< Yeremia 34 >

1 Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
King Nebuchadnezzar of Babylon came with the armies of all the kingdoms that he ruled, and they fought against Jerusalem and the other towns [in Judah]. At that time, Yahweh gave me this message:
2 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
“Go to Zedekiah the King of Judah, and say to him, ‘This is what Yahweh, the God whom we Israelis [worship], says: “I am about to enable the army of the King of Babylon to capture this city, and they will burn it down.
3 Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.
You will not escape from them; they will capture you and take you to the king of Babylon. And [then] they will take you to Babylon.”’
4 “‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga,
But King Zedekiah, listen to this that Yahweh has promised: ‘You will not be killed in a battle [MTY];
5 utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’”
you will die peacefully. [When you die], people will burn incense to honor/remember you just as they did for your ancestors who were kings before you became king. They will mourn for you, crying, “We are very sad that our king is dead!” I, Yahweh, promise that will happen.’”
6 Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu,
[So] I took that message to King Zedekiah.
7 wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.
At that time the army of Babylonia had surrounded Jerusalem and Lachish and Azekah. Those [three] cities were the only cities in Judah that had high walls around them that still had not been captured.
8 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa.
King Zedekiah had decreed that the people must free their slaves.
9 Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa.
[He decreed that] the people must free their Hebrew slaves, [both the] men slaves and the women [slaves]. No one would be allowed to force a fellow Jew to [continue to] be his slave.
10 Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru.
The officials and the rest of the people had obeyed [what the king decreed],
11 Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.
but later they changed their minds. They forced the men and women whom they had freed to become their slaves again.
12 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
[So] Yahweh gave me this message [to tell to them]:
13 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema,
“I, Yahweh, the God whom you Israelis [say you belong to], (made an agreement with/gave this command to) your ancestors [long ago], when I rescued them from being slaves in Egypt.
14 ‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
I told them that they must free all their Hebrew slaves after the slaves had worked for them for six years. But your ancestors did not pay any attention to what I said.
15 Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu.
Recently, you obeyed my command and stopped doing what was wrong and did what was right. You made a solemn agreement at my temple [that you would free your slaves], and [then] you freed them.
16 Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.
But now you have disregarded what you solemnly promised, and you have shown contempt for what I [MTY] said by taking back the women and men whom you had freed and said they could live wherever they wanted to. [Now] you have forced them to be your slaves again.
17 “Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia.
Therefore, this is what [I], Yahweh, say: ‘Because you have not obeyed me by freeing your fellow Israelis, I will free you to [be destroyed by] the swords [of your enemies] and by famines and diseases. All the nations of the earth will be horrified because of [what happens to] you.
18 Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama.
Because you have disregarded what I said in my agreement with you, I will do to you just like you did to the calves that you cut in half to show that you would surely do what you solemnly promised that you would do. I will [enable your enemies to] cut you into pieces, you officials of Judah and you officials of Jerusalem, and you officials in the palace, and you priests and all you common people. I will do that because you have disregarded what you solemnly promised [about freeing your slaves].
19 Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama,
20 nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
I will enable your enemies to capture you, and they will kill you. And your bodies will be food for vultures and wild animals.
21 “Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu.
I will enable the army of the king of Babylon to capture King Zedekiah and his officials. Although the king of Babylon and his army have left Jerusalem [for a short time],
22 Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”
I will summon them back again. [This time], they will fight against this city and capture it and burn it down. I will make [sure] that all the towns in Judah are destroyed, [with the result that] no one will live there [any more].’”

< Yeremia 34 >