< Wahebrania 1 >

1 Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa njia ya manabii mara nyingi na kwa njia mbalimbali,
God, who in ancient days spoke to our forefathers in many distinct messages and by various methods through the Prophets,
2 lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu. (aiōn g165)
has at the end of these days spoken to us through a Son, who is the pre-destined Lord of the universe, and through whom He made the Ages. (aiōn g165)
3 Mwana ni mngʼao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Aliye Mkuu huko mbinguni.
He brightly reflects God's glory and is the exact representation of His being, and upholds the universe by His all-powerful word. After securing man's purification from sin He took His seat at the right hand of the Majesty on high,
4 Kwa hiyo alifanyika bora kuliko malaika, kama jina alilorithi lilivyo bora kuliko lao.
having become as far superior to the angels as the Name He possesses by inheritance is more excellent than theirs.
5 Kwa maana ni malaika yupi ambaye wakati wowote Mungu alipata kumwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa?” Au tena, “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu?”
For to which of the angels did God ever say, "My Son art Thou: I have this day become Thy Father;" and again, "I will be a Father to Him, and He shall be My Son"?
6 Tena, Mungu amletapo mzaliwa wake wa kwanza ulimwenguni, anasema, “Malaika wote wa Mungu na wamsujudu.”
But speaking of the time when He once more brings His Firstborn into the world, He says, "And let all God's angels worship Him."
7 Anenapo kuhusu malaika asema, “Huwafanya malaika wake kuwa pepo, watumishi wake kuwa miali ya moto.”
Moreover of the angels He says, "He changes His angels into winds, and His ministering servants into a flame of fire."
8 Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako. (aiōn g165)
But of His Son, He says, "Thy throne, O God, is for ever and for ever, and the sceptre of Thy Kingdom is a sceptre of absolute justice. (aiōn g165)
9 Umependa haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.”
Thou hast loved righteousness and hated lawlessness; therefore God, Thy God, has anointed Thee with the oil of gladness beyond Thy companions."
10 Pia asema, “Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
It is also of His Son that God says, "Thou, O Lord, in the beginning didst lay the foundations of the earth, and the heavens are the work of Thy hands.
11 Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu; zote zitachakaa kama vazi.
The heavens will perish, but Thou remainest; and they will all grow old like a garment,
12 Utazikungʼutakungʼuta kama joho, nazo zitachakaa kama vazi. Lakini wewe hubadiliki, nayo miaka yako haikomi kamwe.”
and, as though they were a mantle Thou wilt roll them up; yes, like a garment, and they will undergo change. But Thou art the same, and Thy years will never come to an end."
13 Je, ni kwa malaika yupi ambaye Mungu amepata kumwambia wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako”?
To which of the angels has He ever said, "Sit at My right hand till I make Thy foes a footstool for Thy feet"?
14 Je, malaika wote si roho watumikao, waliotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?
Are not all angels spirits that serve Him--whom He sends out to render service for the benefit of those who, before long, will inherit salvation?

< Wahebrania 1 >