< Yeremia 6 >

1 “Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini! Kimbieni kutoka Yerusalemu! Pigeni tarumbeta katika Tekoa! Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu! Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini, na uharibifu wa kutisha.
Synowie Beniamina, zgromadźcie się, by uciekać z Jerozolimy, zadmijcie w trąbę w Tekoa, wznieście znak nad Bet-Kerem. Z północy bowiem nadchodzi nieszczęście i wielkie zniszczenie.
2 Nitamwangamiza Binti Sayuni, aliye mzuri sana na mwororo.
Przyrównałem córkę Syjonu do pięknej, rozkosznej [panny];
3 Wachungaji pamoja na makundi yao watakuja dhidi yake; watapiga mahema yao kumzunguka, kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”
Do niej przyjdą pasterze wraz ze swymi trzodami; rozbiją naprzeciwko niej namioty dokoła, każdy będzie paść w swoim miejscu.
4 “Jiandaeni kwa vita dhidi yake! Inukeni tumshambulie mchana! Lakini, ole wetu, mchana unaisha, na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
Ogłoście przeciwko niej wojnę, wstańcie, wyruszymy w południe. Biada nam, bo dzień się kończy, bo wydłużają się cienie wieczorne!
5 Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku, na kuharibu ngome zake!”
Wstańcie, wtargniemy w nocy i zburzmy jej pałace.
6 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kateni miti mjenge boma kuzunguka Yerusalemu. Mji huu ni lazima uadhibiwe, umejazwa na uonevu.
Tak bowiem mówi PAN zastępów: Narąbcie drzewa i usypcie wał przeciw Jerozolimie. Jest to miasto, które ma być ukarane; pośrodku niej [jest] całkowity ucisk.
7 Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake, ndivyo anavyomwaga uovu wake. Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake, ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima.
Jak źródło wylewa swe wody, tak ona wylewa swoją niegodziwość. Słychać w niej ucisk i spustoszenie, [mam] przed sobą nieustannie cierpienie i bicie.
8 Pokea onyo, ee Yerusalemu, la sivyo nitageukia mbali nawe na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa, asiweze mtu kuishi ndani yake.”
Przyjmij upomnienie, Jerozolimo, aby moja dusza nie odstąpiła od ciebie, bym cię nie zamienił w pustkowie, ziemię bezludną.
9 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Wao na wayakusanye mabaki ya Israeli kwa uangalifu kama kwenye mzabibu; pitisha mkono wako kwenye matawi tena, kama yeye avunaye zabibu.”
Tak mówi PAN zastępów: Wyzbierają resztkę Izraela aż do grona, jak winorośl. Sięgaj swoją ręką do kosza, jak zbieracz.
10 Niseme na nani na kumpa onyo? Ni nani atakayenisikiliza mimi? Masikio yao yameziba, kwa hiyo hawawezi kusikia. Neno la Bwana ni chukizo kwao, hawalifurahii.
Do kogo będę mówić i kogo ostrzegę, aby słyszeli? Oto ich uszy są nieobrzezane, tak że nie mogą słuchać. Oto słowo PANA uważają za hańbę i nie mają w nim upodobania.
11 Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana, nami siwezi kuizuia. “Wamwagie watoto walioko barabarani, na juu ya vijana waume waliokusanyika; mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake, hata nao wazee waliolemewa na miaka.
Dlatego jestem pełen zapalczywości PANA, zamęczam się, aby [ją] powstrzymać. Wyleję ją zarówno na dzieci na ulicy, [jak] i na gromadę młodzieńców, gdyż będą pojmani – mąż z żoną, starzec z podeszłym w wieku.
12 Nyumba zao zitapewa watu wengine, pamoja na mashamba yao na wake zao, nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya wale waishio katika nchi,” asema Bwana.
Ich domy przypadną innym, także ich pola i żony, gdyż wyciągnę swoją rękę na mieszkańców tej ziemi, mówi PAN;
13 “Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata faida zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
Gdyż od najmniejszego z nich aż do największego – wszyscy oddani są chciwości i od proroka aż do kapłana – wszyscy popełniają oszustwo.
14 Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, ‘Amani, amani,’ wakati hakuna amani.
I leczą rany córki mego ludu [tylko] powierzchownie, mówiąc: Pokój, pokój! Ale nie ma pokoju.
15 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo; hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini nitakapowaadhibu,” asema Bwana.
Czy zawstydzili się, że popełnili obrzydliwość? Bynajmniej, wcale nie wstydzili się ani nie potrafili rumienić. Dlatego upadną wśród tych, którzy mają upaść. W czasie gdy ich nawiedzę, upadną, mówi PAN.
16 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Simama kwenye njia panda utazame, ulizia mapito ya zamani, ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’
Tak mówi PAN: Stańcie na drogach, spójrzcie i pytajcie o stare ścieżki, gdzie jest ta dobra droga – i idźcie nią, a znajdziecie odpoczynek dla waszej duszy. Lecz powiedzieli: Nie pójdziemy.
17 Niliweka walinzi juu yenu na kusema, ‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’ Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’
I ustanowiłem nad wami stróżów, [mówiąc]: Słuchajcie głosu trąby! Wtedy powiedzieli: Nie będziemy słuchać.
18 Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa, angalieni, enyi mashahidi, lile litakalowatokea.
Dlatego słuchajcie, narody; poznaj, o zgromadzenie, co się wśród nich dzieje.
19 Sikia, ee nchi: Ninaleta maafa juu ya watu hawa, matunda ya mipango yao, kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu na wameikataa sheria yangu.
Słuchaj, ziemio! Oto sprowadzę nieszczęście na ten lud – owoc jego myśli, gdyż nie słuchał moich słów ani mego prawa, ale je odrzucił.
20 Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba, au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali? Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki, dhabihu zako hazinifurahishi mimi.”
Na cóż mi kadzidło z Szeby i cynamon wonny i wyborny z dalekiej ziemi? Wasze całopalenia nie są [dla mnie] przyjemne i wasze ofiary nie podobają mi się.
21 Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa. Baba na wana wao watajikwaa juu yake, majirani na marafiki wataangamia.”
Dlatego tak mówi PAN: Oto kładę przed tym ludem przeszkody, o które potykać się będą ojcowie wraz z synami; sąsiad i jego przyjaciel zginą.
22 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Tazama, jeshi linakuja kutoka nchi ya kaskazini, taifa kubwa linaamshwa kutoka miisho ya dunia.
Tak mówi PAN: Oto nadciągnie lud z ziemi północnej, wielki naród powstanie z krańców ziemi.
23 Wamejifunga pinde na mkuki, ni wakatili na hawana huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao. Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Sayuni.”
Łuk i włócznię trzymają, są okrutni i bezlitośni. Ich głos huczy jak morze i na koniach jeżdżą, gotowi jak jeden mąż do walki przeciwko tobie, o córko Syjonu!
24 Tumesikia taarifa zao, nayo mikono yetu imelegea. Uchungu umetushika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Gdy usłyszeliśmy wieść o nich, nasze ręce osłabły, ogarnęły nas trwoga i ból, jak u rodzącej.
25 Usitoke kwenda mashambani au kutembea barabarani, kwa kuwa adui ana upanga, na kuna vitisho kila upande.
Nie wychodźcie na pole i nie idźcie po drodze, bo miecz wroga [i] strach dokoła.
26 Enyi watu wangu, vaeni magunia mjivingirishe kwenye majivu, ombolezeni kwa kilio cha uchungu kama amliliaye mwana pekee, kwa maana ghafula mharabu atatujia.
Córko mojego ludu, przepasz się worem i tarzaj się w popiele. Urządź sobie żałobę [jak po] jedynaku, gorzką żałobę, bo nagle spadnie na nas niszczyciel.
27 “Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma, nao watu wangu kama mawe yenye madini, ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao.
Ustanowiłem cię basztą i wieżą wśród mego ludu, abyś poznał i zbadał jego drogi.
28 Wote ni waasi sugu, wakienda huku na huko kusengenya. Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda upotovu.
Wszyscy są ogromnie krnąbrni, postępują jak oszczercy. [Są jak] miedź i żelazo; wszyscy są skażeni.
29 Mivuo inavuma kwa nguvu, kinachoungua kwa huo moto ni risasi, lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure; waovu hawaondolewi.
Miech uległ zużyciu, ołów od ognia niszczeje; na próżno przetapia [go] hutnik, bo źli nie zostali oddaleni.
30 Wanaitwa fedha iliyokataliwa, kwa sababu Bwana amewakataa.”
Będą nazwani srebrem odrzuconym, bo PAN ich odrzucił.

< Yeremia 6 >