< Ezekieli 1 >

1 Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
In the thirtieth year, the fourth month, and the fifth day of the month, it came about that I was living among the captives by the Kebar Canal. The heavens opened, and I saw visions of God.
2 Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
On the fifth day of that month—it was the fifth year of the exile of King Jehoiachin—
3 neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
the word of Yahweh came to Ezekiel son of Buzi the priest, in the land of the Chaldeans by the Kebar Canal, and the hand of Yahweh was upon him there.
4 Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
Then I looked, and there was a windstorm coming from the north; a great cloud with fire flashing within it and brightness surrounding it and inside of it, and the fire was the color of amber inside the cloud.
5 Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
In the middle was the likeness of four living creatures. This was their appearance: They had the likeness of a man,
6 lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
but they had four faces each, and each of the creatures had four wings.
7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
Their legs were straight, but the soles of their feet were like the hooves of a calf that shone like polished bronze.
8 Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
Yet they had human hands under their wings on all four sides. For all four, their faces and wings were like this:
9 nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
their wings were touching the wings of the next creature, and they did not turn as they went; instead, each one went straight forward.
10 Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
The likeness of their faces was like the face of a man. The four of them had the face of a lion to the right side, and the four of them had the face of an ox on the left side. They four had also the face of an eagle.
11 Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
Their faces were like that, and their wings were spread out above, so that each creature had a pair of wings that touched another creature's wing, and also a pair of wings that covered their bodies.
12 Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
Each went straight forward, so that wherever the Spirit directed them to go, they went without turning.
13 Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
As for the likeness of the living creatures, their appearance was like burning coals of fire, like the appearance of torches; bright fire also moved about among the creatures, and there were flashes of lightning.
14 Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
The living creatures were moving swiftly back and forth, and they had the appearance of lightning!
15 Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
Then I looked at the living creatures; and I saw one wheel on the ground beside each of living creatures with its four faces.
16 Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
This was the appearance and structure of the wheels: Each wheel was like beryl, and the four had the same likeness; their appearance and structure was like a wheel intersecting another wheel.
17 Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
As they moved, they went in any of their four directions, without turning as they went.
18 Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
As for their rims, they were high and fearsome, for the rims were full of eyes round about.
19 Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
Whenever the living creatures moved, the wheels moved beside them. When the living creatures rose up from the earth, the wheels also rose up.
20 Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Wherever the Spirit would go, they went, and the wheels rose up beside them, for the spirit of the living creature was in the wheels.
21 Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Whenever the creatures moved, the wheels also moved; and when the creatures stood still, the wheels stood still; when the creatures rose up from the earth, the wheels rose up beside them, because the spirit of the living creature was in the wheels.
22 Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
Over the heads of the living creatures was the likeness of an expansive dome; it looked like awe-inspiring crystal stretched out over their heads above.
23 Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
Beneath the dome, each one of the creature's wings stretched out straight and touched another creature's wings. Each of the living creatures also had a pair to cover themselves; each had a pair to cover his own body.
24 Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
Then I heard the sound of their wings. Like the noise of many waters. Like the voice of the Almighty whenever they moved. Like the sound of a rainstorm. Like the sound of an army. Whenever they stood still, they lowered their wings.
25 Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
A voice came from above the dome over their heads whenever they stood still and lowered their wings.
26 Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
Above the dome over their heads was the likeness of a throne that was like the appearance of a sapphire stone, and on the likeness of the throne was a likeness like the appearance of a man.
27 Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
I saw a figure with the appearance of glowing metal with fire in it from the appearance of his hips up; I saw from the appearance of his hips downward the appearance of fire and brightness all around.
28 Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.
Like the appearance of a rainbow in the clouds on a rainy day was the appearance of the bright light surrounding it. It was the appearance of the likeness of the glory of Yahweh. When I saw it, I fell on my face, and I heard a voice speaking.

< Ezekieli 1 >