< Ayubu 3 >

1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Finally, Job spoke, and he cursed the day that he was born.
2 Kisha akasema:
He said,
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
“I wish that the day when I was born could be eradicated, and also the night when I was conceived.
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
I wish that the day when I was born would have been covered in darkness. I wish that God who is in heaven [MTY] would have forgotten about that day, and that the sun would not have shone on it.
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
I wish that thick/intense darkness would have filled that day, and that a black cloud would have come over it and blotted out all light and caused people to be terrified.
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
I wish that the night when I was conceived would be erased from the calendar, with the result that it would never again appear as one night in any month, and that it would not be included in any calendar.
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
I wish that no child would again be conceived on that night of the month [MET], and that no one would again be happy on that night.
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
I want those people who (curse/put evil spells on) days—those who know how to arouse/awaken the great sea monster—to curse that day.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
I wish that the stars that shone early in the morning on that day [after I was conceived] will not shine again. I want those stars to have wished in vain for light to shine; and that they would not have shone on that day.
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
[That was an evil day] because my mother was able to conceive; instead, I was born, and I have now experienced all these terrible things.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
“I wish that I had died [RHQ] when I was born— at the time I emerged from my mother’s womb.
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
I wish that my mother had not [RHQ] allowed me to live. I wish that she had not nursed me.
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
If I had died at the time when I was born, I would be asleep, resting peacefully [in the place where the dead people are].
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
I would be resting with kings whose [beautiful palaces] that they built are now in ruins (OR, who rebuilt [palaces] that had previously been destroyed), and I would be resting with their officials [who have also died].
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
I would be resting with princes who were wealthy, whose palaces were filled with gold and silver.
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
I wish that I had been buried like a child who died in its mother’s womb and never lived to see the light.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
After wicked people die, they do not cause any more troubles; those who are very tired now will rest.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
Those who were in prison rest peacefully [after they die]; they no longer have slave-drivers who curse them.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
Rich people and poor people are alike after they die, and those who were slaves are no longer controlled by their masters.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
(“Why does God allow those who are suffering greatly [like me] to continue to remain alive?/I do not understand why God allows those who are suffering greatly [like me] to continue to remain alive.) [RHQ] Why does he allow those who are very miserable/distressed to keep living [RHQ]?
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
They long/want to die, but they do not die. They desire to die more than people desire to find a hidden treasure.
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
When they finally die and are buried, they are very happy.
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
Those who do not know where they are [eventually] going when they die [RHQ], people whom God has forced [MET] to continue to live in misery, (it is not right that they continue to live./why do they continue to live?) [RHQ]
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
I continually cry very much; as a result, I cannot eat; and I can never stop groaning.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
Things that I always worried might happen to me, have happened to me; things that I always dreaded have happened to me.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
Now I have no peace [in my inner being], I have no peace; I cannot rest; instead, I have only troubles.”

< Ayubu 3 >