< Waefeso 3 >

1 Kwa sababu hii, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi watu wa Mataifa:
For this cause, I Paul, the prisoner of Christ Jesus for you the nations,
2 Kwa hakika mmekwisha kusikia kuhusu ile huduma ya neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu,
if, indeed, you heard of the dispensation of the grace of God that was given to me in regard to you,
3 yaani, ile siri iliodhihirishwa kwangu kwa njia ya ufunuo, kama nilivyotangulia kuandika kwa kifupi.
that by revelation He made known to me the secret, according as I wrote before in few [words]—
4 Kwa kusoma haya, basi mtaweza kuelewa ufahamu wangu katika siri ya Kristo.
in regard to which you are able, reading [it], to understand my knowledge in the secret of the Christ,
5 Siri hii haikudhihirishwa kwa wanadamu katika vizazi vingine kama vile sasa ilivyodhihirishwa na Roho kwa mitume na manabii watakatifu wa Mungu.
which in other generations was not made known to the sons of men, as it was now revealed to His holy apostles and prophets in the Spirit—
6 Siri hii ni kwamba, kwa njia ya Injili, watu wa Mataifa ni warithi pamoja na Israeli, viungo vya mwili mmoja na washiriki pamoja wa ahadi katika Kristo Yesu.
that the nations are fellow-heirs, and of the same body, and partakers of His promise in the Christ, through the good news,
7 Nimekuwa mtumishi wa Injili hii kwa kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa nguvu yake itendayo kazi.
of which I became a servant, according to the gift of the grace of God that was given to me, according to the working of His power;
8 Ingawa mimi ni mdogo kuliko aliye mdogo kabisa miongoni mwa watakatifu wote, nilipewa neema hii: ili niwahubirie watu wa Mataifa kuhusu utajiri usiopimika ulio ndani ya Kristo,
to me—the less than the least of all the holy ones—was given this grace, among the nations to proclaim good news—the untraceable riches of the Christ,
9 na kuweka wazi kwa kila mtu siri hii iliyokuwa imefichwa tangu zamani katika Mungu, aliyeumba vitu vyote. (aiōn g165)
and to cause all to see what [is] the fellowship of the secret that has been hid from the ages in God, who created all things by Jesus Christ, (aiōn g165)
10 Ili sasa kwa njia ya Kanisa, hekima yote ya Mungu ipate kujulikana kwa watawala na wenye mamlaka katika ulimwengu wa roho,
that there might be made known now to the principalities and the authorities in the heavenly [places], through the Assembly, the manifold wisdom of God,
11 sawasawa na kusudi lake la milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn g165)
according to a purpose of the ages, which He made in Christ Jesus our Lord, (aiōn g165)
12 Ndani yake na kwa njia ya imani katika yeye twaweza kumkaribia Mungu kwa uhuru na kwa ujasiri.
in whom we have the freedom and the access in confidence through the faith of Him,
13 Kwa hiyo, nawaomba msikate tamaa kwa sababu ya mateso yangu kwa ajili yenu, hayo ni utukufu wenu.
for this reason, I ask [you] not to faint in my tribulations for you, which is your glory.
14 Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,
For this cause I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
15 ambaye ubaba wote wa kila jamaa za mbinguni na za duniani unatokana naye.
of whom the whole family in the heavens and on earth is named,
16 Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kwa njia ya Roho wake kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
that He may give to you, according to the riches of His glory, to be strengthened through His Spirit with might, in regard to the inner man,
17 ili kwamba, Kristo apate kukaa mioyoni mwenu kwa njia ya imani. Nami ninaomba kwamba ninyi mkiwa wenye mizizi tena imara katika msingi wa upendo,
that the Christ may dwell through the faith in your hearts, having been rooted and founded in love,
18 mwe na uwezo wa kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, urefu, kimo na kina upendo wa Kristo,
that you may be in strength to comprehend, with all the holy ones, what [is] the breadth, and length, and depth, and height,
19 na kujua upendo huu unaopita fahamu, ili mpate kujazwa na kufikia kipimo cha ukamilifu wote wa Mungu.
to know also the love of the Christ that is exceeding the knowledge, that you may be filled—to all the fullness of God;
20 Basi kwa yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu yasiyopimika kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya uweza wake ule utendao kazi ndani yetu,
and to Him who is able to do exceedingly [and] abundantly above all things that we ask or think, according to the power that is working in us,
21 yeye atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote, milele na milele. Amen. (aiōn g165)
to Him [is] the glory in the Assembly in Christ Jesus, to all the generations of the age of the ages. Amen. (aiōn g165)

< Waefeso 3 >