< Mwanzo 15 >

1 Baada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.”
And after these things the word of the Lord came to Abram in a vision, saying, Fear not, Abram, I shield you, your reward shall be very great.
2 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina hata mtoto na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?”
And Abram said, Master [and] Lord, what will you give me? whereas I am departing without a child, but the son of Masek my home-born female slave, this Eliezer of Damascus [is mine heir.]
3 Abramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”
And Abram said, [I am grieved] since you have given me no seed, but my home-born [servant] shall succeed me.
4 Ndipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.”
And immediately there was a voice of the Lord to him, saying, This shall not be your heir; but he that shall come out of you shall be your heir.
5 Akamtoa nje na kusema, “Tazama juu kuelekea mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”
And he brought him out and said to him, Look up now to heaven, and count the stars, if you shall be able to number them fully, and he said, Thus shall your seed be.
6 Abramu akamwamini Bwana, naye kwake hili likahesabiwa kuwa haki.
And Abram believed God, and it was counted to him for righteousness.
7 Pia akamwambia, “Mimi ndimi Bwana, niliyekutoa toka Uru ya Wakaldayo nikupe nchi hii uimiliki.”
And he said to him, I am God that brought you out of the land of the Chaldeans, so as to give you this land to inherit.
8 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, nitawezaje kujua kwamba nitapata kuimiliki?”
And he said, Master [and] Lord, how shall I know that I shall inherit it?
9 Ndipo Bwana akamwambia, “Niletee mtamba wa ngʼombe, mbuzi na kondoo dume, kila mmoja wa miaka mitatu, pamoja na hua na kinda la njiwa.”
And he said to him, Take for me an heifer in her third year, and a she-goat in her third year, and a ram in his third year, and a dove and a pigeon.
10 Abramu akamletea hivi vyote, akampasua kila mnyama vipande viwili, akavipanga kila kimoja kuelekea mwenzake, lakini hata hivyo ndege, hakuwapasua vipande viwili.
So he took to him all these, and divided them in the midst, and set them opposite to each other, but the birds he did not divide.
11 Kisha ndege walao nyama wakatua juu ya mizoga, lakini Abramu akawafukuza.
And birds came down upon the bodies, [even] upon the divided parts of them, and Abram sat down by them.
12 Wakati jua lilipokuwa linatua, Abramu akashikwa na usingizi mzito, giza nene na la kutisha likaja juu yake.
And about sunset a trance fell upon Abram, and behold! a great gloomy terror falls upon him.
13 Kisha Bwana akamwambia, “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.
And it was said to Abram, You shall surely know that your seed shall be a sojourner in a land not their won, and they shall enslave them, and afflict them, and humble them four hundred years.
14 Lakini nitaliadhibu taifa lile watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka huko na mali nyingi.
And the nation whoever they shall serve I will judge; and after this, they shall come forth hither with much property.
15 Wewe, hata hivyo utakwenda kwa baba zako kwa amani na kuzikwa katika uzee mwema.
But you shall depart to your fathers in peace, nourished in a good old age.
16 Katika kizazi cha nne wazao wako watarudi hapa, kwa maana dhambi ya Waamori bado haijafikia kipimo kilichojaa.”
And in the fourth generation they shall return hither, for the sins of the Amorites are not yet filled up, even until now.
17 Wakati jua lilipokuwa limezama na giza limeingia, tanuru la moshi na mwali wa moto unaowaka vikatokea na kupita kati ya vile vipande vya nyama.
And when the sun was about to set, there was a flame, and behold a smoking furnace and lamps of fire, which passed between these divided pieces.
18 Siku hiyo Bwana akafanya Agano na Abramu, na kumwambia, “Nitawapa wazao wako nchi hii, kuanzia Kijito cha Misri hadi mto ule mkubwa, Frati,
In that day the Lord made a covenant with Abram, saying, To your seed I will give this land, from the river of Egypt to the great river Euphrates.
19 yaani nchi ya Wakeni, Wakenizi, Wakadmoni,
The Kenites, and the Kenezites, and the Kedmoneans,
20 Wahiti, Waperizi, Warefai,
and the Chettites, and the Pherezites, and the Raphaim,
21 Waamori, Wakanaani, Wagirgashi na Wayebusi.”
and the Amorites, and the Chananites, and the Evites, and the Gergesites, and the Jebusites.

< Mwanzo 15 >