< Isaya 32 >

1 Tazama, mfalme atatawala kwa uadilifu na watawala watatawala kwa haki.
Oto król będzie panował w sprawiedliwości, a książęta będą rządzić w prawości.
2 Kila mtu atakuwa kama kivuli cha kujificha kutokana na upepo na kimbilio kutokana na dhoruba, kama vijito vya maji jangwani na kivuli cha mwamba mkubwa katika ardhi yenye kiu.
I ten mężczyzna będzie jak zasłona przed wiatrem i jak schronienie przed burzą; jak strumienie wód w suchym miejscu, jak cień wielkiej skały w spragnionej ziemi.
3 Ndipo macho ya wale wanaoona hayatafumbwa tena, nayo masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.
Oczy patrzących nie będą zaćmione i uszy słuchających będą uważnie słuchać.
4 Moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu na kuelewa, nao ulimi wenye kigugumizi utanena kwa ufasaha.
Serce pochopnych zrozumie wiedzę, a język jąkających się będzie mówić pewnie i wyraźnie.
5 Mpumbavu hataitwa tena muungwana, wala mtu mbaya kabisa kupewa heshima ya juu.
Nieszlachetnego nie będą już nazywać szlachetnym ani o skąpym nie powie się, że [jest] szczodry;
6 Kwa kuwa mpumbavu hunena upumbavu, moyo wake hushughulika na uovu: Hutenda mambo yasiyo ya kumcha Mungu, na hueneza habari za makosa kuhusu Bwana; yeye huwaacha wenye njaa bila kitu, na wenye kiu huwanyima maji.
Nieszlachetny bowiem mówi nikczemnie i jego serce obmyśla nieprawość, aby postępował obłudnie i mówił przeciwko PANU przewrotnie, by wyniszczył duszę głodnego i spragnionego pozbawił napoju.
7 Taratibu za mtu mbaya kabisa ni ovu, hufanya mipango miovu ili kumwangamiza maskini kwa uongo, hata wakati ambapo hoja za mhitaji ni za haki.
Zamierzenia skąpego są złe, bo chytrze obmyśla, jak zniszczyć biednych słowami kłamstwa i mówić przeciwko ubogim przed sądem.
8 Lakini mtu muungwana hufanya mipango ya kiungwana, na kwa matendo ya kiungwana yeye hufanikiwa.
Ale szczodry ma szczodrobliwe myśli i będzie obstawać przy swojej szczodrobliwości.
9 Enyi wanawake wenye kuridhika sana, amkeni na mnisikilize. Enyi binti mnaojisikia kuwa salama, sikieni lile ninalotaka kuwaambia!
Kobiety beztroskie, powstańcie, słuchajcie mego głosu; córki pewne siebie, nakłońcie ucha na moją mowę.
10 Muda zaidi kidogo ya mwaka mmoja, ninyi mnaojisikia salama mtatetemeka, mavuno ya zabibu yatakoma na mavuno ya matunda hayatakuwepo.
Przez wiele dni i lat będziecie zatrwożone, wy pewne siebie! Ustanie bowiem winobranie, zbioru nie będzie.
11 Tetemekeni, enyi wanawake wenye kuridhika, tetemekeni kwa hofu, enyi binti mnaojisikia salama! Vueni nguo zenu, vaeni nguo ya gunia viunoni mwenu.
Zatrwóżcie się, wy beztroskie, ulęknijcie się, pewne siebie! Rozbierzcie się i obnażcie się, a przepaszcie [worem] biodra.
12 Pigeni matiti yenu kwa ajili ya mashamba mazuri, kwa ajili ya mizabibu iliyozaa vizuri
Nastanie lament nad piersiami, nad rozkosznymi polami i nad urodzajną winoroślą.
13 na kwa ajili ya nchi ya watu wangu, nchi ambayo miiba na michongoma imemea: naam, ombolezeni kwa ajili ya nyumba zote za furaha na kwa ajili ya mji huu wenye kufanya sherehe.
Na ziemi mojego ludu wyrosną ciernie i osty – tak, we wszystkich wesołych domach w rozbawionym mieście.
14 Ngome itaachwa, mji wenye kelele nyingi utahamwa, ngome ndani ya mji na mnara wa ulinzi vitakuwa ukiwa milele, mahali pazuri pa punda na malisho ya makundi ya kondoo,
Pałace bowiem zostaną opuszczone, ustanie wrzawa miasta, zamek i baszty staną się jaskiniami na zawsze, miejscem uciechy dla dzikich osłów, pastwiskiem dla stad;
15 mpaka Roho amwagwe juu yetu kutoka juu, nalo jangwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba kuwa kama msitu.
Aż zostanie wylany na nas duch z wysoka, pustynia obróci się w urodzajne pole, a urodzajne pole będzie uważane za las.
16 Haki itakaa katika jangwa, na uadilifu utakaa katika shamba lenye rutuba.
Sąd zamieszka na pustyni, sprawiedliwość osiądzie na urodzajnym polu.
17 Matunda ya haki yatakuwa amani, matokeo ya haki yatakuwa utulivu na matumaini milele.
Dziełem sprawiedliwości będzie pokój, owocem sprawiedliwości odpoczynek i bezpieczeństwo na wieki.
18 Watu wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani, katika nyumba zilizo salama, katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.
Mój lud bowiem będzie mieszkał w przybytku pokoju, w bezpiecznych mieszkaniach i w spokojnych miejscach odpoczynku;
19 Hata kama mvua ya mawe iangushe msitu na mji ubomolewe kabisa,
Gdy spadnie na las grad, a miasto będzie bardzo poniżone.
20 tazama jinsi utakavyobarikiwa, ukipanda mbegu yako katika kila kijito, na kuwaacha ngʼombe wako na punda wajilishe kwa uhuru.
Błogosławieni jesteście, wy, którzy siejecie na wszelkich urodzajnych miejscach, puszczając tam wolno woły i osły.

< Isaya 32 >