< Yeremia 48 >

1 Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
Przeciw Moabowi tak mówi PAN zastępów, Bóg Izraela: Biada [miastu] Nebo, bo jest spustoszone. Kiriataim jest pohańbione i zdobyte. Misgab jest zawstydzone i przerażone.
2 Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
Nie będzie już chwały dla Moabu, w Cheszbonie obmyślono przeciwko niemu nieszczęście: Chodźcie, wytępmy go spośród narodów. I ty, Madmenie, zostaniesz wykorzeniony, miecz będzie cię ścigał.
3 Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
Głos krzyku z Choronaim, spustoszenie i wielkie zniszczenie.
4 Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
Moab jest zmiażdżony, usłyszy się krzyk jego małych.
5 Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
Będzie bowiem ciągły płacz przy wchodzeniu do Luchit, a przy schodzeniu do Choronaim wrogowie usłyszą krzyk nad zniszczeniem.
6 Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
Uciekajcie, ratujcie swoje życie i bądźcie jak wrzos na pustyni.
7 Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
Ponieważ pokładasz ufność w swoich dziełach i skarbach, ty też będziesz zdobyty. Kemosz pójdzie do niewoli wraz ze swoimi kapłanami i książętami.
8 Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
Niszczyciel przyjdzie do każdego miasta i [żadne] miasto nie ocaleje. Dolina też zginie i równina będzie spustoszona, jak mówi PAN.
9 Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
Dajcie skrzydła Moabowi, niech szybko uleci, bo jego miasta zostaną spustoszone, tak że nie będzie [w nich] mieszkańców.
10 “Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
Przeklęty, kto wykonuje dzieło PANA podstępnie; przeklęty także, kto swój miecz powstrzymuje od krwi.
11 “Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
Moab miał pokój od swojej młodości, spoczywał na swoich drożdżach i nie był przelewany z naczynia do naczynia, nie poszedł do niewoli. Dlatego zachował się w nim jego smak i jego zapach się nie zmienił.
12 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
Dlatego oto nadchodzą dni, mówi PAN, że poślę na niego najeźdźców, którzy go uprowadzą, a opróżnią jego naczynia i potłuką jego dzbany.
13 Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
I Moab będzie się wstydzić Kemosza, jak dom Izraela wstydził się Betel, jego nadziei.
14 “Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
Jakże możecie mówić: Jesteśmy mocnymi i dzielnymi wojownikami w walce?
15 Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Moab jest zburzony i wyszedł ze swoich miast, a wyborni jego młodzieńcy pójdą na rzeź, mówi Król, jego imię to PAN zastępów.
16 “Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
Zbliża się klęska Moabu, jego nieszczęście nadchodzi spiesznie.
17 Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
Opłakujcie go, wszyscy, jego [sąsiedzi]; wszyscy, którzy znacie jego imię, mówcie: Jakże się złamała mocna laska i berło ozdobne!
18 “Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
Zejdź ze swej chwały i siądź w pragnieniu, córko, mieszkanko Dibonu! Bo niszczyciel Moabu nadciągnie przeciwko tobie, rozrzuci twoje twierdze.
19 Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
Stań na drodze i przypatrz się uważnie, mieszkanko Aroeru! Spytaj tego, który ucieka, i tej, która uchodzi: Co się dzieje?
20 Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
Moab jest zawstydzony, bo jest rozgromiony; zawódźcie i krzyczcie, opowiadajcie w Arnon, że Moab jest spustoszony.
21 Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
Sąd nadszedł na ziemię tej równiny, na Cholon, na Jahazę i na Mefaat;
22 katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
Na Dibon, na Nebo i na Bet-Dyblataim;
23 katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
Na Kiriataim, na Betgamul i na Bet-Meon.
24 katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
Na Keriot, na Bosrę i na wszystkie miasta ziemi Moabu, dalekie i bliskie.
25 Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
Róg Moabu został odcięty i jego ramię złamane, mówi PAN.
26 “Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
Upójcie go, ponieważ wynosił się przeciw PANU. Niech Moab tarza się w swoich wymiocinach i niech również stanie się pośmiewiskiem.
27 Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
Czy Izrael nie był dla ciebie pośmiewiskiem? Czy złapano go wśród złodziei? Ilekroć bowiem mówisz o nim, skaczesz [z radości].
28 Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
Opuszczajcie miasta i zamieszkajcie na skale, mieszkańcy Moabu! Bądźcie jak gołębica, która się gnieździ na ścianach gardzieli urwiska.
29 “Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
Słyszeliśmy o pysze Moabu, że jest niezmiernie pyszny, o jego zuchwałości, o jego zarozumiałości, o jego dumie i o wyniosłości jego serca.
30 Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
Znam jego gniew, mówi PAN, lecz mu się nie poszczęści; jego kłamstwa nie dojdą do skutku.
31 Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
Dlatego nad Moabem będę zawodził, nad całym Moabem będę wołał, i nad ludźmi z Kir-Cheres [moje serce] będzie wzdychało.
32 Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
Płaczę nad tobą, jak opłakiwano Jazer, winorośli Sibmy! Twoje latorośle sięgają aż za morze, dochodzą aż do morza Jazer. Na twoje letnie owoce i na twoje winobranie wpadł niszczyciel.
33 Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
I zniknęły wesele i radość z urodzajnych pól i z ziemi Moabu, i sprawiłem, że wino się skończyło z pras; nie będą go tłoczyć wśród okrzyków, a ich okrzyk nie będzie okrzykiem.
34 “Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
Od krzyku Cheszbonu aż do Eleale i aż do Jahazy wydają swój głos, z Soaru aż do Choronaim, [jak] trzyletnia jałówka; bo wody Nimrim też staną się spustoszeniem.
35 Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
I sprawię, mówi PAN, że już nie będzie w Moabie nikogo, kto składa ofiarę na wyżynach lub pali kadzidło swoim bogom.
36 “Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
Dlatego moje serce będzie jęczeć nad Moabem jak flet; nad ludźmi z Kir-Cheres moje serce zawodzi jak flet, gdyż ich zgromadzony dobytek wniwecz się obrócił.
37 Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
Na każdej bowiem głowie będzie łysina i każda broda zostanie ogolona. Na wszystkich rękach [będą] nacięcia i na biodrach wory.
38 Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
Na wszystkich dachach Moabu i na jego ulicach tylko powszechny lament, bo rozbiłem Moab jak naczynie nieużyteczne, mówi PAN.
39 “Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
Będą zawodzić, [mówiąc]: Jakże jest rozbity! Jak haniebnie uciekł Moab! Moab będzie pośmiewiskiem i postrachem dla wszystkich, którzy są dokoła niego.
40 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
Tak bowiem mówi PAN: Oto [wróg] jak orzeł przyleci i rozciągnie swe skrzydła nad Moabem.
41 Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Keriot jest zdobyty i twierdze są wzięte, a serce mocarzy Moabu w tym dniu będzie jak serce rodzącej kobiety.
42 Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
Moab zostanie zniszczony, przestanie być ludem, bo wynosił się przeciwko PANU.
43 Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
Strach, dół i sidło nad tobą, który mieszkasz w Moabie, mówi PAN.
44 “Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
Kto ucieknie przed strachem, wpadnie w dół, a kto wyjdzie z dołu, wpadnie w sidła. Sprowadzę bowiem na niego, na Moab, rok jego nawiedzenia, mówi PAN.
45 “Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
W cieniu Cheszbonu zatrzymali się ci, którzy uciekali przed przemocą. Ale ogień wyjdzie z Cheszbonu i płomień ze środka Sichona i pożre krańce Moabu, i czaszkę tych, którzy czynią zgiełk.
46 Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
Biada tobie, Moabie! Ginie lud Kemosza, bo twoi synowie zostali zabrani do niewoli i twoje córki – na wygnanie.
47 “Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.
Odwrócę jednak niewolę Moabu w dniach ostatecznych, mówi PAN. Dotąd sąd nad Moabem.

< Yeremia 48 >