< Isaya 65 >

1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
Objawiłem się tym, którzy o mnie nie pytali, zostałem znaleziony przez tych, którzy mnie nie szukali. Do narodu, który się nie nazywał moim imieniem, mówiłem: Oto jestem, oto jestem.
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
Cały dzień wyciągałem swoje ręce do ludu buntowniczego, który kroczy drogą niedobrą, za własnymi myślami;
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
Do ludu, który stale i zuchwale pobudza mnie do gniewu, składając ofiary w ogrodach i paląc kadzidło na cegłach;
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
Który przesiaduje na grobach i nocuje przy swoich bożkach, który je mięso wieprzowe, a obrzydliwa polewka [jest] w jego naczyniach;
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
I mówi: Odsuń się, nie zbliżaj się do mnie, bo jestem świętszy od ciebie. On jest dymem w moich nozdrzach i ogniem płonącym przez cały dzień.
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
Oto zapisano to przede mną. Nie zamilknę, ale oddam i odpłacę im w zanadrzu;
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
Za wasze nieprawości i nieprawości waszych ojców, mówi PAN, którzy palili kadzidło na górach i hańbili mnie na pagórkach; dlatego wymierzę im w zanadrze za ich dawne czyny.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
Tak mówi PAN: Jak wtedy, gdy znajduje się wino w kiści i mówi się: Nie psuj go, bo w nim jest błogosławieństwo, tak i ja uczynię przez wzgląd na moje sługi – nie zniszczę ich wszystkich.
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
Bo wywiodę z Jakuba potomstwo, a z Judy dziedzica moich gór. Moi wybrani posiądą je i moi słudzy będą tam mieszkać.
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
A Szaron stanie się pastwiskiem dla owiec, a dolina Akor legowiskiem dla wołów – to dla mojego ludu, który mnie szukał.
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
Ale was, którzy opuściliście PANA, którzy zapominacie o mojej świętej górze, którzy zastawiacie stół dla tego wojska i składacie ofiary z płynów temu mnóstwu;
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
Was przeznaczę pod miecz i wy wszyscy schylicie się na rzeź, ponieważ wołałem, a nie odezwaliście się, mówiłem, a nie słyszeliście, ale czyniliście to, co złe w moich oczach, i wybraliście to, co mi się nie podobało.
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
Dlatego tak mówi Pan BÓG: Oto moi słudzy będą jeść, a wy będziecie głodni. Oto moi słudzy będą pić, a wy będziecie spragnieni. Oto moi słudzy będą się radować, a wy będziecie zawstydzeni.
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
Oto moi słudzy będą śpiewać z radości serca, a wy będziecie krzyczeć z boleści serca i zawodzić z powodu zrozpaczonego ducha.
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
I zostawicie swoje imię moim wybranym na przekleństwo, gdyż Pan BÓG zabije was, a swoje sługi nazwie innym imieniem.
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
Ten, który będzie sobie błogosławił na ziemi, będzie sobie błogosławił w Bogu prawdziwym, a kto będzie przysięgał na ziemi, będzie przysięgał na Boga prawdziwego, bo dawne uciski pójdą w zapomnienie i będą zakryte przed moimi oczami.
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
Oto bowiem stworzę nowe niebiosa i nową ziemię i nie będą wspominane pierwsze rzeczy ani nie przyjdą na myśl.
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
Lecz weselcie się i radujcie na wieki wieków z tego, co ja stworzę, bo oto stworzę Jerozolimę radością i jej lud weselem.
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
I będę się radować z powodu Jerozolimy i weselić z powodu mojego ludu, a nie będzie już słychać w nim głosu płaczu ani narzekania.
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
Nie będzie tam już ani niemowlęcia [żyjącego] tylko kilka dni, ani starca, który by nie dożył swoich dni, bo dziecko umrze jako stuletni, ale grzesznik, choćby miał i sto lat, będzie przeklęty.
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
Pobudują też domy i będą w nich mieszkać, zasadzą winnice i będą jeść z nich owoce.
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
Nie będą budować, by ktoś inny tam mieszkał, nie będą sadzić, by ktoś inny jadł, bo dni mojego ludu będą jak dni drzewa i moi wybrani długo będą korzystać z dzieła swoich rąk.
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
Nie będą trudzić się na próżno ani rodzić, aby się bać, gdyż są potomstwem błogosławionym przez PANA, oni i ich potomkowie wraz z nimi.
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
I będzie tak, że zanim zawołają, ja się odezwę, gdy jeszcze będą mówić, ja wysłucham.
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
Wilk z barankiem paść się będą razem, lew jak wół będzie jeść słomę i proch będzie pokarmem węża. Nie będą szkodzić ani niszczyć na całej mojej świętej górze, mówi PAN.

< Isaya 65 >