< Ezekieli 34 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
و کلام خداوند بر من نازل شده، گفت:۱
2 “Mwanadamu, tabiri juu ya wachungaji wa Israeli, tabiri na uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wa wachungaji wa Israeli ambao hujitunza wenyewe tu! Je, haiwapasi wachungaji kutunza kundi la kondoo?
«ای پسر انسان به ضد شبانان اسرائیل نبوت نما و نبوت کرده، به ایشان یعنی به شبانان بگو: خداوند یهوه چنین می‌فرماید: وای بر شبانان اسرائیل که خویشتن را می‌چرانند. آیا نمی بایدشبانان گله را بچرانند؟۲
3 Mnakula mafuta ya wanyama, mnavaa mavazi ya sufu na kuchinja kondoo walionona, lakini hamlitunzi kundi.
شما پیه را می‌خورید وپشم را می‌پوشید و پرواریها را می‌کشید، اما گله را نمی چرانید.۳
4 Hamkuwatia nguvu walio dhaifu wala hamkuwaganga wenye maradhi wala kuwafunga waliojeruhiwa. Hamkuwarudisha waliotangatanga wala kuwatafuta wale waliopotea. Badala yake mmewatawala kwa ukali na kwa ukatili.
ضعیفان را تقویت نمی دهید وبیماران را معالجه نمی نمایید و شکسته‌ها راشکسته بندی نمی کنید و رانده شدگان را پس نمی آورید و گم شدگان را نمی طلبید، بلکه بر آنهابا جور و ستم حکمرانی می‌نمایید.۴
5 Hivyo walitawanyika kwa sababu hapakuwepo mchungaji, nao walipotawanyika, wakawa chakula cha wanyama wa mwitu wote.
پس بدون شبان پراکنده می‌شوند و خوراک همه حیوانات صحرا گردیده، آواره می‌گردند.۵
6 Kondoo wangu walitawanyika, wakatangatanga kwenye milima yote na kwenye kila kilima kirefu. Kondoo wangu walitawanyika juu ya uso wa dunia yote bila kuwa na yeyote wa kuwaulizia wala wa kuwatafuta.
گوسفندان من بر جمیع کوهها و بر همه تلهای بلند آواره شده‌اند. و گله من بر روی تمامی زمین پراکنده گشته، کسی ایشان را نمی طلبد و برای ایشان تفحص نمی نماید.۶
7 “‘Kwa hiyo, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana:
پس‌ای شبانان کلام خداوندرا بشنوید!۷
8 Kwa hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa sababu kondoo zangu wamekosa mchungaji na hivyo wametekwa nyara na kuwa chakula cha wanyama wote wa mwituni na kwa sababu wachungaji wangu, hawakuwatafuta kondoo zangu, bali wachungaji wamejitunza wenyewe, nao hawakuwalisha kondoo zangu,
خداوند یهوه می‌فرماید: به حیات خودم قسم هر آینه چونکه گله من به تاراج رفته وگوسفندانم خوراک همه حیوانات صحرا گردیده، شبانی ندارند. و شبانان من گوسفندانم رانطلبیدند. بلکه شبانان خویشتن را چرانیدند و گله مرا رعایت ننمودند.۸
9 kwa hiyo enyi wachungaji, sikieni neno la Bwana:
«بنابراین‌ای شبانان! کلام خداوند رابشنوید!۹
10 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na wachungaji nami nitawadai kondoo zangu mikononi mwao. Nitawafukuza kutoka kwenye kuchunga kundi langu, ili wachungaji wasiendelee kujitunza wenyewe. Nitaokoa kondoo zangu kutoka kwenye vinywa vyao, nao kondoo hawatakuwa tena chakula chao.
خداوند یهوه چنین می‌فرماید: اینک من به ضد شبانان هستم. و گوسفندان خود را ازدست ایشان خواهم طلبید. و ایشان را از چرانیدن گله معزول خواهم ساخت تا شبانان خویشتن رادیگر نچرانند. و گوسفندان خود را از دهان ایشان خواهم رهانید تا خوراک ایشان نباشند.۱۰
11 “‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitawaulizia kondoo wangu na kuwatafuta.
زیراخداوند یهوه چنین می‌گوید: هان من خودم گوسفندان خویش را طلبیده، آنها را تفقد خواهم نمود.۱۱
12 Kama vile mchungaji atafutavyo kundi lake lililotawanyika wakati akiwa pamoja nalo, hivyo ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawaokoa kutoka mahali pote walipokuwa wametawanyikia katika siku ya mawingu na giza nene.
چنانکه شبان حینی که در میان گوسفندان پراکنده خود می‌باشد، گله خویش راتفقد می‌نماید، همچنان من گوسفندان خویش راتفقد نموده، ایشان را از هر جایی که در روز ابرهاو تاریکی غلیظ پراکنده شده بودند خواهم رهانید.۱۲
13 Nitawatoa katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mbalimbali, nami nitawaleta katika nchi yao wenyewe. Nitawalisha kwenye milima ya Israeli, katika mabonde na mahali pote panapokalika katika nchi.
و ایشان را از میان قوم‌ها بیرون آورده، از کشورها جمع خواهم نمود. و به زمین خودشان درآورده، بر کوههای اسرائیل و در وادیها وجمیع معمورات زمین ایشان را خواهم چرانید.۱۳
14 Nitawachunga kwenye malisho mazuri na miinuko ya mlima wa Israeli patakuwa mahali pao pa malisho. Huko watajipumzisha kwa amani katika nchi ya malisho mazuri, nao watajilisha huko katika malisho tele katika milima ya Israeli.
ایشان را بر مرتع نیکو خواهم چرانید و آرام گاه ایشان بر کوههای بلند اسرائیل خواهد بود. وآنجا در آرام گاه نیکو و مرتع پرگیاه خواهندخوابید. و بر کوههای اسرائیل خواهند چرید.۱۴
15 Mimi mwenyewe nitawachunga kondoo zangu na kuwafanya wapumzike, asema Bwana Mwenyezi.
خداوند یهوه می‌گوید که من گوسفندان خودرا خواهم چرانید و من ایشان را خواهم خوابانید.۱۵
16 Nitawaulizia kondoo waliopotea na kuwaleta waliotangatanga. Nitawafunga waliojeruhiwa na kuwatia nguvu walio dhaifu lakini wale waliojikinai na wenye nguvu nitawaangamiza. Nitalichunga kundi kwa haki.
گم شدگان را خواهم طلبید و رانده شدگان راباز خواهم آورد و شکسته‌ها را شکسته بندی نموده، بیماران را قوت خواهم داد. لیکن فربهان وزورآوران را هلاک ساخته، بر ایشان به انصاف رعایت خواهم نمود.۱۶
17 “‘Kwa habari yenu, enyi kundi langu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo, kati ya kondoo dume na mbuzi.
و اما به شما‌ای گوسفندان من، خداوند یهوه چنین می‌فرماید: هان من در میان گوسفند و گوسفند و در میان قوچهای و بزهای نر داوری خواهم نمود.۱۷
18 Je, haiwatoshi ninyi kujilisha kwenye malisho mazuri? Je, ni lazima ninyi kuyakanyaga pia malisho yenu yaliyobaki kwa miguu yenu? Je, haiwatoshi ninyi kunywa maji safi? Je, ni lazima kuyachafua maji mengine kwa miguu yenu?
آیا برای شما کم بود که مرتع نیکو راچرانیدید بلکه بقیه مرتع خود را نیز به پایهای خویش پایمال ساختید؟ و آب زلال را نوشیدیدبلکه باقی‌مانده را به پایهای خویش گل آلودساختید؟۱۸
19 Je, ni lazima kundi langu wajilishe kwa yale mliyoyakanyaga na kunywa maji mliyoyachafua kwa miguu yenu?
و گوسفندان من آنچه را که از پای شما پایمال شده است، می‌چرند و آنچه را که به پای شما گل آلود گشته است، می‌نوشند.۱۹
20 “‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi awaambialo: Tazama, mimi mwenyewe nitahukumu kati ya kondoo wanono na waliokonda.
بنابراین خداوند یهوه به ایشان چنین می‌گوید: هان من خودم در میان گوسفندان فربه وگوسفندان لاغر داوری خواهم نمود.۲۰
21 Kwa sababu mmewapiga kikumbo na kuwapiga kwa pembe zenu kondoo wote walio dhaifu mpaka wakawafukuza,
چونکه شما به پهلو و کتف خود تنه می‌زنید و همه ضعیفان را به شاخهای خود می‌زنید، حتی اینکه ایشان را بیرون پراکنده ساخته‌اید،۲۱
22 nitaliokoa kundi langu na hawatatekwa nyara tena. Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo.
پس من گله خود را نجات خواهم داد که دیگر به تاراج برده نشوند و در میان گوسفند و گوسفند داوری خواهم نمود.۲۲
23 Nitaweka juu yao mchungaji mmoja, mtumishi wangu Daudi, naye atawachunga, atawachunga na kuwa mchungaji wao.
و یک شبان بر ایشان خواهم گماشت که ایشان را بچراند یعنی بنده خود داودرا که ایشان را رعایت بنماید و او شبان ایشان خواهد بود.۲۳
24 Mimi Bwana nitakuwa Mungu wao, naye mtumishi wangu Daudi atakuwa mkuu miongoni mwao. Mimi Bwana nimenena.
و من یهوه خدای ایشان خواهم بود و بنده من داود در میان ایشان رئیس خواهدبود. من که یهوه هستم گفته‌ام.۲۴
25 “‘Nitafanya nao Agano la amani na kuwaondoa wanyama wa mwitu kutoka nchi yao ili kondoo wangu waweze kupumzika nyikani na msituni kwa salama.
و عهد سلامتی را با ایشان خواهم بست. و حیوانات موذی را اززمین نابود خواهم ساخت و ایشان در بیابان به امنیت ساکن شده، در جنگلها خواهند خوابید.۲۵
26 Nitawabariki wao pamoja na maeneo yanayozunguka kilima changu. Nitawanyeshea mvua kwa majira yake, kutakuwepo mvua za baraka.
و ایشان را و اطراف کوه خود را برکت خواهم ساخت. و باران را در موسمش خواهم بارانید وبارشهای برکت خواهد بود.۲۶
27 Miti ya shambani itatoa matunda yake na ardhi itatoa mazao yake, watu watakaa salama katika nchi yao. Watajua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya nira zao na kuwaokoa kutoka mikono ya wale waliowafanya watumwa.
و درختان صحرامیوه خود را خواهند‌آورد و زمین حاصل خویش را خواهد داد. و ایشان در زمین خود به امنیت ساکن خواهند شد. و حینی که چوبهای یوغ ایشان را شکسته و ایشان را از دست آنانی که ایشان را مملوک خود ساخته بودند رهانیده باشم، آنگاه خواهند دانست که من یهوه هستم.۲۷
28 Hawatatekwa tena nyara na mataifa, wala wanyama pori hawatawala tena. Wataishi kwa salama, wala hakuna yeyote atakayewatia hofu.
ودیگر در میان امت‌ها به تاراج نخواهد رفت وحیوانات صحرا ایشان را نخواهند خورد بلکه به امنیت، بدون ترساننده‌ای ساکن خواهند شد.۲۸
29 Nitawapa nchi yenye sifa kutokana na mazao yake, hawatapatwa na njaa katika nchi tena wala hawatadharauliwa na mataifa.
وبرای ایشان درختستان ناموری بر پا خواهم داشت. و دیگر از قحط در زمین تلف نخواهندشد. و بار دیگر متحمل سرزنش امت‌ها نخواهندگردید.۲۹
30 Ndipo watakapojua kuwa Mimi, Bwana, Mungu wao, niko pamoja nao, na kwamba wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana Mwenyezi.
و خداوند یهوه می‌گوید: خاندان اسرائیل خواهند دانست که من یهوه خدای ایشان با ایشان هستم و ایشان قوم من می‌باشند.۳۰
31 Ninyi ni kondoo wangu, kondoo wa malisho yangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu, asema Bwana Mwenyezi.’”
وخداوند یهوه می‌گوید: شما‌ای گله من و‌ای گوسفندان مرتع من، انسان هستید و من خدای شما می‌باشم.»۳۱

< Ezekieli 34 >