< Isaya 37 >

1 Mfalme Hezekia aliposikia haya, akararua nguo zake na kuvaa nguo ya gunia, naye akaenda katika Hekalu la Bwana.
A gdy król Ezechiasz to usłyszał, rozdarł swoje szaty, oblekł się w wór i wszedł do domu PANA.
2 Akawatuma Eliakimu msimamizi wa nyumba ya mfalme, Shebna mwandishi, na viongozi wa makuhani, wote wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya mwana wa Amozi.
I posłał Eliakima, przełożonego swego domu, pisarza Szebnę i starszych spośród kapłanów, obleczonych w wory, do proroka Izajasza, syna Amosa.
3 Wakamwambia, “Hili ndilo asemalo Hezekia: Siku hii ni siku ya dhiki, ya kukaripiwa na ya aibu, kama wakati watoto wanapofikia karibu kuzaliwa na kumbe hakuna nguvu ya kuwazaa.
I powiedzieli mu: Tak mówi Ezechiasz: Ten dzień jest dniem utrapienia, upomnienia i bluźnierstwa. Nadszedł bowiem czas porodu dzieci, a nie ma siły, aby je urodzić.
4 Yamkini Bwana, Mungu wako atayasikia maneno ya jemadari wa jeshi, ambaye bwana wake, mfalme wa Ashuru, amemtuma kumdhihaki Mungu aliye hai, tena kwamba atamkemea kwa maneno ambayo Bwana, Mungu wako ameyasikia. Kwa hiyo omba kwa ajili ya mabaki ambao bado wako.”
Może PAN, twój Bóg, usłyszy słowa Rabszaka, którego przysłał król Asyrii, jego pan, aby znieważać Boga żywego, i pomści słowa, które usłyszał PAN, twój Bóg. Zanieś więc modlitwę za resztkę, która pozostaje.
5 Maafisa wa Mfalme Hezekia walipofika kwa Isaya,
Tak to słudzy króla Ezechiasza przyszli do Izajasza.
6 Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Usiogope kwa hayo uliyoyasikia, yale maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana nayo.
A Izajasz im odpowiedział: Tak powiedzcie waszemu panu: Tak mówi PAN: Nie bój się tych słów, które słyszałeś, którymi bluźnili mi słudzy króla Asyrii.
7 Sikiliza! Nitatia roho fulani ndani yake ili kwamba atakaposikia taarifa fulani, atarudi nchi yake mwenyewe, nami huko nitafanya auawe kwa upanga.’”
Oto ześlę na niego ducha i usłyszy [pewną] wieść, [a potem] wróci do swojej ziemi i sprawię, że padnie od miecza w swojej ziemi.
8 Jemadari wa jeshi aliposikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi, akamkuta mfalme akipigana na Libna.
Wrócił więc Rabszak i zastał króla Asyrii walczącego przeciwko Libnie. Usłyszał bowiem, że odstąpił od Lakisz.
9 Basi Senakeribu akapata taarifa kwamba Tirhaka, Mkushi mfalme wa Misri, alikuwa anaenda kupigana naye. Aliposikia jambo hili akatuma wajumbe kwa Hezekia na neno hili:
A dotarło do niego, że mówiono o Tirhace, królu Etiopii: Oto wyruszył na wojnę przeciwko tobie. Gdy to usłyszał, wysłał posłańców do Ezechiasza z tymi słowami:
10 “Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda: Usikubali huyo Mungu unayemtumainia akudanganye wakati anaposema, ‘Yerusalemu haitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.’
Tak powiedzcie Ezechiaszowi, królowi Judy: Niech cię nie zwodzi twój Bóg, któremu ufasz, mówiąc: Jerozolima nie zostanie wydana w ręce króla Asyrii.
11 Hakika umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru wametenda kwa nchi zote, wakiwaangamiza kabisa. Je, wewe utaokolewa?
Oto słyszałeś, co uczynili królowie Asyrii wszystkim ziemiom, niszcząc je. A ty miałbyś zostać wybawiony?
12 Je, miungu ya mataifa ambayo yaliangamizwa na baba zangu iliweza kuwaokoa? Yaani miungu ya Gozani, Harani, Resefu, na ya watu wa Edeni waliokuwa Telasari?
Czy bogowie narodów wybawili tych, których moi ojcowie wygubili: Gozan, Charan, Resef i synów Edenu, którzy byli w Telassar?
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa mji wa Sefarvaimu, au wa Hena au wa Iva?”
Gdzie jest król Chamatu, król Arpadu i król miasta Sefarwaim, Heny i Iwwy?
14 Hezekia akapokea barua kutoka kwa wale wajumbe naye akaisoma. Kisha akapanda katika Hekalu la Bwana, akaikunjua mbele za Bwana.
Gdy Ezechiasz wziął list z rąk posłów, przeczytał go, wszedł do domu PANA i rozwinął go przed PANEM.
15 Naye Hezekia akamwomba Bwana akisema:
I Ezechiasz modlił się do PANA, mówiąc:
16 “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya kiti cha enzi kati ya makerubi, wewe peke yako ndiwe Mungu juu ya falme zote za dunia. Wewe umeumba mbingu na nchi.
PANIE zastępów, Boże Izraela, który zasiadasz pomiędzy cherubinami, ty, ty jedynie jesteś Bogiem wszystkich królestw ziemi, ty stworzyłeś niebo i ziemię.
17 Tega sikio, Ee Bwana, usikie; fungua macho yako, Ee Bwana, uone; sikiliza maneno yote ambayo Senakeribu ametuma kumtukana Mungu aliye hai.
Nakłoń swego ucha, PANIE, i słuchaj. Otwórz swe oczy, PANIE, i spójrz. Słuchaj wszystkich słów Sennacheryba, które przesłał, aby znieważać Boga żywego.
18 “Ni kweli, Ee Bwana, kwamba wafalme wa Ashuru wameyaangamiza mataifa haya yote pamoja na nchi zao.
To prawda, PANIE, że królowie Asyrii spustoszyli wszystkie narody i ich ziemie;
19 Wameitupa miungu yao kwenye moto na kuiangamiza, kwa kuwa haikuwa miungu, bali miti na mawe tu, iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
I powrzucali ich bogów do ognia. Nie byli bowiem bogami, ale dziełem rąk ludzkich, drewnem i kamieniem. Dlatego ich zniszczyli.
20 Sasa basi, Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe kutoka mkononi mwake, ili kwamba falme zote duniani zipate kujua kwamba wewe peke yako, Ee Bwana, ndiwe Mungu.”
Teraz więc, PANIE, nasz Boże, wybaw nas z jego ręki, aby wszystkie królestwa ziemi poznały, że jedynie ty jesteś PANEM.
21 Kisha Isaya mwana wa Amozi akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akasema: “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Kwa sababu umeniomba kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru,
Wtedy Izajasz, syn Amosa, posłał [wiadomość] do Ezechiasza: Tak mówi PAN, Bóg Izraela: Ponieważ modliłeś się do mnie w sprawie Sennacheryba, króla Asyrii;
22 hili ndilo neno ambalo Bwana amelisema dhidi yake: “Bikira binti Sayuni anakudharau na kukudhihaki. Binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake unapokimbia.
Oto słowo, które PAN o nim wypowiedział: Dziewica, córka Syjonu, wzgardziła tobą i śmiała się z ciebie. Córka Jerozolimy kiwała głową za tobą.
23 Ni nani uliyemtukana na kumkufuru? Ni nani uliyeinua sauti yako dhidi yake, na kumwinulia macho yako kwa kiburi? Ni dhidi ya yule Aliye Mtakatifu wa Israeli!
Kogo znieważyłeś i komu bluźniłeś? Przeciwko komu podniosłeś swój głos i wysoko podniosłeś swoje oczy? Przeciwko Świętemu Izraela.
24 Kupitia kwa wajumbe wako umelundika matukano juu ya Bwana. Nawe umesema, ‘Kwa magari yangu mengi ya vita, nimepanda juu ya vilele vya milima, vilele vya juu sana katika Lebanoni. Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu, misunobari yake iliyo bora sana. Nimefikia sehemu zake zilizoinuka juu sana, misitu yake iliyo mizuri sana.
Przez swoje sługi znieważyłeś Pana i powiedziałeś: Z mnóstwem swoich rydwanów wyszedłem na wysokie góry i zbocza Libanu. Wytnę jego wysokie cedry i jego wyborowe cyprysy i przyjdę aż do najwyższego jego szczytu, do lasów i do lasu jego pola.
25 Nimechimba visima katika nchi za kigeni na kunywa maji yake. Kwa nyayo za miguu yangu nimekausha vijito vyote vya Misri.’
Ja wykopałem studnie i piłem wody, swoimi stopami wysuszyłem wszystkie rzeki oblężonych miejsc.
26 “Je, hujasikia? Zamani sana niliamuru hili. Siku za kale nilipanga hili; sasa nimelifanya litokee, kwamba umegeuza miji yenye ngome kuwa malundo ya mawe.
Czy nie słyszałeś, że ja dawno to uczyniłem i za dawnych dni to sprawiłem? A teraz wypełniam, gdy obracasz warowne miasta w stosy gruzów.
27 Watu wa miji hiyo wameishiwa nguvu, wanavunjika mioyo na kuaibishwa. Wao ni kama mimea katika shamba, kama machipukizi mororo ya kijani, kama majani yachipuayo juu ya paa la nyumba, ambayo hukauka kabla ya kukua.
Ich mieszkańcy, bezsilni, przestraszyli się i zawstydzili. Byli jak trawa polna, jak świeża zieleń, jak trawa na dachach, jak [zboże], które uschło, zanim dojrzało.
28 “Lakini ninajua mahali ukaapo, kutoka kwako na kuingia kwako, na jinsi unavyoghadhibika dhidi yangu.
Znam twoje miejsce pobytu, twoje wyjście i twoje wejście, a także twoją wściekłość przeciwko mnie.
29 Kwa sababu unaghadhibika na ufidhuli dhidi yangu, na kwa sababu ufidhuli wako umefika masikioni mwangu, nitaweka ndoana yangu puani mwako na hatamu yangu kinywani mwako, nami nitakufanya urudi kwa njia ile uliyoijia.
Ponieważ twoja wściekłość na mnie i twoja zuchwałość doszły do moich uszu, włożę moje kółko w twoje nozdrza i moje wędzidło na twoje wargi i zawrócę cię tą drogą, którą przyszedłeś.
30 “Hii ndiyo itakuwa ishara kwako, ee Hezekia: “Mwaka huu utakula kile kiotacho chenyewe, na mwaka wa pili utakula kutoka machipukizi yake. Lakini katika mwaka wa tatu panda na uvune, panda mashamba ya mizabibu na ule matunda yake.
A to będzie znakiem dla ciebie: Tego roku będziesz jadł zboże samorodne, w drugim roku także zboże samorodne, w trzecim roku zaś siejcie i zbierajcie żniwo, sadźcie winnice i jedzcie ich owoce.
31 Mara nyingine tena mabaki ya nyumba ya Yuda wataeneza mizizi chini na kuzaa matunda juu.
Resztka ocalonych z domu Judy ponownie zapuści korzenie w głąb i wyda owoc w górze.
32 Kwa kuwa kutoka Yerusalemu watakuja mabaki, na kutoka Mlima Sayuni kundi la walionusurika. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, ndio utatimiza jambo hili.
Z Jerozolimy wyjdą bowiem resztka i ci, którzy ocaleli z góry Syjon. Sprawi to gorliwość PANA zastępów.
33 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme wa Ashuru: “Hataingia katika mji huu wala hatapiga mshale hapa. Hatakuja mbele yake na ngao wala kupanga majeshi kuuzingira.
Dlatego tak mówi PAN o królu Asyrii: Nie wejdzie do tego miasta ani nie wypuści tam strzały, nie wyruszy przeciw niemu z tarczą ani nie usypie szańców przeciwko niemu.
34 Kwa njia ile aliyoijia ndiyo atakayorudi; hataingia katika mji huu,” asema Bwana.
Drogą, którą przyszedł, powróci, a do tego miasta nie wejdzie, mówi PAN.
35 “Nitaulinda mji huu na kuuokoa, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu!”
Będę bowiem bronił tego miasta i ocalę je ze względu na siebie i ze względu na Dawida, swego sługę.
36 Ndipo malaika wa Bwana akaenda, akawaua wanajeshi 185,000 katika kambi ya Waashuru. Wenzao walipoamka asubuhi yake, walikuta maiti kila mahali!
Wtedy wyszedł Anioł PANA i zabił w obozie Asyrii sto osiemdziesiąt pięć tysięcy [osób]. A gdy wstali wcześnie rano, oto wszędzie [było] pełno trupów.
37 Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akavunja kambi na kuondoka. Akarudi Ninawi na kukaa huko.
Sennacheryb, król Asyrii, wycofał się więc i wyruszył. Wrócił i zamieszkał w Niniwie.
38 Siku moja, alipokuwa akiabudu katika hekalu la mungu wake Nisroki, wanawe Adrameleki na Shareza wakamuua kwa upanga, nao wakakimbilia nchi ya Ararati. Naye Esar-Hadoni mwanawe akawa mfalme badala yake.
A gdy oddawał pokłon w domu swego boga Nisroka, jego synowie – Adramelek i Sareser – zabili go mieczem. Potem uciekli do ziemi Ararat. I Asarchaddon, jego syn, królował w jego miejsce.

< Isaya 37 >