< Yeremia 49 >

1 Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
Contre les enfants d'Ammon. Ainsi parle Yahweh: Israël n'a-t-il pas de fils, n'a-t-il pas d'héritier? Pourquoi Melchom a-t-il pris possession de Gad, et son peuple s'est-il installé dans ses villes?
2 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
C'est pourquoi voici que des jours viennent, — oracle de Yahweh, où je ferai retentir à Rabba des enfants d'Ammon le cri de guerre. Elle deviendra un monceau de ruines, et ses filles seront livrées au feu, et Israël héritera de ceux qui ont hérité de lui, — oracle de Yahweh.
3 “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
Lamente-toi, Hésébon, car Haï a été saccagée; poussez des cris, filles de Rabbah, ceignez-vous de sacs, lamentez-vous; errez le long des clôtures; car Melchom s'en va en exil, et avec lui, ses prêtres et ses chefs.
4 Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
Pourquoi te glorifier de tes vallées? — elle est riche, ta vallée! — fille rebelle, toi qui te confies dans tes trésors, disant: " Qui oserait venir contre moi? "
5 Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
Voici que j'amène contre toi la terreur, — oracle du Seigneur Yahweh des armées, de tous les alentours; vous serez chassés, chacun droit devant soi, et personne ne ralliera les fuyards.
6 “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
Mais après cela, je ramènerai les captifs des enfants d'Ammon, — oracle de Yahweh.
7 Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
Contre Edom. Ainsi parle Yahweh, des armées: N'y a-t-il plus de sagesse en Théman? Les avisés sont-ils à bout de conseils? Leur sagesse s'est-elle évanouie?
8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
Fuyez, retournez sur vos pas, blottissez-vous, habitants de Dédan car j'amènerai sur Esaü la ruine, au temps où je le visite.
9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
Si des vendangeurs viennent chez toi, ils ne laissent rien à grappiller; si ce sont des voleurs de nuit, ils pillent tout leur soûl.
10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
Car c'est moi qui ai mis à nu Esaü et découvert ses retraites, et il ne peut plus se cacher; sa race est ravagé, ses frères, ses voisins, — et il n'est plus.
11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
Abandonne tes orphelins, c'est moi qui les ferai vivre, et que tes veuves se confient en moi!
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
Car ainsi parle Yahweh: Voici que ceux qui ne devaient pas boire cette coupe la boiront sûrement; et toi, tu en serais tenu quitte? Non, tu n'en seras pas tenu quitte, tu la boiras sûrement!
13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
Car je l'ai juré par moi-même, — oracle de Yahweh: Bosra sera un sujet d'étonnement et d'opprobre, un lieu désert et maudit, et toutes ses villes seront des ruines à jamais.
14 Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
J'en ai appris de Yahweh la nouvelle, et un messager a été envoyé parmi les nations: " Rassemblez-vous et marchez contre lui! Levez-vous pour le combat! "
15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
Car voici que je t'ai rendu petit parmi les nations, méprisé parmi les hommes.
16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
La terreur que tu inspirais t'a égaré, ainsi que la fierté de ton cœur, toi qui habites le creux des rochers, qui occupes le sommet de la colline. Mais quand tu élèverais ton aire comme l'aigle, de là je te ferai descendre, — oracle de Yahweh.
17 “Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
Edom sera un sujet d'étonnement; tous les passants s'étonneront, et siffleront à la vue de toutes ses plaies.
18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Ce sera comme la catastrophe de Sodome, de Gomorrhe et des villes voisines, dit Yahweh; personne n'y habitera, aucun fils de l'homme n'y séjournera.
19 “Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Pareil à un lion, voici qu'il monte des halliers du Jourdain au pâturage perpétuel; soudain j'en ferai fuir Edom, et j'y établirai celui que j'ai choisi. Car qui est semblable à moi? Qui me provoquerait, et quel est le berger qui me tiendrait tête?
20 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Ecoutez donc la résolution qu'a prise Yahweh contre Edom, et les desseins qu'il a médités contre les habitants de Théman: Oui, on les entraînera comme de faibles brebis; oui, leur pâturage en sera dans la stupeur.
21 Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
Au bruit de leur chute, la terre tremble; le bruit de leur voix se fait entendre jusqu'à la mer Rouge.
22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Voici qu'il monte et prend son vol comme l'aigle, il étend ses ailes sur Bosra; et le cœur des guerriers d'Edom est en ce jour comme le cœur d'une femme en travail.
23 Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
Contre Damas. Hamath et Arphad sont dans la confusion, parce qu'elles ont reçu une mauvaise nouvelle; elles se fondent de peur; c'est la mer en tourmente, qui ne peut s'apaiser.
24 Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Damas est sans force, elle se tourne pour fuir, et l'effroi s'empare d'elle; l'angoisse et les douleurs la saisissent, comme une femme qui enfante.
25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
A quel point n'est-elle pas abandonnée, la ville glorieuse, la cité de délices, de joie!
26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Aussi ses jeunes gens tomberont sur ses places, ainsi que tous ses hommes de guerre; ils périront en ce jour-là, — oracle de Yahweh des armées.
27 “Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
J'allumerai un feu dans les murs de Damas, et il dévorera les palais de Ben-Hadad.
28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
Contre Cédar et les royaumes de Hasor, que frappa Nabuchodonosor, roi de Babylone. Ainsi parle Yahweh: Debout! Marchez contre Cédar, exterminez les fils de l'Orient!
29 Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
Qu'on prenne leurs tentes et leurs troupeaux! Qu'on leur enlève leurs tentures, tous leurs bagages et leurs chameaux! Et qu'on leur crie: Terreur de toutes parts!
30 “Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
Sauvez-vous, fuyez de toutes vos forces, blottissez-vous, habitants de Hasor! — oracle de Yahweh. Car Nabuchodonosor, roi de Babylone, a formé contre vous un dessein, il a conçu un projet contre vous.
31 “Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
Debout! Marchez contre un peuple tranquille, en assurance dans sa demeure, — oracle de Yahweh, qui n'a ni portes ni barres, qui vit à l'écart.
32 Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
Leurs chameaux seront votre butin, et la multitude de leurs troupeaux vos dépouilles. Je les disperserai à tous les vents, ces hommes aux tempes rasées, et de tous côtés je ferai venir sur leur ruine, — oracle de Yahweh.
33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
Et Hasor deviendra un repaire de chacals, une solitude pour toujours; personne n'y demeurera, aucun fils d'homme n'y séjournera.
34 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
La parole de Yahweh qui fut adressée à Jérémie, le prophète, pour Élam, au commencement du règne de Sédécias, roi de Juda, en ces termes:
35 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
Ainsi parle Yahweh des armées: Voici que je vais briser l'arc d'Élam, principe de sa force.
36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
Je ferai venir sur Élam quatre vents, des quatre coins du ciel, et je le disperserai à tous ces vents; et il n'y aura pas une nation où n'arrivent pas des fugitifs d'Élam.
37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
Je ferai trembler Élam devant ses ennemis, et devant ceux qui en veulent à sa vie. Et j'amènerai sur eux des malheurs, le feu de mon ardente colère, — oracle de Yahweh. Et j'enverrai après eux l'épée, jusqu'à ce que je les aie anéantis.
38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
Je placerai mon trône en Élam, et j'en exterminerai roi et chefs, — oracle de Yahweh.
39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.
Mais à la fin des jours, je ramènerai les captifs d'Élam, — oracle de Yahweh.

< Yeremia 49 >