< Ezra 3 >

1 Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
After the Israeli people [returned to Israel, and] had begun to live in their towns, (in the autumn of/after the hot season ended in) that year, they all gathered together in Jerusalem.
2 Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu.
Then Jeshua, the son of Jehozadak, and his fellow priests, and Zerubbabel the son of Shealtiel and his friends, all began to rebuild the altar of God, the one whom the Israeli people [worshiped]. They did that in order that they could sacrifice burned offerings on it, according to what the prophet Moses had written in the laws [that God gave to him].
3 Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni.
Even though they were afraid of the people who were already living in that area, they rebuilt the altar at the same place [where the previous altar had been]. Before they started to lay the foundation of Yahweh’s temple, [the priests] started to burn sacrifices to Yahweh [on the altar]. They offered sacrifices every morning and every evening. Fifteen days after [they started to offer these sacrifices], the people celebrated the Festival of [Living in Temporary] Shelters, as [Moses] had commanded them to do in the laws [that God gave to him]. Each day the priests offered the sacrifices [that were required] for that day. In addition, they presented the regular burned offerings and the offerings [that were required] for the New Moon Festivals and the other festivals that they celebrated each year to [honor] Yahweh. They also brought other offerings only because they desired to bring them, [not because they were required to bring them].
4 Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa.
5 Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana.
6 Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
7 Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.
Then the Israelis hired masons and carpenters, and they bought [logs from] cedar trees from the people of Tyre and Sidon [cities], and they gave those people food and wine and olive oil for the logs. They brought the logs down from [the mountains in] Lebanon [to the Mediterranean seacoast and then floated them along the coast of the Sea, ] to Joppa. King Cyrus permitted them to do that. [Then the logs were brought from Joppa inland up to Jerusalem].
8 Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana.
The Israelis started to rebuild the temple in the (spring/time before the hot season) of the second year after they returned to Jerusalem. Zerubbabel and Jeshua and all the people who had returned to Jerusalem worked on the building. All the (Levites/men who did work in the temple) supervised this work.
9 Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.
Jeshua and his sons and his other relatives, and Kadmiel and his sons, who were descendants of Hodaviah, also helped to supervise the work. The family of Henadad, who were also all Levites, joined with them in supervising this work.
10 Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli.
When the builders finished laying the foundation of the temple, the priests put on their robes and stood in their places, blowing their trumpets. Then the Levites, who were descendants of Asaph, clashed/banged their cymbals to praise Yahweh, just as King David had [many years previously] told [Asaph and the other musicians] to do.
11 Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi: “Yeye ni mwema; upendo wake kwa Israeli wadumu milele.” Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa.
They praised Yahweh and thanked him, and they sang this song about him: “He is very good [to us]! He faithfully loves us Israeli people, and he will love us forever.” Then all the people shouted loudly, praising Yahweh because they had finished laying the foundation of Yahweh’s temple.
12 Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha.
Many of the [old] priests, Levites, and leaders of families remembered [what] the first temple [was like], and they cried aloud when they saw the foundation of this temple being laid [because they knew that the new temple would not be as beautiful as the first temple]. But the other people shouted joyfully.
13 Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.
The shouting and the crying was very loud; [even people] far away could hear it.

< Ezra 3 >