< Ezekieli 34 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
A palavra de Javé veio a mim, dizendo:
2 “Mwanadamu, tabiri juu ya wachungaji wa Israeli, tabiri na uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wa wachungaji wa Israeli ambao hujitunza wenyewe tu! Je, haiwapasi wachungaji kutunza kundi la kondoo?
“Filho do homem, profetiza contra os pastores de Israel”. Profetiza, e diz-lhes, até mesmo aos pastores: “O Senhor Javé diz: “Ai dos pastores de Israel que se alimentam! Os pastores não deveriam alimentar as ovelhas?
3 Mnakula mafuta ya wanyama, mnavaa mavazi ya sufu na kuchinja kondoo walionona, lakini hamlitunzi kundi.
Você come a gordura. Você se veste com a lã. Você mata os gordos, mas não alimenta as ovelhas.
4 Hamkuwatia nguvu walio dhaifu wala hamkuwaganga wenye maradhi wala kuwafunga waliojeruhiwa. Hamkuwarudisha waliotangatanga wala kuwatafuta wale waliopotea. Badala yake mmewatawala kwa ukali na kwa ukatili.
Você não fortalece os enfermos. Você não curou o que estava doente. Você não amarrou o que estava quebrado. Você não trouxe de volta o que foi expulso. Você não procurou o que estava perdido, mas governou sobre eles com força e com rigor.
5 Hivyo walitawanyika kwa sababu hapakuwepo mchungaji, nao walipotawanyika, wakawa chakula cha wanyama wa mwitu wote.
Eles estavam dispersos, porque não havia pastor. Eles se tornaram alimento para todos os animais do campo, e foram dispersos.
6 Kondoo wangu walitawanyika, wakatangatanga kwenye milima yote na kwenye kila kilima kirefu. Kondoo wangu walitawanyika juu ya uso wa dunia yote bila kuwa na yeyote wa kuwaulizia wala wa kuwatafuta.
Minhas ovelhas perambulavam por todas as montanhas e em todas as colinas altas. Sim, minhas ovelhas estavam espalhadas por toda a superfície da terra. Não havia ninguém que procurasse ou procurasse”.
7 “‘Kwa hiyo, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana:
“'Portanto, vocês pastores, ouçam a palavra de Javé:
8 Kwa hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa sababu kondoo zangu wamekosa mchungaji na hivyo wametekwa nyara na kuwa chakula cha wanyama wote wa mwituni na kwa sababu wachungaji wangu, hawakuwatafuta kondoo zangu, bali wachungaji wamejitunza wenyewe, nao hawakuwalisha kondoo zangu,
“Como eu vivo”, diz o Senhor Javé, “certamente porque minhas ovelhas se tornaram presas, e minhas ovelhas se tornaram alimento para todos os animais do campo, porque não havia pastor, e meus pastores não procuraram minhas ovelhas, mas os pastores se alimentaram, e não alimentaram minhas ovelhas,
9 kwa hiyo enyi wachungaji, sikieni neno la Bwana:
portanto, vocês pastores, ouçam a palavra de Javé”!
10 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na wachungaji nami nitawadai kondoo zangu mikononi mwao. Nitawafukuza kutoka kwenye kuchunga kundi langu, ili wachungaji wasiendelee kujitunza wenyewe. Nitaokoa kondoo zangu kutoka kwenye vinywa vyao, nao kondoo hawatakuwa tena chakula chao.
O Senhor Javé diz: “Eis que eu sou contra os pastores”. Vou exigir minhas ovelhas às mãos deles e fazê-los parar de alimentar as ovelhas”. Os pastores não se alimentarão mais. Entregarei minhas ovelhas da boca deles, para que elas não sejam alimento para eles”.
11 “‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitawaulizia kondoo wangu na kuwatafuta.
“'Pois o Senhor Javé diz: “Eis que eu mesmo, eu mesmo, procurarei minhas ovelhas, e as buscarei”.
12 Kama vile mchungaji atafutavyo kundi lake lililotawanyika wakati akiwa pamoja nalo, hivyo ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawaokoa kutoka mahali pote walipokuwa wametawanyikia katika siku ya mawingu na giza nene.
Como um pastor procura seu rebanho no dia em que está entre suas ovelhas dispersas no exterior, assim procurarei minhas ovelhas”. Vou libertá-las de todos os lugares onde elas foram dispersas no dia nublado e escuro.
13 Nitawatoa katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mbalimbali, nami nitawaleta katika nchi yao wenyewe. Nitawalisha kwenye milima ya Israeli, katika mabonde na mahali pote panapokalika katika nchi.
Eu as tirarei dos povos, as recolherei dos países e as trarei para suas próprias terras. Vou alimentá-los nas montanhas de Israel, junto aos cursos de água e em todos os lugares habitados do país.
14 Nitawachunga kwenye malisho mazuri na miinuko ya mlima wa Israeli patakuwa mahali pao pa malisho. Huko watajipumzisha kwa amani katika nchi ya malisho mazuri, nao watajilisha huko katika malisho tele katika milima ya Israeli.
Alimentá-los-ei com bom pasto, e seu rebanho estará nas montanhas da altura de Israel. Lá eles se deitarão em uma boa prega. Eles se alimentarão de pastos ricos nas montanhas de Israel.
15 Mimi mwenyewe nitawachunga kondoo zangu na kuwafanya wapumzike, asema Bwana Mwenyezi.
Eu mesmo serei o pastor de minhas ovelhas, e as farei deitar”, diz o Senhor Javé.
16 Nitawaulizia kondoo waliopotea na kuwaleta waliotangatanga. Nitawafunga waliojeruhiwa na kuwatia nguvu walio dhaifu lakini wale waliojikinai na wenye nguvu nitawaangamiza. Nitalichunga kundi kwa haki.
“Buscarei o que foi perdido, e trarei de volta o que foi expulso, e amarrarei o que foi quebrado, e fortalecerei o que estava doente; mas destruirei o gordo e o forte”. Alimentá-los-ei com justiça”.
17 “‘Kwa habari yenu, enyi kundi langu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo, kati ya kondoo dume na mbuzi.
“Quanto a você, ó meu rebanho, o Senhor Javé diz: “Eis que eu julgo entre ovelhas e ovelhas, os carneiros e os cabritos machos.
18 Je, haiwatoshi ninyi kujilisha kwenye malisho mazuri? Je, ni lazima ninyi kuyakanyaga pia malisho yenu yaliyobaki kwa miguu yenu? Je, haiwatoshi ninyi kunywa maji safi? Je, ni lazima kuyachafua maji mengine kwa miguu yenu?
Does parece-lhe uma coisa pequena ter se alimentado do bom pasto, mas você deve pisar com seus pés os resíduos de seu pasto...”. E para ter bebido das águas claras, mas você deve sujar os resíduos com seus pés?
19 Je, ni lazima kundi langu wajilishe kwa yale mliyoyakanyaga na kunywa maji mliyoyachafua kwa miguu yenu?
As para minhas ovelhas, elas comem o que você pisou com seus pés, e bebem o que você sujou com seus pés”.
20 “‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi awaambialo: Tazama, mimi mwenyewe nitahukumu kati ya kondoo wanono na waliokonda.
“Portanto, o Senhor Javé lhes diz: “Eis que eu, até mesmo eu, julgarei entre a ovelha gorda e a ovelha magra”.
21 Kwa sababu mmewapiga kikumbo na kuwapiga kwa pembe zenu kondoo wote walio dhaifu mpaka wakawafukuza,
Porque você empurra com o lado e com o ombro, e empurra todos os enfermos com seus chifres, até que você os tenha espalhado para o exterior,
22 nitaliokoa kundi langu na hawatatekwa nyara tena. Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo.
portanto eu salvarei meu rebanho, e eles não serão mais uma presa. Julgarei entre ovelhas e carneiros.
23 Nitaweka juu yao mchungaji mmoja, mtumishi wangu Daudi, naye atawachunga, atawachunga na kuwa mchungaji wao.
eu criarei um pastor sobre elas, e ele as alimentará, inclusive meu servo David. Ele os alimentará e será o pastor deles.
24 Mimi Bwana nitakuwa Mungu wao, naye mtumishi wangu Daudi atakuwa mkuu miongoni mwao. Mimi Bwana nimenena.
Eu, Javé, serei seu Deus, e meu servo Davi príncipe entre eles. Eu, Yahweh, já o disse.
25 “‘Nitafanya nao Agano la amani na kuwaondoa wanyama wa mwitu kutoka nchi yao ili kondoo wangu waweze kupumzika nyikani na msituni kwa salama.
“'Farei com eles um pacto de paz, e farei com que animais malignos cessem de sair da terra. Eles habitarão em segurança no deserto e dormirão na floresta.
26 Nitawabariki wao pamoja na maeneo yanayozunguka kilima changu. Nitawanyeshea mvua kwa majira yake, kutakuwepo mvua za baraka.
farei deles e dos lugares ao redor da minha colina uma bênção. Farei com que o banho desça em sua estação do ano. Haverá chuveiros de bênção.
27 Miti ya shambani itatoa matunda yake na ardhi itatoa mazao yake, watu watakaa salama katika nchi yao. Watajua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya nira zao na kuwaokoa kutoka mikono ya wale waliowafanya watumwa.
A árvore do campo dará seus frutos, e a terra produzirá seu aumento, e eles estarão seguros em suas terras. Então eles saberão que eu sou Yahweh, quando eu tiver quebrado as barras de seu jugo, e os terei libertado da mão daqueles que fizeram deles escravos.
28 Hawatatekwa tena nyara na mataifa, wala wanyama pori hawatawala tena. Wataishi kwa salama, wala hakuna yeyote atakayewatia hofu.
Eles não serão mais uma presa para as nações, nem os animais da terra os devorarão; mas viverão em segurança, e ninguém os fará ter medo.
29 Nitawapa nchi yenye sifa kutokana na mazao yake, hawatapatwa na njaa katika nchi tena wala hawatadharauliwa na mataifa.
Eu levantarei para eles uma plantação de renome, e eles não serão mais consumidos pela fome na terra, e não suportarão mais a vergonha das nações.
30 Ndipo watakapojua kuwa Mimi, Bwana, Mungu wao, niko pamoja nao, na kwamba wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana Mwenyezi.
Eles saberão que eu, Javé, seu Deus estou com eles, e que eles, a casa de Israel, são meu povo, diz o Senhor Javé.
31 Ninyi ni kondoo wangu, kondoo wa malisho yangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu, asema Bwana Mwenyezi.’”
Vós, minhas ovelhas, as ovelhas do meu pasto, sois homens e eu sou vosso Deus”, diz o Senhor Yahweh”.

< Ezekieli 34 >