< Torati 3 >

1 Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
Potem zawróciliśmy i poszliśmy drogą w kierunku Baszanu. I wyszedł nam naprzeciw Og, król Baszanu – on i cały jego lud – by stoczyć z nami bitwę w Edrei.
2 Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
Wtedy PAN powiedział do mnie: Nie bój się go, gdyż wydałem go w twoje ręce wraz z całym jego ludem i ziemią; uczynisz mu, jak uczyniłeś Sichonowi, królowi Amorytów, który mieszkał w Cheszbonie.
3 Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
PAN, nasz Bóg, wydał więc w nasze ręce również Oga, króla Baszanu, i cały jego lud. Pobiliśmy go tak, że nikt po nim nie pozostał.
4 Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
Zdobyliśmy w tym czasie wszystkie jego miasta; nie było miasta, którego im nie zabraliśmy: sześćdziesiąt miast, całą krainę Argob, królestwo Oga w Baszanie.
5 Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
Wszystkie te miasta [były] obwarowane wysokimi murami, bramami i ryglami, a oprócz tego [było] bardzo wiele nieobwarowanych miasteczek.
6 Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
I spustoszyliśmy je, jak uczyniliśmy Sichonowi, królowi Cheszbonu, zniszczyliśmy we wszystkich miastach mężczyzn, kobiety i dzieci.
7 Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
Lecz całe bydło i łupy z miast zgarnęliśmy dla siebie.
8 Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
W tym czasie wzięliśmy również z ręki dwóch królów Amorytów ziemię, która leży po tej stronie Jordanu, od rzeki Arnon aż do góry Hermon;
9 (Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
(Sydończycy nazywają Hermon Sirionem, a Amoryci – Sanirem).
10 Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
Wszystkie miasta na równinie i cały Gilead oraz cały Baszan aż do Salka i Edrei, miasta królestwa Oga w Baszanie.
11 (Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
Gdyż tylko sam Og, król Baszanu, pozostał z olbrzymów; a jego łoże, łoże żelazne, czy nie [znajduje się] w Rabbie synów Ammona? Długie na dziewięć łokci, a szerokie na cztery łokcie, według łokcia męskiego.
12 Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
A ziemię, którą wzięliśmy w posiadanie w tym czasie od Aroeru, który leży nad rzeką Arnon, i połowę góry Gilead oraz jej miasta dałem Rubenitom i Gadytom.
13 Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
A resztę Gileadu i cały Baszan, królestwa Oga, dałem połowie pokolenia Manassesa: całą krainę Argob i cały Baszan nazwano ziemią olbrzymów.
14 Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
Jair, syn Manassesa, posiadł całą krainę Argob aż do granicy Geszurytów i Machaty i nazwał ją od swego imienia Baszan-Chawot-Jair; [nazywa się tak] aż do dziś.
15 Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
Makirowi zaś dałem Gilead.
16 Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
A Rubenitom i Gadytom dałem [krainę] od Gileadu aż do rzeki Arnon, ze środkiem rzeki jako granicą, aż do rzeki Jabbok, [która jest] granicą synów Ammona;
17 Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
Do tego równinę i Jordan z granicą od Kinneret aż do Morza Równinnego, czyli Morza Słonego, pod górą Pizga na wschodzie.
18 Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
W tym czasie rozkazałem wam: PAN, wasz Bóg, dał wam tę ziemię w posiadanie. Pójdziecie uzbrojeni przed waszymi braćmi, synami Izraela, wszyscy wojownicy.
19 Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
Tylko wasze żony i dzieci oraz wasze bydło (gdyż wiem, że macie wiele stad) zostaną w waszych miastach, które wam dałem.
20 mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
Aż PAN da odpoczynek waszym braciom, jak również wam, i [aż] oni posiądą ziemię, którą PAN, wasz Bóg, dał im za Jordanem. Wtedy każdy wróci do swojej posiadłości, którą wam dałem.
21 Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
W tym czasie przykazałem też Jozuemu: Twoje oczy widziały wszystko, co PAN, wasz Bóg, uczynił tym dwom królom. Tak samo uczyni PAN wszystkim królestwom, do których pójdziesz.
22 Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
Nie bójcie się ich, ponieważ sam PAN, wasz Bóg, walczy za was.
23 Wakati huo nilimsihi Bwana:
I prosiłem PANA w tym czasie:
24 “Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
Panie BOŻE, ty zacząłeś okazywać twemu słudze swoją wielkość i swoją potężną rękę; któryż bóg na niebie albo na ziemi potrafi czynić takie potężne dzieła jak ty?
25 Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
Pozwól mi, proszę, przejść i zobaczyć tę dobrą ziemię, która jest za Jordanem, tę dobrą górę i Liban.
26 Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
Lecz PAN rozgniewał się na mnie z waszego powodu i nie wysłuchał mnie. I PAN powiedział do mnie: Dosyć, nie mów już do mnie w tej sprawie.
27 Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
Wejdź na szczyt [góry] Pizga i podnieś oczy na zachód, na północ, na południe i na wschód, i przypatrz się [temu] własnymi oczami, gdyż nie przejdziesz tego Jordanu;
28 Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
Ale rozkaż Jozuemu, zachęć go i wzmocnij, gdyż on pójdzie przed tym ludem i on da mu w dziedzictwo ziemię, którą zobaczysz.
29 Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.
Mieszkaliśmy więc w dolinie naprzeciw Bet-Peor.

< Torati 3 >