< Ezekieli 38 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de l'Éternel me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
Fils de l'homme, tourne ta face vers Gog, au pays de Magog, vers le prince de Rosh, de Méshec et de Tubal, et prophétise contre lui;
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
Et dis: Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Voici, j'en veux à toi, Gog, prince de Rosh, de Méshec et de Tubal;
4 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
Je t'entraînerai, et je mettrai une boucle à tes mâchoires, et je te ferai sortir avec toute ton armée, avec les chevaux et les cavaliers, tous parfaitement équipés, grande multitude armée d'écus et de boucliers, et tous maniant l'épée.
5 Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
Ceux de Perse, d'Éthiopie, de Put, sont avec eux, portant tous des boucliers et des casques;
6 pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
Gomer et toutes ses troupes, la maison de Togarma à l'extrême nord, avec toutes ses troupes, peuples nombreux qui t'accompagnent.
7 “‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
Sois prêt, prépare-toi, toi et toute la multitude assemblée avec toi; sois leur chef.
8 Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
Après beaucoup de jours, tu seras sommé; dans la suite des années tu viendras en un pays délivré de l'épée et rassemblé d'entre plusieurs peuples, sur les montagnes d'Israël, longtemps désertes; maintenant tous ramenés d'entre les nations, ils y habitent en sécurité.
9 Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
Tu t'avanceras, et tu viendras comme l'ouragan; comme une nuée tu couvriras le pays, toi, toutes tes troupes et les nombreux peuples qui sont avec toi.
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: En ces jours-là, des pensées monteront dans ton cœur, et tu formeras de mauvais desseins.
11 Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
Tu diras: Je monterai contre ce pays de villes sans murailles; je fondrai sur des hommes tranquilles, en sécurité dans leurs demeures, habitant tous des villes sans murailles, sans barres, ni portes.
12 Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
J'irai faire du butin et du pillage, mettre la main sur les lieux déserts qui ont été repeuplés, et sur le peuple ramené du milieu des nations, et qui soigne le bétail et ses biens, et habite au centre de la terre.
13 Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
Shéba et Dédan, les marchands de Tarsis et tous ses lionceaux, te diront: Ne viens-tu pas pour enlever du butin, et n'as-tu pas assemblé ta multitude pour faire du pillage, pour emporter de l'argent et de l'or, pour prendre le bétail et les biens, pour enlever un grand butin?
14 “Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
C'est pourquoi, fils de l'homme, prophétise, et dis à Gog: Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Ne sauras-tu pas en ce jour-là qu'Israël, mon peuple, habite en sécurité?
15 Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
Et pourtant tu viendras de ton pays, de l'extrême nord, toi et plusieurs peuples avec toi, tous gens de cheval, une grande multitude et une puissante armée.
16 Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
Tu monteras contre mon peuple d'Israël, pareil à une nuée qui couvre le pays. Ce sera dans les derniers jours; je te ferai marcher contre mon pays, afin que les nations me connaissent, quand je serai sanctifié par toi sous leurs yeux, ô Gog!
17 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: N'est-ce pas de toi que j'ai parlé jadis, par le ministère de mes serviteurs les prophètes d'Israël, qui ont prophétisé alors pendant des années que je te ferai venir contre eux?
18 Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
Mais, en ce jour-là, au jour où Gog marchera contre le pays d'Israël, dit le Seigneur, l'Éternel, la colère me montera au visage.
19 Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
Je le dis dans ma jalousie, dans l'ardeur de ma colère: oui, en ce jour-là, il y aura un grand trouble dans le pays d'Israël.
20 Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
Les poissons de la mer, les oiseaux des cieux, les bêtes des champs et tout reptile qui rampe sur la terre, et tous les hommes qui sont sur la face de la terre, trembleront devant moi; les montagnes seront renversées, les rochers escarpés tomberont, et toutes les murailles s'écrouleront par terre.
21 Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
Et j'appellerai contre lui l'épée sur toutes mes montagnes, dit le Seigneur, l'Éternel; l'épée de chacun se tournera contre son frère.
22 Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
Et j'entrerai en jugement avec lui par la peste et par le sang; je ferai pleuvoir sur lui, sur ses troupes, et sur les grands peuples qui l'accompagnent, une pluie violente, des grêlons, du feu et du soufre.
23 Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
Et je me glorifierai, et je me sanctifierai, et je me ferai connaître aux yeux de nations nombreuses, et elles sauront que je suis l'Éternel.

< Ezekieli 38 >