< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Ijob respondis kaj diris:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
Se estus pesita mia ĉagreno, Kaj samtempe estus metita sur la pesilon mia suferado,
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Ĝi estus nun pli peza, ol la sablo ĉe la maroj; Pro tio miaj vortoj estas plenaj de plendo.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Ĉar la sagoj de la Plejpotenculo estas en mi, Ilian venenon trinkas mia spirito; La teruraĵoj de Dio direktiĝis sur min.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Ĉu krias sovaĝa azeno sur herbo? Ĉu bovo blekas kolere ĉe sia manĝaĵo?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Ĉu oni manĝas sengustaĵon sen salo? Ĉu havas guston la albumeno de ovo?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
Kion ne volis tuŝi mia animo, Tio nun estas abomeninde mia manĝaĵo.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
Ho, se mia peto plenumiĝus, Kaj se Dio donus al mi tion, kion mi esperas!
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
Ho, se Dio komencus kaj disbatus min, Donus liberecon al Sia mano kaj frakasus min!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Tio estus ankoraŭ konsolo por mi; Kaj mi ĝojus, se en la turmento Li ne kompatus, Ĉar mi ne forpuŝis ja la vortojn de la Sanktulo.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
Kio estas mia forto, ke mi persistu? Kaj kia estas mia fino, ke mi havu paciencon?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Ĉu mia forto estas forto de ŝtonoj? Ĉu mia karno estas kupro?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Mi havas ja nenian helpon, Kaj savo estas forpuŝita for de mi.
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
Al malfeliĉulo decas kompato de amiko, Eĉ se li forlasas la timon antaŭ la Plejpotenculo.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Miaj fratoj trompas kiel torento, Kiel akvaj fluegoj, kiuj pasas,
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Kiuj estas malklaraj pro glacio, En kiuj kaŝas sin neĝo;
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
En la tempo de degelo ili malaperas, En la tempo de varmego ili forŝoviĝas de sia loko.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Ili forklinas la direkton de sia vojo, Iras en la dezerton, kaj malaperas.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Serĉas ilin per sia rigardo la vojoj de Tema, Esperas je ili la karavanoj el Ŝeba;
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
Sed ili hontas pro sia fido; Ili aliras, kaj ruĝiĝas de honto.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Nun vi neniiĝis; Vi ekvidis teruraĵon, kaj ektimis.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Ĉu mi diris: Donu al mi, El via havaĵo donacu pro mi,
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
Savu min el la mano de premanto, Aŭ liberigu min el la mano de turmentantoj?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Instruu min, kaj mi eksilentos; Komprenigu al mi, per kio mi pekis.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Kial vi mallaŭdas pravajn vortojn? Kaj kion povas instrui la moralinstruanto el vi?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Ĉu vi intencas riproĉi pro vortoj? Sed paroloj de malesperanto iras al la vento.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Eĉ orfon vi atakus, Kaj sub via amiko vi fosus.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Nun, ĉar vi komencis, rigardu min; Ĉu mi mensogos antaŭ via vizaĝo?
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Rigardu denove, vi ne trovos malpiaĵon; Ripetu, vi trovos mian pravecon en la afero.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Ĉu estas peko sur mia lango? Ĉu mia palato ne komprenas tion, kio estas malbona?

< Ayubu 6 >