< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
La vingt-cinquième année de notre captivité, au commencement de l'année, le dixième jour du mois, la quatorzième année après que la ville eut été ruinée, ce jour-là même, la main de Yahweh fut sur moi, et il m'emmena en ce lieu-là.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
Dans des visions divines il m'emmena au pays d'Israël, et il me plaça sur une montagne très élevée; et sur cette montagne, il y avait comme une construction de ville au midi.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
Quand il m'eut amené là, je vis un homme dont l'aspect était comme l'aspect de l'airain; dans sa main était un cordeau de lin et une canne à mesurer, et il se tenait dans le portique.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
Cet homme me dit: " Fils de l'homme, regarde de tes yeux et écoute de tes oreilles, et applique ton cœur à tout ce que je vais te faire voir, car c'est pour qu'on te le fasse voir que tu as été amené ici. Fais connaître à la maison d'Israël tout ce que tu vas voir. "
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
Et voici qu'un mur extérieur entourait la maison de tous côtés, et l'homme avait à la main un roseau à mesurer de six coudées, chaque coudée étant d'une coudée et un palme. Il mesura la largeur de cette construction: elle était d'un roseau; et la hauteur: elle était d'un roseau.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Puis il alla au portique dont la façade était dans la direction de l'orient, et il en monta les degrés; et il mesura le seuil du portique, qui était d'un roseau en largeur; savoir, le premier seuil, d'un roseau en largeur.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
Chaque loge avait un roseau en longueur et un roseau en largeur; entre les loges, il y avait cinq coudées. Le seuil du portique, du côté du vestibule du portique, du côté de la maison, était d'un roseau.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
Il mesura le vestibule du portique, du côté de la maison; il était d'un roseau.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
Il mesura encore le vestibule du portique: il avait huit coudées, et ses piliers deux coudées. Le vestibule du portique était du côté de la maison.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Les loges du portique oriental étaient au nombre de trois d'un côté, et de trois de l'autre côté; toutes les trois avaient la même mesure, et les piliers de chaque côté avaient aussi la même mesure.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
Il mesura la largeur de l'ouverture du portique: elle était de dix coudées; et la longueur du portique de treize coudées.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
Il y avait devant les loges une clôture d'une coudée de chaque côté; et chaque loge avait six coudées d'un côté et six de l'autre.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
Et il mesura le portique du toit d'une loge jusqu'au toit de l'autre: vingt-cinq coudées en largeur, d'une porte jusqu'à l'autre porte.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
Il compta soixante coudées pour les piliers, et à ces piliers touchait le parvis qui entourait le portique.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
L'espace entre le devant de la porte d'entrée et le devant du vestibule intérieur de la porte était de cinquante coudées.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
Il y avait aux loges, à leurs piliers, des fenêtres grillées du côté intérieur du portique, tout autour; il en était de même aux vestibules; et ainsi il y avait des fenêtres tout autour, donnant à l'intérieur; et aux pilastres il y avait des palmiers.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Puis il me conduisit au parvis extérieur: et voici qu'il y avait des chambres et un pavé disposés tout autour du parvis; il y avait trente chambres le long du pavé.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
Le pavé longeait les portiques, correspondant à la longueur des portiques; c'était le pavé inférieur.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Il mesura la largeur du devant du portique inférieur jusqu'au devant du parvis intérieur: cent coudées, à l'orient et au septentrion.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
Quant au portique du parvis extérieur dont la façade est dans la direction du nord, il en mesura la longueur et la largeur,
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
— ses loges, trois d'un côté et trois de l'autre; ses piliers et son vestibule ayant la même mesure que ceux du premier portique, — cinquante coudées en longueur et vingt-cinq coudées en largeur.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
Ses fenêtres, son vestibule et ses palmiers avaient la même mesure que ceux du portique dont la façade est dans la direction de l'orient; on y montait par sept degrés, et son vestibule était en face des degrés.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
Il y avait un portique au parvis intérieur, en face du portique du septentrion comme en face de celui de l'orient; il mesura d'un portique à l'autre: cent coudées.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
Il me conduisit ensuite dans la direction du midi, et voici un portique dans la direction du midi; il en mesura les pilastres et le vestibule, qui avaient les mêmes dimensions
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
— il avait tout autour, ainsi que son vestibule, des fenêtres pareilles aux autres fenêtres —: cinquante coudées en longueur et vingt-cinq coudées en largeur.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
On y montait par sept degrés, et son vestibule était en face des degrés; il y avait des palmiers à ses pilastres, l'un d'un côté, l'autre de l'autre.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
Le parvis intérieur avait aussi un portique dans la direction du midi; il mesura d'un portique à l'autre dans la direction du midi: cent coudées.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
Il me conduisit dans le parvis intérieur par le portique du midi, et il mesura le portique qui était au midi, qui avait les mêmes dimensions
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
— ses loges, ses pilastres et son vestibule avaient les mêmes dimensions; et il avait, ainsi que son vestibule, des fenêtres tout autour —: cinquante coudées de longueur et vingt-cinq coudées de largeur.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
Il y avait des vestibules tout autour, de vingt-cinq coudées en longueur et de cinq coudées en largeur.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Son vestibule était du côté du parvis extérieur; il avait des palmiers à ses pilastres et huit degrés pour y monter.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
Puis il me conduisit, dans le parvis intérieur, vers la direction de l'orient, et il mesura le portique qui avait les mêmes dimensions
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
— ses loges, ses pilastres et son vestibule avaient les mêmes dimensions; et il avait, ainsi que son vestibule, des fenêtres tout autour — cinquante coudées en longueur et vingt-cinq coudées en largeur.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Son vestibule touchait au parvis extérieur; il avait des palmiers à ses pilastres, d'un côté et de l'autre, et huit degrés pour y monter.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
Puis il me conduisit vers le portique du septentrion, et il y mesura les mêmes dimensions
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
— Il y avait à ses loges, à ses pilastres et à son vestibule des fenêtres tout autour —: cinquante coudées de longueur et vingt-cinq coudées de largeur.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Ses piliers touchaient au parvis extérieur; il y avait des palmiers sur ses pilastres et huit degrés pour y monter.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
Il y avait une chambre, avec sa porte, près des pilastres des portiques; c'est là qu'on lavait les holocaustes.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
Dans le vestibule du portique, il y avait deux tables d'un côté et deux tables de l'autre, sur lesquelles on devait immoler les victimes destinées à l'holocauste, au sacrifice pour le péché et au sacrifice pour le délit.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
Au côté extérieur, au septentrion pour celui qui montait à l'entrée du portique, il y avait deux tables, et de l'autre côté, vers le vestibule du portique, deux tables.
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
Il se trouvait ainsi, sur les côtés de la porte, quatre tables d'une part et quatre tables de l'autre; en tout huit tables, sur lesquelles on devait immoler.
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
Il y avait encore quatre tables servant aux holocaustes, en pierre de taille, longues d'une coudée et demie, larges d'une coudée et demie et hautes d'une coudée, sur lesquelles on posait les instruments avec lesquels on immolait les victimes destinées à l'holocauste et aux autres sacrifices.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
Des crochets d'un palme étaient fixés tout autour de l'édifice; et la chair des sacrifices devait être placée sur les tables.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
En dehors du portique intérieur, il y avait les chambres des chantres, dans le parvis intérieur; celle qui était à côté du portique septentrional, avait sa façade dans la direction du midi; l'autre à côté du portique oriental, avait sa façade dans la direction du nord.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
Il me dit: " Cette chambre dont la façade est dans la direction du midi est pour les prêtres qui sont chargés du service de la maison.
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
Et la chambre dont la façade est dans la direction du nord est pour les prêtres chargés du service de l'autel. " Ce sont les fils de Sadoc qui, parmi les enfants de Lévi, s'approchent de Yahweh pour le servir.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
Puis il mesura le parvis, qui était carré, ayant cent coudées de longueur et cent coudées de largeur. L'autel était devant la maison.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Il me conduisit ensuite vers le vestibule de la maison, et il mesura le pilier du vestibule: cinq coudées d'un côté et cinq coudées de l'autre; et la largeur du portique: trois coudées d'un côté et trois coudées de l'autre.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
La longueur du vestibule était de vingt coudées, et la largeur de onze coudées, aux degrés par lesquels on y montait; et il y avait des colonnes près des piliers, l'une d'un côté, l'autre de l'autre.

< Ezekieli 40 >