< Yohana 11 >

1 Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake.
Now a certain [man] was sick, [named] Lazarus, of Bethany, the town of Mary and her sister Martha.
2 Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.
(It was [that] Mary which anointed the Lord with ointment, and wiped his feet with her hair, whose brother Lazarus was sick.)
3 Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”
Therefore his sisters sent unto him, saying, Lord, behold, he whom thou lovest is sick.
4 Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”
When Jesus heard [that], he said, This sickness is not unto death, but for the glory of God, that the Son of God might be glorified thereby.
5 Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao,
Now Jesus loved Martha, and her sister, and Lazarus.
6 baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.
When he had heard therefore that he was sick, he abode two days still in the same place where he was.
7 Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”
Then after that saith he to [his] disciples, Let us go into Judæa again.
8 Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”
[His] disciples say unto him, Master, the Jews of late sought to stone thee; and goest thou thither again?
9 Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu.
Jesus answered, Are there not twelve hours in the day? If any man walk in the day, he stumbleth not, because he seeth the light of this world.
10 Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”
But if a man walk in the night, he stumbleth, because there is no light in him.
11 Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”
These things said he: and after that he saith unto them, Our friend Lazarus sleepeth; but I go, that I may awake him out of sleep.
12 Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”
Then said his disciples, Lord, if he sleep, he shall do well.
13 Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.
Howbeit Jesus spake of his death: but they thought that he had spoken of taking of rest in sleep.
14 Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.
Then said Jesus unto them plainly, Lazarus is dead.
15 Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”
And I am glad for your sakes that I was not there, to the intent ye may believe; nevertheless let us go unto him.
16 Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”
Then said Thomas, which is called Didymus, unto his fellowdisciples, Let us also go, that we may die with him.
17 Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
Then when Jesus came, he found that he had [lain] in the grave four days already.
18 Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,
Now Bethany was nigh unto Jerusalem, about fifteen furlongs off:
19 na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
And many of the Jews came to Martha and Mary, to comfort them concerning their brother.
20 Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.
Then Martha, as soon as she heard that Jesus was coming, went and met him: but Mary sat [still] in the house.
21 Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.
Then said Martha unto Jesus, Lord, if thou hadst been here, my brother had not died.
22 Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
But I know, that even now, whatsoever thou wilt ask of God, God will give [it] thee.
23 Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
Jesus saith unto her, Thy brother shall rise again.
24 Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
Martha saith unto him, I know that he shall rise again in the resurrection at the last day.
25 Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi
Jesus said unto her, I am the resurrection, and the life: he that believeth in me, though he were dead, yet shall he live:
26 na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?” (aiōn g165)
And whosoever liveth and believeth in me shall never die. Believest thou this? (aiōn g165)
27 Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
She saith unto him, Yea, Lord: I believe that thou art the Christ, the Son of God, which should come into the world.
28 Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
And when she had so said, she went her way, and called Mary her sister secretly, saying, The Master is come, and calleth for thee.
29 Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.
As soon as she heard [that], she arose quickly, and came unto him.
30 Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
Now Jesus was not yet come into the town, but was in that place where Martha met him.
31 Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.
The Jews then which were with her in the house, and comforted her, when they saw Mary, that she rose up hastily and went out, followed her, saying, She goeth unto the grave to weep there.
32 Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”
Then when Mary was come where Jesus was, and saw him, she fell down at his feet, saying unto him, Lord, if thou hadst been here, my brother had not died.
33 Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
When Jesus therefore saw her weeping, and the Jews also weeping which came with her, he groaned in the spirit, and was troubled,
34 Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
And said, Where have ye laid him? They said unto him, Lord, come and see.
35 Yesu akalia machozi.
Jesus wept.
36 Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
Then said the Jews, Behold how he loved him!
37 Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
And some of them said, Could not this man, which opened the eyes of the blind, have caused that even this man should not have died?
38 Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake.
Jesus therefore again groaning in himself cometh to the grave. It was a cave, and a stone lay upon it.
39 Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.” Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”
Jesus said, Take ye away the stone. Martha, the sister of him that was dead, saith unto him, Lord, by this time he stinketh: for he hath been [dead] four days.
40 Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”
Jesus saith unto her, Said I not unto thee, that, if thou wouldest believe, thou shouldest see the glory of God?
41 Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.
Then they took away the stone [from the place] where the dead was laid. And Jesus lifted up [his] eyes, and said, Father, I thank thee that thou hast heard me.
42 Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”
And I knew that thou hearest me always: but because of the people which stand by I said [it], that they may believe that thou hast sent me.
43 Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!”
And when he thus had spoken, he cried with a loud voice, Lazarus, come forth.
44 Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”
And he that was dead came forth, bound hand and foot with graveclothes: and his face was bound about with a napkin. Jesus saith unto them, Loose him, and let him go.
45 Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini.
Then many of the Jews which came to Mary, and had seen the things which Jesus did, believed on him.
46 Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya.
But some of them went their ways to the Pharisees, and told them what things Jesus had done.
47 Kwa hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakaita mkutano wa baraza. Wakaulizana, “Tufanyeje? Huyu mtu anafanya ishara nyingi.
Then gathered the chief priests and the Pharisees a council, and said, What do we? for this man doeth many miracles.
48 Kama tukimwacha aendelee hivi, kila mtu atamwamini, nao Warumi watakuja na kupaharibu mahali petu patakatifu na taifa letu.”
If we let him thus alone, all [men] will believe on him: and the Romans shall come and take away both our place and nation.
49 Mmoja wao aliyeitwa Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, akasema, “Ninyi hamjui kitu chochote!
And one of them, [named] Caiaphas, being the high priest that same year, said unto them, Ye know nothing at all,
50 Hamjui kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa lote liangamie?”
Nor consider that it is expedient for us, that one man should die for the people, and that the whole nation perish not.
51 Hakusema haya kutokana na mawazo yake mwenyewe bali kama kuhani mkuu mwaka huo, alitabiri kuwa Yesu angelikufa kwa ajili ya taifa la Wayahudi,
And this spake he not of himself: but being high priest that year, he prophesied that Jesus should die for that nation;
52 wala si kwa ajili ya taifa hilo pekee, bali pia kwa ajili ya watoto wa Mungu waliotawanyika, ili kuwaleta pamoja na kuwafanya wawe wamoja.
And not for that nation only, but that also he should gather together in one the children of God that were scattered abroad.
53 Hivyo tangu siku hiyo wakawa wanafanya mipango ili wamuue Yesu.
Then from that day forth they took counsel together for to put him to death.
54 Kwa hiyo Yesu akawa hatembei hadharani miongoni mwa Wayahudi, bali alijitenga akaenda sehemu iliyo karibu na jangwa kwenye kijiji kiitwacho Efraimu. Akakaa huko na wanafunzi wake.
Jesus therefore walked no more openly among the Jews; but went thence unto a country near to the wilderness, into a city called Ephraim, and there continued with his disciples.
55 Basi Pasaka ya Wayahudi ilipokuwa imekaribia, watu wengi walitoka vijijini wakaenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili wakajitakase.
And the Jews’ passover was nigh at hand: and many went out of the country up to Jerusalem before the passover, to purify themselves.
56 Watu wakawa wanamtafuta Yesu, nao waliposimama kwenye eneo la Hekalu waliulizana, Je, mtu huyu hatakuja kamwe kwenye Sikukuu?
Then sought they for Jesus, and spake among themselves, as they stood in the temple, What think ye, that he will not come to the feast?
57 Viongozi wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kuwa yeyote atakayejua mahali Yesu aliko, lazima atoe taarifa ili wapate kumkamata.
Now both the chief priests and the Pharisees had given a commandment, that, if any man knew where he were, he should shew [it], that they might take him.

< Yohana 11 >