< Ezekieli 45 >

1 “‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
Gdy będziecie dzielić tę ziemię w dziedzictwo przez losowanie, oddacie na ofiarę PANU [dział] święty z tej ziemi, długi na dwadzieścia pięć tysięcy [prętów] i szeroki na dziesięć tysięcy. Będzie to święty [dział] we wszystkich waszych granicach dokoła.
2 Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
Z tego będzie kwadrat na świątynię pięćset [prętów długości] na pięćset [szerokości] dokoła; a wokół niego [będzie] wolna przestrzeń na pięćdziesiąt łokci.
3 Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
Z tej [pierwszej] miary odmierzysz dwadzieścia pięć tysięcy długości i dziesięć tysięcy szerokości, a na tym będzie świątynia i Miejsce Najświętsze.
4 Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
Ten święty dział ziemi będzie należeć do kapłanów pełniących służbę w świątyni, którzy przystępują, aby służyć PANU. Będzie to miejsce na ich domy i miejsce święte na świątynię.
5 Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
A [obszar] długi na dwadzieścia pięć tysięcy i szeroki na dziesięć tysięcy też będzie dla Lewitów, którzy służą w domu, na posiadłość [liczącą] dwadzieścia komórek.
6 “‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
A na własność dacie miastu [obszar] szeroki na pięć tysięcy i długi na dwadzieścia pięć tysięcy wzdłuż [działu] świętej ofiary. Będzie to dla całego domu Izraela.
7 “‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
Dla księcia będzie obszar z obu stron [działu] świętej ofiary i własności miasta, przed [działem] świętej ofiary i przed własnością miasta, od strony zachodniej ku zachodowi i od strony wschodniej ku wschodowi, a długość [będzie] naprzeciwko każdego z tych działów od granicy zachodniej [aż] do granicy wschodniej.
8 Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
[Ten dział] ziemi będzie jego posiadłością w Izraelu, a moi książęta nie będą już uciskać mojego ludu; ale wydzielą ziemię domowi Izraela według jego pokoleń.
9 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
Tak mówi Pan BÓG: Dosyć tego, książęta Izraela! Zaniechajcie przemocy i grabieży, wykonujcie sąd i sprawiedliwość i wycofajcie wasze obciążenia od mego ludu, mówi Pan BÓG;
10 Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
Będziecie mieli sprawiedliwe wagi, sprawiedliwą efę i sprawiedliwy bat.
11 Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
Efa i bat będą miały jednakową miarę, tak by bat zawierał dziesiątą część chomera, a także efa dziesiątą część chomera. Chomer będzie podstawą miary.
12 Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
Sykl [będzie miał] dwadzieścia ger. Dwadzieścia syklów, dwadzieścia pięć syklów i piętnaście syklów stanowi dla was minę.
13 “‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
A taka [będzie] ofiara wzniesienia, którą będziecie ofiarowywać: szóstą część efy z chomera pszenicy; [dacie] również szóstą część efy z chomera jęczmienia.
14 Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
Ustawa dotycząca oliwy jest taka: bat jest miarą oliwy. Będziecie dawać dziesiątą część bat z kor, czyli chomer z dziesięciu bat, bo dziesięć bat stanowi chomer.
15 Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
Także jedną owcę z trzody liczącej dwieście [owiec] z bujnych pastwisk Izraela na ofiarę z pokarmów, na całopalenie i na ofiary pojednawcze, aby dokonać przebłagania za nich, mówi Pan BÓG.
16 Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
Cały lud tej ziemi ma składać te ofiary wzniesienia księciu w Izraelu.
17 Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
Na księciu będzie ciążył [obowiązek] całopaleń i ofiar z pokarmów i z płynów na święta, na dni nowiu, na szabaty i na wszystkie uroczyste święta domu Izraela. On będzie sprawować ofiarę za grzech, ofiarę z pokarmów i całopalną oraz ofiary pojednawcze, aby dokonać przebłagania za dom Izraela.
18 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
Tak mówi Pan BÓG: Pierwszego dnia pierwszego miesiąca weźmiesz młodego cielca bez skazy i oczyścisz świątynię.
19 Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
Kapłan weźmie nieco krwi z ofiary za grzech i pomaże odrzwia domu, cztery narożniki podstawy tego ołtarza i odrzwia bramy dziedzińca wewnętrznego.
20 Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
Tak samo uczynisz siódmego dnia tego miesiąca za każdego, który [zgrzeszył] nieświadomie, i za prostego. Tak oczyścicie dom.
21 “‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
W pierwszym miesiącu, czternastego [dnia] tego miesiąca, będziecie mieli święto Paschy, święto siedmiu dni, w [których] będą spożywane chleby przaśne.
22 Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
I w tym dniu książę złoży cielca [na ofiarę] za grzech za siebie i za cały lud tej ziemi.
23 Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Przez siedem dni tego święta będzie ofiarowywać PANU na całopalenie siedem cielców i siedem baranów bez skazy, codziennie, przez siedem dni, a na ofiarę za grzech codziennie jednego kozła.
24 Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
A na ofiarę z pokarmów złoży efę na cielca, efę na barana i hin oliwy na efę.
25 “‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.
W siódmym miesiącu, piętnastego dnia tego miesiąca, w święto, będzie ofiarowywać właśnie to samo przez siedem dni, jak również ofiarę za grzech, całopalenie, ofiarę z pokarmów i oliwę.

< Ezekieli 45 >