< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Respondens autem Iob, dixit:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
Utinam appenderentur peccata mea, quibus iram merui: et calamitas, quam patior, in statera.
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Quasi arena maris hæc gravior appareret: unde et verba mea dolore sunt plena:
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Quia sagittæ Domini in me sunt, quarum indignatio ebibit spiritum meum, et terrores Domini militant contra me.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Numquid rugiet onager cum habuerit herbam? aut mugiet bos cum ante præsepe plenum steterit?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Aut poterit comedi insulsum, quod non est sale conditum? aut potest aliquis gustare, quod gustatum affert mortem?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
Quæ prius nolebat tangere anima mea, nunc præ angustia, cibi mei sunt.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
Quis det ut veniat petitio mea: et quod expecto, tribuat mihi Deus?
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
Et qui cœpit, ipse me conterat: solvat manum suam, et succidat me?
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Et hæc mihi sit consolatio ut affligens me dolore, non parcat, nec contradicam sermonibus Sancti.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
Quæ est enim fortitudo mea ut sustineam? aut quis finis meus, ut patienter agam?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Nec fortitudo lapidum fortitudo mea, nec caro mea ænea est.
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Ecce, non est auxilium mihi in me, et necessarii quoque mei recesserunt a me.
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
Qui tollit ab amico suo misericordiam, timorem Domini derelinquit.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Fratres mei præterierunt me, sicut torrens qui raptim transit in convallibus.
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Qui timent pruinam, irruet super eos nix.
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
Tempore, quo fuerint dissipati, peribunt: et ut incaluerit, solventur de loco suo.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Involutæ sunt semitæ gressuum eorum: ambulabunt in vacuum, et peribunt.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Considerate semitas Thema, itinera Saba, et expectate paulisper.
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
Confusi sunt, quia speravi: venerunt quoque usque ad me, et pudore cooperti sunt.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Nunc venistis: et modo videntes plagam meam timetis.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Numquid dixi: Afferte mihi, et de substantia vestra donate mihi?
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
Vel, Liberate me de manu hostis, et de manu robustorum eruite me?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Docete me, et ego tacebo: et siquid forte ignoravi, instruite me.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Quare detraxistis sermonibus veritatis, cum e vobis nullus sit qui possit arguere me?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Ad increpandum tantum eloquia concinnatis, et in ventum verba profertis.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Super pupillum irruitis, et subvertere nitimini amicum vestrum.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Verumtamen quod cœpistis explete: præbete aurem, et videte an mentiar.
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Respondete obsecro absque contentione: et loquentes id quod iustum est, iudicate.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Et non invenietis in lingua mea iniquitatem, nec in faucibus meis stultitia personabit.

< Ayubu 6 >