwi komnaty, wzięli klucz i otworzyli; a oto ich pan leżał na ziemi martwy.
26 Walipokuwa wangali wanangoja, Ehudi akatoroka, akapita hapo kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe na kukimbilia Seira.
Lecz Ehud uciekł, kiedy oni zwlekali [z wejściem], minął kamienne góry i uciekł aż do Seiru.
27 Alipofika huko, akapiga tarumbeta katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakateremka pamoja naye kutoka vilimani, yeye akiwa anawaongoza.
A gdy przyszedł, zadął w trąbę na górze Efraim; i synowie Izraela zeszli z nim z góry, a on na ich czele.
28 Akawaagiza, “Nifuateni, kwa kuwa Bwana amewatia Moabu, adui zenu, mikononi mwenu.” Kwa hiyo wakateremka wakamfuata, wakavishika vivuko vya Yordani kuelekea Moabu, wala hawakuacha mtu yeyote kuvuka.
I powiedział do nich: Pójdźcie za mną. PAN bowiem wydał waszych wrogów, Moabitów, w wasze ręce. Poszli więc za nim, zajęli brody Jordanu do Moabu i nie pozwalali nikomu przejść.
29 Wakati huo wakawaua Wamoabu watu waume wapatao 10,000 ambao wote walikuwa wenye nguvu na mashujaa; hakuna mtu yeyote aliyetoroka.
W tym czasie zabili około dziesięciu tysięcy mężczyzn spośród Moabitów, samych krzepkich i walecznych, i nikt nie uszedł [z życiem].
30 Siku ile Moabu wakashindwa na Israeli, nayo nchi ikawa na amani kwa miaka themanini.
W tym dniu Moab został poniżony pod ręką Izraela; i ziemia żyła w pokoju przez osiemdziesiąt lat.
31 Baada ya Ehudi akaja Shamgari mwana wa Anathi, aliyewapiga Wafilisti 600 kwa fimbo iliyochongoka ya kuongozea ngʼombe. Naye pia akawaokoa Waisraeli.
A po nim był Szamgar, syn Anata. Zabił on sześciuset mężczyzn spośród Filistynów ościeniem na woły. On także wybawił Izraela.

< Waamuzi 3 >