< Yeremia 29 >

1 Haya ndiyo maneno ya ile barua ambayo nabii Yeremia aliituma kutoka Yerusalemu kwenda kwa wazee waliobaki miongoni mwa wale waliohamishwa, na kwa makuhani, manabii na watu wengine wote ambao Nebukadneza alikuwa amewachukua kwenda uhamishoni Babeli kutoka Yerusalemu.
These are the words in the scroll that Jeremiah the prophet sent out from Jerusalem to the remaining elders among the captives and to the priests, prophets, and all the people that Nebuchadnezzar exiled from Jerusalem to Babylon.
2 (Hii ilikuwa ni baada ya Mfalme Yekonia na malkia mamaye, maafisa wa mahakama, viongozi wa Yuda na wa Yerusalemu, mafundi na wahunzi kwenda uhamishoni kutoka Yerusalemu.)
This was after Jehoiachin the king, the queen mother, and the high officials, the leaders of Judah and Jerusalem, and the craftsmen had been sent away from Jerusalem.
3 Barua ilikabidhiwa kwa Elasa mwana wa Shafani, na kwa Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia mfalme wa Yuda aliwatuma kwa Mfalme Nebukadneza huko Babeli. Barua yenyewe ilisema:
He sent this scroll by the hand of Elasah son of Shapan and Gemariah son of Hilkiah whom Zedekiah, king of Judah, had sent to Nebuchadnezzar king of Babylon.
4 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, awaambialo wale wote niliowapeleka kutoka Yerusalemu kwenda uhamishoni Babeli:
The scroll said, “Yahweh of hosts, God of Israel, says this to all the captives whom I caused to be exiled from Jerusalem to Babylon,
5 “Jengeni nyumba na mstarehe, pandeni bustani na mle mazao yake.
'Build houses and live in them. Plant gardens and eat their fruit.
6 Oeni wake na mzae wana na binti, waozeni wana wenu wake, nanyi watoeni binti zenu waolewe, ili nao pia wazae wana na binti. Ongezekeni idadi yenu huko, wala msipungue.
Take wives and give birth to sons and daughters. Then take wives for your sons, and give your daughters to husbands. Let them give birth to sons and daughters and increase there so you do not become too few.
7 Pia tafuteni amani na mafanikio ya mji ambamo nimewapeleka uhamishoni. Mwombeni Bwana kwa ajili ya mji huo, kwa sababu ukistawi, ninyi pia mtastawi.”
Seek the peace of the city where I have caused you to be exiled, and intercede with me on its behalf since there will be peace for you if it is at peace.'
8 Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Msikubali manabii na wabashiri walioko miongoni mwenu wawadanganye. Msisikilize ndoto ambazo mmewatia moyo kuota.
For Yahweh of hosts, God of Israel, says this, 'Do not let your prophets who are in your midst and your diviners deceive you, and do not listen to the dreams that you yourselves are having.
9 Wanawatabiria ninyi uongo kwa jina langu. Sikuwatuma,” asema Bwana.
For they are prophesying deceitfully to you in my name. I did not send them—this is Yahweh's declaration.'
10 Hili ndilo asemalo Bwana: “Miaka sabini itakapotimia kwa ajili ya Babeli, nitakuja kwenu na kutimiza ahadi yangu ya rehema ya kuwarudisha mahali hapa.
For Yahweh says this, 'When Babylon has ruled you for seventy years, I will help you and carry out my good word for you to bring you back to this place.
11 Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,” asema Bwana, “ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo.
For I myself know the plans that I have for you—this is Yahweh's declaration—plans for peace and not for disaster, to give you a future and a hope.
12 Kisha mtaniita, na mtakuja na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Then you will call to me, and go and pray to me, and I will listen to you.
13 Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
For you will seek me and find me, since you will seek me with all your heart.
14 Nitaonekana kwenu,” asema Bwana, “nami nitawarudisha watu wenu waliotekwa. Nitawakusanya kutoka mataifa yote na mahali pote nilipokuwa nimewafukuzia, nami nitawarudisha mahali ambapo nilikuwa nimewatoa walipochukuliwa uhamishoni,” asema Bwana.
Then I will be found by you—this is Yahweh's declaration—and I will bring back your fortunes; I will gather you from all the nations and places where I scattered you—this is Yahweh's declaration—for I will bring you back to the place from where I caused you to be exiled.'
15 Mnaweza mkasema, “Bwana ameinua manabii kwa ajili yetu huku Babeli,”
Since you said that Yahweh has raised up prophets for us in Babylon,
16 lakini hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme aketiaye kiti cha enzi cha Daudi, na watu wa kwenu wote wanaobaki katika mji huu, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni.
Yahweh says this to the king who sits on the throne of David and to all the people who are staying in that city, your brothers who have not gone out with you into captivity—
17 Naam, hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nitatuma upanga, njaa na tauni dhidi yao, nami nitawafanya kuwa kama tini dhaifu zile ambazo ni mbovu sana zisizofaa kuliwa.
Yahweh of hosts says this, 'See, I am about to send sword, famine, and disease on them. For I will make them like rotten figs that are too bad to be eaten.
18 Nitawafukuza kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawafanya kitu cha kuchukiza sana kwa falme zote za dunia, na kuwa kitu cha laana na cha kuogofya, cha dharau na kukemewa, miongoni mwa mataifa yote nitakakowafukuzia.
Then I will pursue them with sword, famine, and plague and make them a horrible sight to all the kingdoms on earth—a horror, an object of curses and hissing, and a shameful thing among all the nations where I scattered her.
19 Kwa kuwa hawakuyasikiliza maneno yangu,” asema Bwana, “maneno ambayo niliwatumia tena na tena kupitia watumishi wangu manabii. Wala ninyi watu wa uhamisho hamkusikiliza pia,” asema Bwana.
This is because they did not listen to my word—this is Yahweh's declaration—that I sent out to them through my servants the prophets. I repeatedly sent them, but you would not listen—this is Yahweh's declaration.'
20 Kwa hiyo, sikieni neno la Bwana, enyi nyote mlio uhamishoni, niliowapeleka Babeli kutoka Yerusalemu.
So you yourselves listen to the word of Yahweh, all you exiles whom he has sent out from Jerusalem to Babylon,
21 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya, na Sedekia mwana wa Maaseya, wanaowatabiria uongo kwa jina langu: “Nitawatia mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atawaua mbele ya macho yenu hasa.
'Yahweh of hosts, God of Israel, says this about Ahab son of Kolaiah and Zedekiah son of Maaseiah, who prophesy falsely to you in my name: See, I am about to put them into the hand of Nebuchadnezzar king of Babylon. He will kill them before your eyes.
22 Kwa ajili yao, watu wote wa uhamisho kutoka Yuda walioko Babeli watatumia laana hii: ‘Bwana na akutendee kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwachoma kwa moto.’
Then a curse will be spoken about these persons by all the captives of Judah in Babylon. The curse will say: May Yahweh make you like Zedekiah and Ahab, whom the king of Babylon roasted in fire.
23 Kwa kuwa wamefanya mambo maovu kabisa katika Israeli, wamezini na wake za majirani zao, tena kwa Jina langu wamesema uongo, mambo ambayo sikuwaambia kuyafanya. Nami nayajua haya, na ni shahidi wa jambo hilo,” asema Bwana.
This will happen because of the shameful things they did in Israel when they committed adultery with their neighbor's wives and declared false words in my name, things that I never commanded them to say. For I am the one who knows; I am the witness—this is Yahweh's declaration.'”
24 Mwambie Shemaya Mnehelami,
“About Shemaiah the Nehelamite, say this:
25 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ulituma barua kwa jina lako mwenyewe kwa watu wote wa Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa kuhani Maaseya na kwa makuhani wengine wote. Ulimwambia Sefania,
'Yahweh of hosts, God of Israel, says this: Because you sent out letters in your own name to all the people in Jerusalem, to Zephaniah son of Maaseiah the priest, and to all the priests, and said,
26 ‘Bwana amekuweka wewe uwe kuhani badala ya Yehoyada ili uwe msimamizi wa nyumba ya Bwana. Unapaswa kufunga kwa mikatale na mnyororo wa shingoni mwendawazimu yeyote anayejifanya nabii.
“Yahweh has made you priest instead of Jehoiada the priest, for you to be in charge of Yahweh's house. You are in control of all the people who rave and make themselves into prophets. You should put them in stocks and chains.
27 Kwa nini basi hukumkemea Yeremia Mwanathothi, aliyejifanya kama nabii miongoni mwenu?
So now, why have you not rebuked Jeremiah of Anathoth, who makes himself into a prophet against you?
28 Ametutumia ujumbe huu huku Babeli: Mtakuwako huko muda mrefu. Kwa hiyo jengeni nyumba mkakae; pandeni mashamba na mle mazao yake.’”
For he has sent to us in Babylon and said, 'It will be a long time. Build houses and live in them, and plant gardens and eat their fruit.”'”
29 Kuhani Sefania, hata hivyo, akamsomea nabii Yeremia ile barua.
Zephaniah the priest read this letter in the hearing of Jeremiah the prophet.
30 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Then the word of Yahweh came to Jeremiah, saying,
31 “Tuma ujumbe huu kwa watu wote walio uhamishoni: ‘Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, hata ingawa sikumtuma, naye amewafanya kuamini uongo,
“Send word to all the exiles and say, 'Yahweh says this about Shemaiah the Nehelamite: Because Shemaiah has prophesied to you when I myself did not send him, and he has led you to believe lies,
32 hili ndilo Bwana asemalo: Hakika nitamwadhibu Shemaya Mnehelami pamoja na uzao wake. Hapatakuwa na yeyote atakayebaki miongoni mwa watu hawa, wala hataona mema nitakayowatendea watu wangu, asema Bwana, kwa sababu ametangaza uasi dhidi yangu.’”
therefore Yahweh says this: Look, I am about to punish Shemaiah the Nehelamite and his descendants. There will not be a man for him to stay among this people. He will not see the good that I will do for my people—this is Yahweh's declaration—for he has proclaimed rebellion against Yahweh.'”

< Yeremia 29 >