< Yeremia 25 >

1 Neno likamjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
This is the word that came to Jeremiah about all the people of Judah. It came in the fourth year of Jehoiakim son of Josiah, king of Judah. That was the first year of Nebuchadnezzar, king of Babylon.
2 Hivyo nabii Yeremia akawaambia watu wote wa Yuda na wale wote waishio Yerusalemu:
Jeremiah the prophet proclaimed this to all the people of Judah and all the inhabitants of Jerusalem.
3 Kwa miaka ishirini na mitatu, kuanzia mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda, hadi siku hii ya leo, neno la Bwana limekuwa likinijia, nami nimesema nanyi mara kwa mara, lakini hamkusikiliza.
He said, “For twenty-three years, from the thirteenth year of Josiah son of Amon, king of Judah until this day, Yahweh's words have been coming to me and I have spoken to you again and again, but you have not listened.
4 Ingawa Bwana amewatuma watumishi wake wote hao manabii kwenu mara kwa mara, hamkusikiliza wala hamkujali.
Yahweh sent out all his servants the prophets to you again and again, but you have not listened or paid any attention.
5 Walisema, “Geukeni sasa, kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya na matendo yake maovu, ndipo mtaweza kukaa katika nchi ambayo Bwana aliwapa ninyi na baba zenu milele.
These prophets said, 'Let each man turn from his wicked way and the corruption of his practices and return to the land that Yahweh gave in ancient times to your ancestors and to you, as a permanent gift.
6 Msiifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Msinikasirishe kwa vitu ambavyo mmevitengeneza kwa mikono yenu.”
So do not walk after other gods to worship them or bow down to them, and do not provoke him with the work of your hands so that he does you harm.'
7 “Lakini ninyi hamkunisikiliza mimi, tena mkanikasirisha kwa vitu mlivyovitengeneza kwa mikono yenu, nanyi mmejiletea madhara juu yenu wenyewe,” asema Bwana.
But you have not listened to me—this is Yahweh's declaration—so you have provoked me with the work of your hands to do harm to you.
8 Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asema hivi: “Kwa sababu hamkuyasikiliza maneno yangu,
So Yahweh of hosts says this, 'Because you did not listen to my words,
9 nitayaita mataifa yote ya kaskazini na mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli,” asema Bwana. “Nitawaleta waishambulie nchi hii na wakazi wake wote, na dhidi ya mataifa yote yanayowazunguka. Nitawaangamiza kabisa na kuwafanya kitu cha kuchukiwa na kudharauliwa, na kuwa magofu daima.
see, I am about to send out a command to gather all the peoples of the north—this is Yahweh's declaration—with Nebuchadnezzar my servant, king of Babylon, and bring them against this land and its inhabitants, and against all the nations around you. For I will set them apart for destruction. I will turn them into a horror, an object for hissing, and an unending desolation.
10 Nitawaondolea sauti ya shangwe na furaha, sauti ya bibi na bwana arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na mwanga wa taa.
I will put an end to the sound of joy and sound of gladness, the sound of the groom and the sound of the bride, the sound of the millstones and the light of the lamp.
11 Nchi hii yote itakuwa ukiwa na isiyofaa kitu, nayo mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babeli kwa miaka sabini.”
Then all of this land will become a desolation and a horror, and these nations will serve the king of Babylon for seventy years.
12 “Lakini miaka sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na taifa lake na nchi ya Wakaldayo kwa ajili ya hatia yao,” asema Bwana. “Nitaifanya kuwa ukiwa milele.
Then it will happen when seventy years have been completed, that I will punish the king of Babylon and that nation, the land of the Chaldeans—this is Yahweh's declaration—for their iniquity and make it an unending desolation.
13 Nitaleta juu ya nchi hiyo mambo yote niliyosema dhidi yake, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki, na kutolewa unabii na Yeremia dhidi ya mataifa yote.
Then I will carry out against that land all the words that I had spoken, and everything written in this book that Jeremiah has prophesied against all the nations.
14 Wao wenyewe watakuwa watumwa wa mataifa mengi na wafalme wakuu. Nitawalipizia sawasawa na matendo yao na kazi ya mikono yao.”
For also many other nations and great kings will make slaves out of these nations. I will repay them for their deeds and the works of their hands.'”
15 Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, aliloniambia: “Chukua kutoka mkononi mwangu kikombe hiki kilichojaa divai ya ghadhabu yangu, na kuyanywesha mataifa yote ambayo ninakutuma kwao.
For Yahweh, God of Israel, said this to me, “Take this cup of the wine of fury from my hand and make all the nations to which I am sending you drink it.
16 Watakapoinywa, watapepesuka na kukasirika sana kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka katikati yao.”
For they will drink and then stagger about and rant madly before the sword that I am sending out among them.”
17 Hivyo nikakichukua kikombe kutoka mkononi mwa Bwana, na kuyafanya mataifa yote aliyonituma kwao kukinywa:
So I took the cup from Yahweh's hand, and I made all the nations to which Yahweh had sent me drink it:
18 Yaani Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na maafisa wake, kuwafanya magofu na kuwa kitu cha kuchukiza, cha dhihaka na laana, kama walivyo leo;
Jerusalem, the cities of Judah and her kings and officials—to turn them into ruins and something terrifying, and into an object for hissing and cursing, as they are at this present day.
19 pia Farao mfalme wa Misri, watumishi wake, maafisa wake na watu wake wote,
Other nations also had to drink it: Pharaoh king of Egypt and his servants; his officials and all his people;
20 pia wageni wote walioko huko; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa Wafilisti (wale wa Ashkeloni, Gaza, Ekroni na watu walioachwa huko Ashdodi);
all people of mixed heritage and all the kings of the land of Uz; all the kings of the land of Philistia—Ashkelon, Gaza, Ekron, and the remnant of Ashdod;
21 Edomu, Moabu na Amoni;
Edom and Moab and the people of Ammon.
22 wafalme wote wa Tiro na Sidoni; wafalme wa nchi za pwani ngʼambo ya bahari;
The kings of Tyre and Sidon, the kings of the coasts on the other side of the sea,
23 Dedani, Tema, Buzi na wote walio maeneo ya mbali;
Dedan, Tema, and Buz with all the ones who cut the hair on the sides of their heads, they also had to drink it.
24 wafalme wote wa Arabuni na wafalme wote wa watu wageni wanaoishi katika jangwa;
All the kings of Arabia and all the kings of people of mixed heritage who live in the wilderness;
25 wafalme wote wa Zimri, Elamu na Umedi;
all the kings of Zimri, all the kings of Elam, and all the kings of the Medes;
26 na wafalme wote wa pande za kaskazini, wa karibu na wa mbali, mmoja baada ya mwingine; yaani falme zote juu ya uso wa dunia. Baada ya hao wote, mfalme wa Sheshaki atakunywa pia.
all the kings of the north, the ones close by and the ones far away—everyone with his brother and all the kingdoms of the world that are on the surface of the earth, all of them had to drink the cup from Yahweh's hand. Finally, the king of Babylon will also drink from that cup.
27 “Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kunyweni, mlewe na mtapike; angukeni, wala msiinuke tena kwa sababu ya upanga nitakaotuma miongoni mwenu.’
Yahweh said to me, “Now you must say to them, 'Yahweh of hosts, God of Israel, says this: Drink and become drunk, then vomit, fall down, and do not rise before the sword that I am sending among you.'
28 Lakini kama wakikataa kupokea kikombe kutoka mikononi mwako na kunywa, waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Ni lazima mnywe!
Then it will happen that if they refuse to take the cup from your hand to drink, you will say to them, 'Yahweh of hosts says this: You must certainly drink it.
29 Tazama, nimeanza kuleta maafa juu ya mji ulio na Jina langu, na je, kweli ninyi mtaepuka kuadhibiwa? Hamwezi kuepuka kuadhibiwa, kwa maana nitaleta vita juu ya wote waishio duniani, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
For see, I am about to bring disaster on the city that is called by my name, and should you yourselves be free from punishment? You will not be free, for I am calling a sword against all the inhabitants of the land!—this is the declaration of Yahweh of hosts.'
30 “Basi sasa toa unabii kwa maneno haya yote dhidi yao, uwaambie: “‘Bwana atanguruma kutoka juu; atatoa sauti ya ngurumo kutoka makao yake matakatifu na kunguruma kwa nguvu sana dhidi ya nchi yake. Atapiga kelele kama wao wakanyagao zabibu, atapiga kelele dhidi ya wote waishio duniani.
You must prophesy all these words against them, and say to them, 'Yahweh will roar from the heights and he will shout with his voice from his holy dwelling, and he will roar mightily against his fold; and he will shout, like those who tread the grapes against all those who live on the earth.
31 Ghasia zitasikika hadi miisho ya dunia, kwa maana Bwana ataleta mashtaka dhidi ya mataifa; ataleta hukumu juu ya wanadamu wote na kuwaua waovu wote,’” asema Bwana.
The sound of battle will resound to the ends of the earth, for Yahweh brings charges against the nations, and he brings judgment on all flesh, and the wicked ones he will put to the sword—this is Yahweh's declaration.'
32 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama! Maafa yanaenea kutoka taifa moja hadi jingine; tufani kubwa inainuka kutoka miisho ya dunia.”
Yahweh of hosts says this, 'See, disaster is going out from nation to nation, and a great storm is beginning from the farthest parts of the earth.
33 Wakati huo, hao waliouawa na Bwana watatapakaa kila mahali, kuanzia mwisho mmoja wa dunia hadi mwisho mwingine. Hawataombolezewa wala kukusanywa au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyoenea juu ya ardhi.
Then those killed by Yahweh will on that day extend from one end of the earth to the other; they will not be mourned, gathered, or buried. They will be like dung on the ground.
34 Lieni na kuomboleza, enyi wachungaji, mgaagae mavumbini, ninyi viongozi wa kundi. Kwa maana wakati wenu wa kuchinjwa umewadia; mtaanguka na kuvunjavunjwa kama vyombo vizuri vya udongo.
Wail, shepherds, and shout for help! Roll about in the dust, you leaders of the flock, for the days of your slaughter have come; you will be scattered when you fall like fine pottery.
35 Wachungaji hawatakuwa na mahali pa kukimbilia, viongozi wa kundi hawatapata mahali pa kutorokea.
There is no refuge for the shepherds, there will be no escape for the leaders of the flock.
36 Sikia kilio cha wachungaji, maombolezo ya viongozi wa kundi, kwa maana Bwana anayaharibu malisho yao.
Hear the cries of the shepherds and the wails of the leaders of the flock, for Yahweh is destroying their pastures.
37 Makao yao ya amani yataharibiwa kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
So the peaceful pastures will be devastated because of Yahweh's fierce anger.
38 Kama simba ataacha pango lake, nchi yao itakuwa ukiwa kwa sababu ya upanga wa mdhalimu, na kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.
Like a young lion, he has left his den, for their land will become a horror because of the oppressor's anger, because of his angry wrath.'”

< Yeremia 25 >