< Yeremia 17 >

1 “Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma, imeandikwa kwa ncha ya almasi, kwenye vibao vya mioyo yao na kwenye pembe za madhabahu zao.
Grzech Judy jest zapisany żelaznym rylcem, ostrzem diamentu jest wyryty na tablicy ich serca i na rogach waszych ołtarzy;
2 Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao na nguzo za Ashera, kandokando ya miti iliyotanda na juu ya vilima virefu.
Gdy ich synowie wspominają ich ołtarze i gaje pod drzewami zielonymi, na wysokich pagórkach.
3 Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara, pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.
[Moja] góro na polu! Twoje bogactwo [i] wszystkie twoje skarby wydam na łup z powodu grzechu twoich wyżyn we wszystkich twoich granicach.
4 Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza urithi niliokupa. Nitakufanya mtumwa wa adui zako katika nchi usiyoijua, kwa kuwa umeiwasha hasira yangu, nayo itawaka milele.”
A [ty] opuścisz swoje dziedzictwo, które ci dałem. I sprawię, że będziesz służył swoim wrogom w ziemi, której nie znasz, bo rozpaliliście ogień mojej zapalczywości, [który] będzie płonąć na wieki.
5 Hili ndilo asemalo Bwana: “Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu, ategemeaye mwenye mwili kwa ajili ya nguvu zake, ambaye moyo wake umemwacha Bwana.
Tak mówi PAN: Przeklęty człowiek, który ufa człowiekowi i który czyni ciało swoim ramieniem, a od PANA odstępuje jego serce.
6 Atakuwa kama kichaka cha jangwani; hataona mafanikio yatakapokuja. Ataishi katika sehemu zisizo na maji, katika nchi ya chumvi ambapo hakuna yeyote aishiye humo.
Będzie bowiem jak wrzos na pustyni, który nie czuje, gdy przychodzi coś dobrego, ale wybiera suche miejsca na pustyni, w ziemi słonej i bezludnej.
7 “Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana, ambaye matumaini yake ni katika Bwana.
Błogosławiony człowiek, który ufa PANU, a którego nadzieją jest PAN.
8 Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji. Hauogopi wakati wa joto ujapo; majani yake ni mabichi daima. Hauna hofu katika mwaka wa ukame na hautaacha kuzaa matunda.”
Będzie bowiem jak drzewo zasadzone nad wodami, które swoje korzenie zapuszcza nad strumieniem i nie zauważa, gdy upał przychodzi, ale jego liść pozostaje zielony. W roku suszy nie troszczy się i nie przestaje przynosić owocu.
9 Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote, ni mwovu kupita kiasi. Ni nani awezaye kuujua?
Najzdradliwsze ponad wszystko [jest] serce i najbardziej przewrotne. Któż zdoła je poznać?
10 “Mimi Bwana huchunguza moyo na kuzijaribu nia, ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake, kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”
Ja, PAN, badam serca i doświadczam nerki, aby oddać każdemu według jego dróg i według owocu jego uczynków.
11 Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga, ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki. Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha, na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.
[Jak] kuropatwa gromadzi [swoje jajka], ale ich nie wysiaduje, [tak] kto zbiera bogactwa niesprawiedliwie, zostawi je w połowie swoich dni, a u swego kresu okaże się głupcem;
12 Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo, ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.
Wzniosłym tronem chwały od początku [jest] miejsce naszej świątyni.
13 Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli, wote wakuachao wataaibika. Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini kwa sababu wamemwacha Bwana, chemchemi ya maji yaliyo hai.
PANIE, nadziejo Izraela! Wszyscy, którzy cię opuszczają, będą zawstydzeni; ci, którzy odstępują ode mnie, będą zapisani na ziemi, gdyż opuścili PANA, źródło żywych wód.
14 Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe nami nitaokoka, kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.
Uzdrów mnie, PANIE, a będę uzdrowiony; zbaw mnie, a będę zbawiony. Ty bowiem jesteś moją chwałą.
15 Wao huendelea kuniambia, “Liko wapi neno la Bwana? Sasa na litimie!”
Oto oni mówią do mnie: Gdzie jest słowo PANA? Niech się już spełni!
16 Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako; unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa. Kile kipitacho midomoni mwangu ki wazi mbele yako.
Ale ja nie zabiegałem, aby być twoim pasterzem ani nie pragnąłem dnia boleści; ty wiesz: cokolwiek wyszło z moich ust, jest przed twoim obliczem.
17 Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu; wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.
Nie bądź dla mnie postrachem. Ty jesteś moją nadzieją w dniu utrapienia.
18 Watesi wangu na waaibishwe, lakini nilinde mimi nisiaibike; wao na watiwe hofu kuu, lakini unilinde mimi na hofu kuu. Waletee siku ya maafa; waangamize kwa maangamizi maradufu.
Niech będą zawstydzeni ci, którzy mnie prześladują, lecz niech ja nie będę zawstydzony. Niech się oni lękają, lecz niech ja się nie lękam. Sprowadź na nich dzień utrapienia i zniszcz ich podwójnym zniszczeniem.
19 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu.
Tak PAN powiedział do mnie: Idź i stań w bramie synów [tego] ludu, którą wchodzą i wychodzą królowie Judy, oraz we wszystkich bramach Jerozolimy;
20 Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya.
I powiedz im: Słuchajcie słowa PANA, królowie Judy, cała Judo i wszyscy mieszkańcy Jerozolimy, którzy wchodzicie przez te bramy!
21 Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu.
Tak mówi PAN: Strzeżcie pilnie waszych dusz i nie noście [żadnego] ciężaru w dzień szabatu ani nie wnoście [tego] przez bramy Jerozolimy;
22 Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu.
Nie wynoście ciężarów z waszych domów w dzień szabatu ani nie wykonujcie żadnej pracy, ale święćcie dzień szabatu, jak nakazałem waszym ojcom.
23 Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu.
Oni jednak nie usłuchali ani nie nakłonili swego ucha, lecz zatwardzili swój kark, aby nie słuchać i nie przyjąć pouczenia.
24 Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo,
A jeśli będziecie mnie pilnie słuchać, mówi PAN, i nie wnosić ciężarów przez bramy tego miasta w dzień szabatu, ale będziecie święcić dzień szabatu, nie wykonując w nim żadnej pracy;
25 ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima.
Wtedy przez bramy tego miasta będą wchodzić królowie i książęta zasiadający na tronie Dawida, będą wjeżdżać na rydwanach i na koniach, oni, ich książęta, Judejczycy i mieszkańcy Jerozolimy, a to miasto będzie trwać na wieki.
26 Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana.
I zbiegną się z miast Judy, z okolic Jerozolimy i z ziemi Beniamina, z równin, z gór i z południa, przynosząc całopalenia, ofiary, dary i kadzidło i przynosząc także dziękczynienie do domu PANA.
27 Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’”
Ale jeśli mnie nie usłuchacie, aby święcić dzień szabatu i nie nosić ciężaru, gdy wchodzicie przez bramy Jerozolimy w dzień szabatu, wtedy rozniecę ogień w jej bramach, który pochłonie pałace Jerozolimy i nie będzie ugaszony.

< Yeremia 17 >