< Ezekieli 29 >

1 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Bwana likanijia kusema:
I det tiende Aar, i den tiende Maaned, paa den tolvte Dag i Maaneden kom Herrens Ord til mig saaledes:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote.
Du Menneskesøn! vend dit Ansigt imod Farao, Kongen af Ægypten, og spaa imod ham og imod al Ægypten.
3 Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako. Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe; niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”
Tal og sig: Saa siger den Herre, Herre: Se, jeg kommer imod dig, Farao, Konge i Ægypten, du, som er den store Drage, der ligger midt i sine Strømme, og som siger: Min Strøm er min, og jeg har skabt mig den.
4 Lakini nitatia ndoana katika mataya yako nami nitawafanya samaki wa vijito vyako washikamane na magamba yako. Nitakutoa katikati ya vijito vyako, pamoja na samaki wote walioshikamana na magamba yako.
Men jeg vil kaste Kroge i dine Kæver og lade Fiskene i dine Strømme hænge ved dine Skæl, og jeg vil trække dig op midt af dine Strømme tillige med alle de Fisk i dine Strømme, der hænge ved dine Skæl.
5 Nitakutupa jangwani, wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa au kuchukuliwa. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama wa nchi na ndege wa angani.
Og jeg vil kaste dig ud i Ørken, dig og alle Fisk fra dine Strømme, paa Marken skal du falde hen, du skal ikke samles til Hobe og ej sankes op, jeg har givet dig til Dyrene i Landet og til Fuglene under Himmelen som Føde.
6 Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli.
Og alle Ægyptens Indbyggere skulle fornemme, at jeg er Herren. Fordi de have været Israels Hus en Rørkæp —
7 Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.
naar de gribe din Haand, knækker du og splitter dem hver Skulder; og naar de støtte sig paa dig, sønderbrydes du og bringer dem alle Lænder til at vakle —
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao.
derfor, saa siger den Herre, Herre: Se, jeg lader et Sværd komme over dig, og jeg vil udrydde Mennesker og Kvæg af dig.
9 Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,”
Og Ægyptens Land skal blive til Ødelæggelse og Øde; og de skulle fornemme, at jeg er Herren. Fordi han siger: Det er min Strøm, og jeg har skabt den:
10 kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia.
Derfor se! vil jeg komme til dig og til dine Strømme og gøre Ægyptens Land til aldeles øde Ørkener, fra Migdol til Sy ene, og indtil Morlands Landemærke.
11 Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini.
Der skal ikke gaa Menneskefod igennem det, og Fæs Fod skal ikke gaa der igennem; og det skal ikke bebos i fyrretyve Aar.
12 Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine.
Og jeg vil gøre Ægyptens Land til et Øde midt iblandt de ødelagte Lande, og dets Stæder skulle blive øde midt iblandt de ødelagte Stæder, fyrretyve Aar; og jeg vil adsprede Ægypterne iblandt Folkene og strø dem ud i Landene.
13 “‘Lakini hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa.
Thi saa siger den Herre, Herre: Naar fyrretyve Aar ere til Ende, vil jeg samle Ægypterne hjem fra Folkene, hvorhen de vare adspredte.
14 Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu.
Og jeg vil vende Ægyptens Fangenskab og føre dem tilbage til Pathros Land, til deres Stammeland, og de skulle der være et ringe Rige.
15 Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine.
Det skal være ringe fremfor andre Riger og ikke ophøje sig ydermere over Folkene; og jeg vil gøre dem ubetydelige, at de ikke skulle regere over Folkene.
16 Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’”
Og det skal ikke ydermere være Israels Hus til Fortrøstning, saa at det bringer mig deres Synd i Erindring, naar disse vende sig om efter dem, og de skulle fornemme, at jeg er den Herre, Herre.
17 Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
Og det skete i det syv og tyvende Aar, i den første Maaned, paa den første Dag i Maaneden, at Herrens Ord kom til mig saaledes:
18 “Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro.
Du Menneskesøn! Nebukadnezar, Kongen af Babel, har paalagt sin Krigshær et svart Arbejde imod Tyrus, saa at hvert Hoved er skaldet og hver Skulder opslidt, og Løn har han og hans Hær ikke faaet ud af Tyrus for det Arbejde, han har haft med den.
19 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake.
Derfor, saa siger den Herre, Herre: Se, jeg giver Nebukadnezar, Kongen af Babel, Ægyptens Land, og han skal tage dets Gods og bytte dets Bytte og røve dets Rov, og det skal være Løn for hans Hær.
20 Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mwenyezi.
Som hans Løn, for hvilken han har tjent imod den, har jeg givet ham Ægyptens Land; thi for mig have de tjent, siger den Herre, Herre.
21 “Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”
Paa den Dag vil jeg lade et Horn skyde op for Israels Hus, og dig vil jeg give en opladt Mund midt iblandt dem; og de skulle fornemme, at jeg er Herren.

< Ezekieli 29 >