< Ezekieli 11 >

1 Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
Potem duch uniósł mnie i zaprowadził do wschodniej bramy domu PANA, która jest zwrócona na wschód. A oto u wejścia tej bramy [było] dwudziestu pięciu mężczyzn, wśród których zobaczyłem Jaazaniasza, syna Azzura, i Pelatiasza, syna Benajasza, książąt ludu.
2 Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
Wtedy powiedział mi: Synu człowieczy, to są mężczyźni, [którzy] obmyślają nieprawość i dają złe rady w tym mieście;
3 Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
Mówią: To nie tak blisko, budujmy domy. Oto [miasto] jest kotłem, a my – mięsem.
4 Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
Dlatego prorokuj przeciwko nim, prorokuj, synu człowieczy!
5 Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
Wtedy zstąpił na mnie Duch PANA i powiedział do mnie: Mów: Tak mówi PAN: Tak mówiliście, domu Izraela. Znam bowiem wszystko, co wam przychodzi na myśl.
6 Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
Zabiliście wielkie mnóstwo [ludzi] w tym mieście i napełniliście ulice zabitymi.
7 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
Dlatego tak mówi Pan BÓG: Wasi zabici, których położyliście w środku miasta, są mięsem, a miasto – kotłem. Lecz wyprowadzę was z niego.
8 Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.
Baliście się miecza, a ja sprowadzę na was miecz, mówi Pan BÓG.
9 Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
A wyprowadzę was z niego, wydam was w ręce obcych i wykonam nad wami sądy.
10 Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Padniecie od miecza, osądzę was na granicy Izraela i dowiecie się, że ja jestem PANEM.
11 Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
Miasto nie będzie dla was kotłem ani wy nie będziecie w nim mięsem; na granicy Izraela osądzę was.
12 Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
I dowiecie się, że ja jestem PANEM, ponieważ nie postępowaliście według moich ustaw, nie wykonaliście moich sądów, ale czyniliście według sądów tych pogan, którzy [są] dokoła was.
13 Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
A gdy prorokowałem, umarł Pelatiasz, syn Benajasza. Wtedy upadłem na twarz i zawołałem donośnym głosem: Ach, Panie BOŻE! Czy doszczętnie wyniszczysz resztkę Izraela?
14 Neno la Bwana likanijia kusema:
I doszło do mnie słowo PANA mówiące:
15 “Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
Synu człowieczy, twoi bracia, [właśnie] twoi bracia, twoi krewni i cały dom Izraela [są tymi], do których mówili mieszkańcy Jerozolimy: Oddalcie się od PANA. Nam została dana ta ziemia w posiadanie.
16 “Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’
Dlatego mów: Tak mówi Pan BÓG: Chociaż wygnałem ich daleko pomiędzy pogan i chociaż rozproszyłem ich po krajach, jednak przez krótki czas będę dla nich świątynią w krajach, do których przybędą.
17 “Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
Dlatego mów: Tak mówi Pan BÓG: Zgromadzę was z pogan i zbiorę was z krajów, do których zostaliście rozproszeni, i dam wam ziemię Izraela.
18 “Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.
Wejdą tam i usuną z niej wszystkie jej plugastwa i wszystkie jej obrzydliwości.
19 Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
I dam im jedno serce, i włożę nowego ducha w wasze wnętrze; usunę z ich ciała serce kamienne, a dam im serce mięsiste;
20 Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
Aby postępowali według moich ustaw i strzegli moich sądów oraz czynili je. I będą moim ludem, a ja będę ich Bogiem.
21 Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”
Ale co do tych, których serce chodzi za żądzami ich plugastw i obrzydliwości, złożę im na głowę ich własną drogę, mówi Pan BÓG.
22 Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
Wtedy cherubiny podniosły swoje skrzydła i wraz z nimi koła, a chwała Boga Izraela [była] nad nimi u góry.
23 Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.
I odeszła chwała PANA z pośrodku miasta, i stanęła na górze, która [jest] na wschód od miasta.
24 Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
A duch uniósł mnie i przyprowadził w widzeniu przez Ducha Bożego do ziemi Chaldei, do pojmanych. I odeszło ode mnie widzenie, które miałem.
25 nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.
Następnie opowiedziałem pojmanym te wszystkie rzeczy, które PAN mi ukazał.

< Ezekieli 11 >