< Ezekieli 11 >

1 Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
Moreover the spirit lifted me up, and brought me unto the east gate of the LORD’S house, which looketh eastward: and behold, at the door of the gate five and twenty men; and I saw in the midst of them Jaazaniah the son of Azzur, and Pelatiah the son of Benaiah, princes of the people.
2 Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
And he said unto me, Son of man, these are the men that devise iniquity, and that give wicked counsel in this city.
3 Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
which say, [The time] is not near to build houses: this [city] is the caldron, and we be the flesh.
4 Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
Therefore prophesy against them, prophesy, O son of man.
5 Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
And the spirit of the LORD fell upon me, and he said unto me, Speak, Thus saith the LORD: Thus have ye said, O house of Israel; for I know the things that come into your mind.
6 Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
Ye have multiplied your slain in this city, and ye have filled the streets thereof with the slain.
7 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
Therefore thus saith the Lord GOD: Your slain whom ye have laid in the midst of it, they are the flesh, and this [city] is the caldron: but ye shall be brought forth out of the midst of it.
8 Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.
Ye have feared the sword; and I will bring the sword upon you, saith the Lord GOD.
9 Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
And I will bring you forth out of the midst thereof, and deliver you into the hands of strangers, and will execute judgments among you.
10 Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Ye shall fall by the sword; I will judge you in the border of Israel; and ye shall know that I am the LORD.
11 Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
This [city] shall not be your caldron, neither shall ye be the flesh in the midst thereof; I will judge you in the border of Israel;
12 Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
and ye shall know that I am the LORD: for ye have not walked in my statutes, neither have ye executed my judgments, but have done after the ordinances of the nations that are round about you.
13 Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
And it came to pass, when I prophesied, that Pelatiah the son of Benaiah died. Then fell I down upon my face, and cried with a loud voice, and said, Ah Lord GOD! wilt thou make a full end of the remnant of Israel?
14 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the LORD came unto me, saying,
15 “Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
Son of man, thy brethren, even thy brethren, the men of thy kindred, and all the house of Israel, all of them, [are they] unto whom the inhabitants of Jerusalem have said, Get you far from the LORD; unto us is this land given for a possession:
16 “Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’
Therefore say, Thus saith the Lord GOD: Whereas I have removed them far off among the nations, and whereas I have scattered them among the countries, yet will I be to them a sanctuary for a little while in the countries where they are come.
17 “Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
Therefore say, Thus saith the Lord GOD: I will gather you from the peoples, and assemble you out of the countries where ye have been scattered, and I will give you the land of Israel.
18 “Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.
And they shall come thither, and they shall take away all the detestable things thereof and all the abominations thereof from thence.
19 Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
And I will give them one heart, and I will put a new spirit within you; and I will take the stony heart out of their flesh, and will give them an heart of flesh:
20 Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
that they may walk in my statutes, and keep mine ordinances, and do them: and they shall be my people, and I will be their God.
21 Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”
But as for them whose heart walketh after the heart of their detestable things and their abominations, I will bring their way upon their own heads, saith the Lord GOD.
22 Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
Then did the cherubim lift up their wings, and the wheels were beside them; and the glory of the God of Israel was over them above.
23 Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.
And the glory of the LORD went up from the midst of the city, and stood upon the mountain which is on the east side of the city.
24 Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
And the spirit lifted me up, and brought me in the vision by the spirit of God into Chaldea, to them of the captivity. So the vision that I had seen went up from me.
25 nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.
Then I spake unto them of the captivity all the things that the LORD had shewed me.

< Ezekieli 11 >