< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
И отвечал Иов и сказал:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
о, если бы верно взвешены были вопли мои, и вместе с ними положили на весы страдание мое!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Оно верно перетянуло бы песок морей! Оттого слова мои неистовы.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Ибо стрелы Вседержителя во мне; яд их пьет дух мой; ужасы Божии ополчились против меня.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Ревет ли дикий осел на траве? мычит ли бык у месива своего?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Едят ли безвкусное без соли, и есть ли вкус в яичном белке?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
До чего не хотела коснуться душа моя, то составляет отвратительную пищу мою.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
О, когда бы сбылось желание мое и чаяние мое исполнил Бог!
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
О, если бы благоволил Бог сокрушить меня, простер руку Свою и сразил меня!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Это было бы еще отрадою мне, и я крепился бы в моей беспощадной болезни, ибо я не отвергся изречений Святаго.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
Что за сила у меня, чтобы надеяться мне? и какой конец, чтобы длить мне жизнь мою?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Твердость ли камней твердость моя? и медь ли плоть моя?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Есть ли во мне помощь для меня, и есть ли для меня какая опора?
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
К страждущему должно быть сожаление от друга его, если только он не оставил страха к Вседержителю.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Но братья мои неверны, как поток, как быстро текущие ручьи,
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
которые черны от льда и в которых скрывается снег.
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
Когда становится тепло, они умаляются, а во время жары исчезают с мест своих.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Уклоняют они направление путей своих, заходят в пустыню и теряются;
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
смотрят на них дороги Фемайские, надеются на них пути Савейские,
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
но остаются пристыженными в своей надежде; приходят туда и от стыда краснеют.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Так и вы теперь ничто: увидели страшное и испугались.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Говорил ли я: дайте мне, или от достатка вашего заплатите за меня;
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
и избавьте меня от руки врага, и от руки мучителей выкупите меня?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Научите меня, и я замолчу; укажите, в чем я погрешил.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Как сильны слова правды! Но что доказывают обличения ваши?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Вы придумываете речи для обличения? На ветер пускаете слова ваши.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Вы нападаете на сироту и роете яму другу вашему.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Но прошу вас, взгляните на меня; буду ли я говорить ложь пред лицом вашим?
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Пересмотрите, есть ли неправда? пересмотрите, - правда моя.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Есть ли на языке моем неправда? Неужели гортань моя не может различить горечи?

< Ayubu 6 >