< Yoshua 16 >

1 Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
The lot came out for the descendants of Joseph from the Jordan at Jericho, at the waters of Jericho on the east, even the wilderness, going up from Jericho through the hill country to Bethel.
2 Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
It went out from Bethel to Luz, and passed along to the border of the Archites at Ataroth;
3 ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
and it went down westward to the border of the Japhletites, to the border of Lower Beth Horon, even to Gezer; and ended at the sea.
4 Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
The descendants of Joseph, Manasseh and Ephraim, took their inheritance.
5 Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
This was the border of the descendants of Ephraim according to their families. The border of their inheritance eastward was Ataroth Addar, to Upper Beth Horon.
6 na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
The border went out westward at Michmethath on the north of Termah. The border turned about eastward to Taanath Shiloh, and passed along it on the east of Janoah.
7 Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
It went down from Janoah to Ataroth, to Naaratah, reached to Jericho, and went out at the Jordan.
8 Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
From Tappuah the border went along westward to Wadi Kanah; and ended at the sea. This is the inheritance of the tribe of the descendants of Ephraim according to their families;
9 Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
together with the cities which were set apart for the descendants of Ephraim in the midst of the inheritance of the descendants of Manasseh, all the cities with their villages.
10 Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.
They did not drive out the Canaanites who lived in Gezer; but the Canaanites dwell in the midst of Ephraim to this day, and have become servants to do forced labor.

< Yoshua 16 >