< Mhubiri 3 >

1 Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:
Jest pora na wszystko i czas na każdą sprawę pod niebem.
2 wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kungʼoa yaliyopandwa,
[Jest] czas rodzenia i czas umierania, czas sadzenia i czas wyrywania tego, co zasadzono;
3 wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga,
Czas zabijania i czas leczenia, czas burzenia i czas budowania;
4 wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,
Czas płaczu i czas śmiechu, czas smutku i czas pląsów;
5 wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe, wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia,
Czas rzucania kamieni i czas zbierania kamieni, czas uścisków i czas powstrzymywania się od uścisków;
6 wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuweka na wakati wa kutupa,
Czas szukania i czas tracenia, czas zachowania i czas wyrzucania;
7 wakati wa kurarua na wakati wa kushona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza,
Czas rozdzierania i czas zszywania, czas milczenia i czas mówienia;
8 wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
Czas miłowania i czas nienawiści, czas wojny i czas pokoju.
9 Mfanyakazi anapata faida gani kutokana na taabu yake?
Jaki pożytek ma ten, kto pracuje, z całego swego trudu?
10 Nimeona mzigo Mungu alioweka juu ya wanadamu.
Widziałem pracę, którą Bóg dał synom ludzkim, aby się nią trudzili.
11 Amefanya kila kitu kiwe kizuri kwa wakati wake. Pia ameiweka hiyo milele katika mioyo ya wanadamu, wala hawawezi kutambua kwa kina yale ambayo Mungu amefanya tangu mwanzo hadi mwisho.
Wszystko dobrze uczynił w swoim czasie. Włożył także świat w ich serca, mimo że człowiek nie zdoła pojąć dzieła, którego Bóg dokonuje od początku do końca.
12 Ninajua kwamba hakuna kitu bora kwa wanadamu kuliko kuwa na furaha na kutenda mema wakati wanapoishi.
Dlatego wiem, że dla nich nie ma nic lepszego nad to, by się radowali i czynili dobrze za swego życia.
13 Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.
Również i to, gdy każdy człowiek je i pije, i cieszy się dobrem całego swego trudu, jest darem Boga.
14 Ninajua kwamba kila kitu anachokifanya Mungu kitadumu milele, hakuna kinachoweza kuongezwa au kupunguzwa. Mungu hufanya hivyo ili watu wamche yeye.
Wiem i to, że cokolwiek czyni Bóg, będzie trwać na wieki. Nie można do tego nic dodać ani z tego odjąć, a Bóg czyni to, aby ludzie się go bali.
15 Chochote kilichopo kilishakuwepo, na kitakachokuwepo kimekwishakuwepo kabla; naye Mungu huyaita yale yaliyopita yarudi tena.
To, co było, jest teraz, a to, co będzie, już było. Bóg bowiem żąda tego, co przeminęło.
16 Pia nikaona kitu kingine tena chini ya jua: Mahali pa kutolea hukumu, uovu ulikuwepo, mahali pa kupatia haki, uovu ulikuwepo.
Widziałem jeszcze pod słońcem niegodziwość w miejscu sądu, a w miejscu sprawiedliwości – nieprawość.
17 Nikafikiri moyoni mwangu, “Mungu atawaleta hukumuni wote wawili wenye haki na waovu, kwa maana kutakuwako na wakati kwa ajili ya kila jambo, wakati kwa ajili ya kila tendo.”
I powiedziałem w sercu: Bóg osądzi zarówno sprawiedliwego, jak i niegodziwego, gdyż tam będzie czas na [osądzenie] każdego zamiaru i uczynku.
18 Pia nikafikiri, “Kuhusu wanadamu, Mungu huwajaribu ili wajione kwamba wao ni kama wanyama.
Powiedziałem w sercu o sprawie synów ludzkich: Oby Bóg im pokazał, aby wiedzieli, że są tylko zwierzętami.
19 Hatima ya mwanadamu ni kama ile ya wanyama; wote wana mwisho unaofanana: Jinsi anavyokufa mnyama, ndivyo anavyokufa mwanadamu. Wote wana pumzi inayofanana; mwanadamu hana cha zaidi kuliko mnyama. Kila kitu ni ubatili.
Bo jednakowy jest los synów ludzkich i los zwierząt. Jak umiera ten, tak umiera i tamto. Wszyscy mają jednakowe tchnienie, a nie ma człowiek przewagi nad zwierzęciem, gdyż wszystko jest marnością.
20 Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi.
Wszystko to idzie do jednego miejsca; wszystko jest z prochu i wszystko w proch się obraca.
21 Ni nani ajuaye kama roho ya mtu huenda juu na roho ya mnyama hushuka chini ardhini?”
A któż wie, że duch synów ludzkich idzie w górę, a duch zwierzęcia zstępuje do ziemi?
22 Kwa hiyo nikaona kwamba hakuna kitu kilicho bora zaidi kwa mwanadamu kuliko kuifurahia kazi yake, kwa sababu hilo ndilo fungu lake. Kwa maana ni nani awezaye kumrudisha ili aje kuona kile kitakachotendeka baada yake?
Dlatego zobaczyłem, że nie ma nic lepszego nad to, żeby człowiek się radował ze swoich dzieł, gdyż to jest jego dział. Któż bowiem doprowadzi go [do tego], aby poznał to, co ma być po nim?

< Mhubiri 3 >