< Kutoka 9 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
Potem PAN powiedział do Mojżesza: Idź do faraona i powiedz mu: Tak mówi PAN, Bóg Hebrajczyków: Wypuść mój lud, aby mi służył;
2 Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
Bo jeśli będziesz się wzbraniał go wypuścić i nadal będziesz go zatrzymywał;
3 mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
Oto ręka PANA będzie na twoje stada, które [są] na polu, na koniach, na osłach, na wielbłądach, na wołach i na owcach. [Będzie] bardzo ciężka zaraza.
4 Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
PAN rozdzieli stada Izraela i stada Egiptu, aby nie zdechło nic ze wszystkiego, co należy do synów Izraela.
5 Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
I PAN wyznaczył czas, mówiąc: Jutro PAN to uczyni na [tej] ziemi.
6 Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
Nazajutrz PAN tak uczynił. Pozdychały wszystkie stada Egiptu, lecz ze stad synów Izraela nie zdechło ani jedno.
7 Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
Faraon posłał więc [na zwiady], a oto z bydła Izraela nie zdechło ani jedno. Ale serce faraona pozostało zatwardziałe i nie wypuścił ludu.
8 Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
Potem PAN powiedział do Mojżesza i Aarona: Weźcie pełne garści popiołu z pieca i niech Mojżesz rozrzuci go ku niebu na oczach faraona.
9 Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
Zamieni się w pył na całej ziemi Egiptu, który spowoduje wrzody pęczniejące ropą na ludziach i na zwierzętach na całej ziemi Egiptu.
10 Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
Wzięli więc popiół z pieca i stanęli przed faraonem, a Mojżesz rozrzucił popiół ku niebu i powstały wrzody pęczniejące ropą na ludziach i na zwierzętach.
11 Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
Czarownicy zaś nie mogli stanąć przed Mojżeszem z powodu wrzodów, bo wrzody były na nich i na wszystkich Egipcjanach.
12 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
I PAN zatwardził serce faraona, i [ten] nie posłuchał ich, jak PAN zapowiedział Mojżeszowi.
13 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
PAN powiedział do Mojżesza: Wstań rano, stań przed faraonem i powiedz mu: Tak mówi PAN, Bóg Hebrajczyków: Wypuść mój lud, aby mi służył;
14 au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
Tym razem bowiem ześlę wszystkie moje plagi na twoje serce, na twoje sługi i na twój lud, abyś wiedział, że nie ma równego mi na całej ziemi.
15 Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
Bo teraz wyciągnę rękę i uderzę ciebie i twój lud zarazą, i będziesz wytracony z ziemi.
16 Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
Lecz dlatego cię postawiłem, aby okazać na tobie moją moc i żeby rozgłaszano moje imię na całej ziemi.
17 Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
A ty jeszcze się wynosisz [i stajesz] przeciw memu ludowi, nie chcąc go wypuścić?
18 Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
Jutro o tej porze spuszczę bardzo ciężki grad, jakiego nie było w Egipcie od dnia jego założenia aż do tego czasu.
19 Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
Poślij więc teraz i zgromadź swoje bydło i wszystko, co masz na polu; [bo] każdy człowiek i każde zwierzę, które znajdzie się na polu, a nie zostanie zegnane do domu, zginie, gdy na nich spadnie grad.
20 Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
Kto więc ze sług faraona uląkł się słowa PANA, kazał uciekać swym sługom wraz z bydłem do domu;
21 Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
Ale kto nie wziął do serca słowa PANA, ten zostawił swe sługi i bydło na polu.
22 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
PAN powiedział do Mojżesza: Wyciągnij rękę ku niebu, by spadł grad na całej ziemi Egiptu, na ludzi, na bydło i na wszelkie rośliny polne w ziemi Egiptu.
23 Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
I Mojżesz wyciągnął swą laskę ku niebu, a PAN zesłał grzmoty i grad i na ziemię zstąpił ogień. PAN spuścił grad na ziemię Egiptu.
24 mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
I był grad i ogień zmieszany z bardzo ciężkim gradem, jakiego nie było w całej ziemi Egiptu, odkąd stał się narodem.
25 Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
Grad poraził na całej ziemi Egiptu cokolwiek było na polu, od człowieka aż do zwierzęcia. Poraził też wszelkie rośliny polne i połamał wszystkie drzewa na polu;
26 Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
Tylko w ziemi Goszen, gdzie mieszkali synowie Izraela, nie było gradu.
27 Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
Faraon kazał więc wezwać Mojżesza i Aarona i powiedział do nich: Tym razem zgrzeszyłem. PAN jest sprawiedliwy, a ja i mój lud jesteśmy niegodziwi.
28 Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
Wstawcie się u PANA, aby ustały Boże grzmoty i grad, bo [już] dość. Wypuszczę was i nie będziecie [tu] dłużej mieszkać.
29 Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
Mojżesz powiedział do niego: Gdy wyjdę z miasta, wyciągnę ręce do PANA, a grzmoty ustaną i nie będzie więcej gradu, abyś wiedział, że ziemia należy do PANA.
30 Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
Ale wiem, że ty i twoi słudzy jeszcze nie boicie się PANA Boga.
31 (Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
Len i jęczmień zostały zbite, bo jęczmień miał już kłosy, a len zakwitł.
32 Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
Pszenica jednak i żyto nie zostały zbite, bo były późniejsze.
33 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
Mojżesz wyszedł więc od faraona za miasto i wyciągnął ręce do PANA. Ustały wtedy grzmoty i grad, a deszcz nie padał na ziemię.
34 Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
Kiedy faraon zobaczył, że deszcz, grad i grzmoty ustały, jeszcze bardziej zgrzeszył i zatwardził serce, on i jego słudzy.
35 Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.
I serce faraona pozostało zatwardziałe i nie wypuścił synów Izraela, jak PAN zapowiedział przez Mojżesza.

< Kutoka 9 >