< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
But Job answered and said,
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
How hast thou helped [him that is] without power? [how] savest thou the arm [that hath] no strength?
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
How hast thou counseled [him that hath] no wisdom? and [how] hast thou abundantly declared the thing as it is?
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
To whom hast thou uttered words? and whose spirit came from thee?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
Dead [things] are formed from under the waters, and the inhabitants thereof.
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
Hell [is] naked before him, and destruction hath no covering. (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
He stretcheth out the north over the empty place, [and] hangeth the earth upon nothing.
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
He bindeth up the waters in his thick clouds; and the cloud is not rent under them.
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
He holdeth back the face of [his] throne, [and] spreadeth his cloud upon it.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
He hath encompassed the waters with bounds, until the day and night come to an end.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
The pillars of heaven tremble and are astonished at his reproof.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
He divideth the sea by his power, and by his understanding he smiteth through the proud.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
By his spirit he hath garnished the heavens; his hand hath formed the crooked serpent.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Lo, these [are] parts of his ways: but how little a portion is heard of him? but the thunder of his power who can understand?

< Ayubu 26 >