< Ezekieli 47 >

1 Yule mtu akanirudisha mpaka kwenye ingilio la Hekalu, nami nikaona maji yakitoka chini ya kizingiti cha Hekalu yakitiririkia upande wa mashariki (kwa maana upande wa mbele wa Hekalu ulielekea mashariki). Maji yalikuwa yakitoka chini upande wa kusini wa Hekalu, kusini mwa madhabahu.
Adam beni tapınağın girişine geri getirdi. Doğuya doğru tapınağın kapı eşiğinin altından sular aktığını gördüm. Tapınak doğuya bakıyordu. Sular tapınağın güney yanının altından, sunağın güneyinden aşağıya akıyordu.
2 Ndipo akanitoa nje kupitia lango la kaskazini na kunizungusha mpaka kwenye lango la nje linaloelekea mashariki, nayo maji yalikuwa yakitiririka kutoka upande wa kusini.
Beni oradan, Kuzey Kapısı'ndan çıkarıp dış yoldan doğuya bakan dış kapıya götürdü. Sular güney yönünden akıyordu.
3 Mtu yule alipokwenda upande wa mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake, akapima dhiraa 1,000 kisha akanipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
Adam elinde bir ölçü ipiyle doğuya doğru gitti. Bin arşın ölçtükten sonra beni ayak bileğine dek çıkan sulara getirdi.
4 Akapima dhiraa 1,000 nyingine na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika magotini. Akapima dhiraa nyingine 1,000 na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kiunoni.
Bin arşın daha ölçtü ve beni dize kadar çıkan sulara getirdi. Bin arşın daha ölçtü, beni bele kadar çıkan sulara getirdi.
5 Akapima tena dhiraa 1,000 nyingine, lakini wakati huu yalikuwa mto ambao sikuweza kuvuka, kwa kuwa maji yalikuwa na kina kirefu ambacho ni cha kuogelea, mto ambao hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kuvuka.
Bin arşın daha ölçtü, içinden geçemediğim bir ırmak oluştu. Sular yükselmişti, içinden yürüyerek karşıya geçilemezdi, yüzülecek kadar derin bir ırmak oluşmuştu.
6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto.
Bana, “İnsanoğlu, bunu gördün mü?” diye sordu. Daha sonra beni ırmağın kıyısına geri getirdi.
7 Nilipofika pale, nikaona idadi kubwa ya miti kila upande wa ule mto.
Oraya varınca, ırmağın her iki kıyısında birçok ağaç gördüm.
8 Akaniambia, “Haya maji yanatiririka kuelekea nchi ya mashariki na kushuka mpaka Araba, ambapo huingia Baharini. Yanapomwagikia kwenye hiyo Bahari, maji yaliyoko humo huponywa na kuwa safi.
Bana şöyle dedi: “Bu sular doğu bölgesine doğru akıyor, oradan Arava Vadisi'ne, sonra Lut Gölü'ne dökülüyor. Göle dökülünce oradaki sular tatlı suya dönüşecek.
9 Popote mto huu uendapo kila kiumbe hai kinachoyaparamia hayo maji kitaishi, nako kutakuwa na samaki wengi mno, mara maji haya yafikapo huko. Maji hayo yatakuwa hai na kila kitu kitakachoishi kule mto uendako.
Irmağın aktığı yerlerde her çeşit canlı yaratık kaynaşacak. Çok sayıda balık olacak. Çünkü bu sular oraya akıyor, oradaki tuzlu suyu tatlı suya dönüştürüyor. Irmak aktığı her yere yaşam getirecek.
10 Wavuvi watasimama kando ya bahari, kuanzia En-Gedi hadi En-Eglaimu huko patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki. Samaki watakuwa wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kuu
Irmak kıyısı boyunca balıkçılar duracak; Eyn-Gedi'den Eyn-Eglayim'e dek ağ gerecek yerler olacak. Akdeniz'deki gibi çok sayıda balık çeşidi olacak.
11 Lakini madimbwi yake na mabwawa yake hayatakuwa na maji yanayofaa kunywa, bali yatabakia kuwa maji ya chumvi.
Ama Lut Gölü'nün çamurlu, bataklık kesimi tatlı suya dönüşmeyecek, tuzla olarak kalacak.
12 Miti ya matunda ya kila aina itaota kwenye kingo zote mbili za mto huu. Majani yake hayatanyauka wala haitaacha kuwa na matunda katika matawi yake. Kila mwezi kutakuwa na matunda, kwa sababu maji yatokayo patakatifu yanaitiririkia. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa dawa.”
Irmağın her iki yanında her çeşit meyve ağacı yetişecek. Yaprakları solmayacak, meyveleri tükenmeyecek. Her ay meyve verecekler, çünkü tapınaktan çıkan sular oraya akıyor. Meyveleri yiyecek olarak, yaprakları şifa için kullanılacak.”
13 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Hii ndiyo mipaka ambayo kwayo mtagawanya hiyo nchi kuwa urithi miongoni mwa hayo makabila kumi na mawili ya Israeli, pamoja na mafungu mawili ya Yosefu.
Egemen RAB şöyle diyor: “Ülkeyi mülk olarak İsrail'in on iki oymağına böleceğiniz sınırlar şöyle olacak: Yusuf'a iki pay düşecek.
14 Mtagawa kwa usawa miongoni mwao. Kwa sababu niliapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu, nchi hii itakuwa urithi wenu.
Ülkeyi on iki oymak arasında eşit olarak paylaşacaksınız. Ülkeyi atalarınıza vereceğime ant içtim. Bu ülke size mülk olarak verilecek.
15 “Huu ndio utakuwa mpaka wa hiyo nchi: “Upande wa kaskazini utaanzia Bahari Kuu kwa njia ya Hethloni kupitia Lebo-Hamathi hadi maingilio ya Sedadi.
“Ülkenin sınırı şöyle olacak: Kuzeyde Akdeniz'den, Hetlon yoluyla Levo-Hamat'a, Sedat'a,
16 Berotha na Sibraimu (ambao uko kwenye mpaka kati ya Dameski na Hamathi), hadi kufikia Haser-Hatikoni, ambao uko katika mpaka wa Haurani.
Berota'ya ve Şam'la Hama'nın toprakları arasında bulunan Sivrayim'e, Havran sınırında Haser-Hattikon'a kadar uzanacak.
17 Hivyo mpaka utaendelea kuanzia Baharini hadi Hasar-Enoni, ukiambaa na mpaka wa kaskazini wa Dameski, pamoja na mpaka wa Hamathi upande wa kaskazini. Huu utakuwa ndio mpaka wa kaskazini.
Sınır denizden Hasar-Enan'a, Şam'ın kuzey sınırı boyunca uzanacak, Hama sınırı kuzeyde olacak. Kuzey sınırı bu olacak.
18 Upande wa mashariki mpaka utapita kati ya Haurani na Dameski, kuambaa Yordani na kati ya Gileadi na nchi ya Israeli, hadi bahari ya mashariki na kufika Tamari. Huu utakuwa ndio mpaka wa mashariki.
“Doğuda sınır Havran'la Şam arasında Gilat'ı İsrail'den ayıran Şeria Irmağı boyunca Lut Gölü'ne ve Tamar'a dek uzanacak. Doğu sınırı bu olacak.
19 Upande wa kusini utaanzia Tamari hadi kufikia maji ya Meriba-Kadeshi, kisha utaambaa na Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu. Huu utakuwa ndio mpaka wa kusini.
“Güneyde sınır Tamar'dan Meriva-Kadeş sularına, Mısır Vadisi boyunca Akdeniz'e dek uzanacak. Güney sınırı bu olacak.
20 Upande wa magharibi, Bahari Kuu itakuwa ndio mpaka hadi kwenye sehemu mkabala na Lebo-Hamathi. Huu utakuwa ndio mpaka wa magharibi.
“Batıda Levo-Hamat'ın karşısındaki noktaya dek Akdeniz sınır oluşturacak. Batı sınırı bu olacak.
21 “Mtagawanya nchi hii miongoni mwenu kufuatana na makabila ya Israeli.
“Bu ülkeyi İsrail oymaklarına göre aranızda paylaşacaksınız.
22 Mtaigawanya kuwa urithi kwa ajili yenu na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwenu na ambao wana watoto. Wao watakuwa kwenu kama wenyeji wazawa wa Israeli, pamoja na ninyi watagawiwa urithi miongoni mwa makabila ya Israeli.
Ülkeyi içinizde yaşayan ve içinizdeyken çocukları olan yabancılarla kendiniz arasında mülk olarak bölüşeceksiniz. Onları İsrail'de doğan yerliler sayacaksınız. Onların da İsrail oymakları arasında sizin gibi mülkleri olacak.
23 Katika kabila lolote mgeni atakapoishi hapo ndipo mtakapompatia urithi wake,” asema Bwana Mwenyezi.
Yabancı hangi oymağa yerleşmişse, orada ona düşen payı mülk olarak vereceksiniz.” Egemen RAB böyle diyor.

< Ezekieli 47 >