< Ezra 3 >

1 Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
A gdy nadszedł siódmy miesiąc, a synowie Izraela znajdowali się w miastach, zgromadził się lud jak jeden mąż w Jerozolimie.
2 Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu.
Wtedy powstał Jeszua, syn Jocadaka, ze swymi braćmi kapłanami, oraz Zorobabel, syn Szealtiela, wraz ze swymi braćmi, i zbudowali ołtarz Boga Izraela, aby na nim składać całopalenia, jak jest napisane w Prawie Mojżesza, męża Bożego.
3 Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni.
Potem postawili ołtarz na swoich fundamentach i chociaż bali się sąsiednich narodów, składali na nim PANU całopalenia – rano i wieczorem.
4 Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa.
Obchodzili też Święto Namiotów, jak jest napisane, i [składali] codzienne całopalenia w liczbie ustalonej według zwyczaju na każdy dzień;
5 Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana.
Potem składali całopalenie nieustanne – zarówno w dni nowiu, jak i każde święto poświęcone PANU – oraz [dary] od każdego, kto składał PANU dobrowolną ofiarę.
6 Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
Od pierwszego dnia siódmego miesiąca zaczęli składać PANU całopalenia, chociaż fundamenty świątyni [jeszcze] nie zostały położone.
7 Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.
Dali też pieniądze kamieniarzom i cieślom oraz żywność, napój i oliwę Sydończykom i Tyryjczykom, aby przywozili drzewo cedrowe z Libanu morzem do Jafy, zgodnie z zezwoleniem Cyrusa, króla Persji.
8 Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana.
A w drugim roku po ich przybyciu do domu Bożego w Jerozolimie, w drugim miesiącu, Zorobabel, syn Szealtiela, i Jeszua, syn Jocadaka, i pozostali ich bracia kapłani i Lewici oraz wszyscy, którzy powrócili z niewoli do Jerozolimy, zaczęli [odbudowę], a ustanowili Lewitów od dwudziestu lat wzwyż, aby byli nadzorcami robót wokół domu PANA.
9 Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.
I Jeszua, jego synowie i bracia: Kadmiel i jego synowie, synowie Judy, stanęli jak jeden mąż, aby kierować tymi, którzy pracowali przy [budowie] domu Bożego: synami Chenadada, ich synami i ich braćmi, Lewitami.
10 Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli.
A gdy budowniczowie położyli fundamenty świątyni PANA, postawili kapłanów, ubranych w szaty i z trąbami, oraz Lewitów, synów Asafa, z cymbałami, aby chwalić PANA zgodnie z postanowieniem Dawida, króla Izraela.
11 Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi: “Yeye ni mwema; upendo wake kwa Israeli wadumu milele.” Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa.
I śpiewali jedni po drugich, chwaląc PANA i dziękując mu [za to], że jest dobry – że jego miłosierdzie nad Izraelem [trwa] na wieki. Cały lud wznosił głośny okrzyk, gdy chwalił PANA za to, że zostały położone fundamenty domu PANA.
12 Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha.
Lecz wielu kapłanów, Lewitów i naczelników rodów, którzy byli starcami i widzieli tamten pierwszy dom, głośno płakało, gdy na ich oczach zakładano fundamenty tego domu, wielu natomiast innych głośno krzyczało z radości;
13 Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.
Tak że lud nie mógł odróżnić głośnego krzyku radości od głośnego płaczu ludu. Lud bowiem wznosił tak wielki okrzyk, że było go słychać z daleka.

< Ezra 3 >