< Danieli 11 >

1 Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
W pierwszym roku Dariusza Meda stanąłem, aby go pokrzepić i wzmocnić.
2 “Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
A teraz oznajmię ci prawdę: Oto jeszcze trzej królowie będą panować w Persji, potem czwarty wzbogaci się o wiele bardziej niż wszyscy, a gdy się umocni w swoich bogactwach, podburzy wszystkich przeciw królestwu Grecji.
3 Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
I powstanie potężny król, który będzie sprawował wielką władzę, i będzie czynił według swojej woli.
4 Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
A gdy on się umocni, jego królestwo zostanie pokruszone i rozdzielone na cztery strony świata, ale nie między jego potomków i nie według władzy, jaką sprawował. Jego królestwo bowiem zostanie wykorzenione, a [dostanie się] innym, ale nie tym.
5 “Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
Wtedy umocni się król południa oraz jeden z jego książąt. Ten będzie mocniejszy od niego i będzie panować, a jego władza będzie władzą rozległą.
6 Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
Lecz po upływie kilku lat połączą się, bo córka króla południa przybędzie do króla północy, aby zawrzeć przymierze. Ona jednak nie otrzyma siły ramienia ani on nie ostoi się ze swoim ramieniem. Ale zostanie ona wydana, a [z nią] ci, którzy ją sprowadzili, jej syn oraz ten, co ją umacniał w tych czasach.
7 “Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
Potem z latorośli jej korzenia powstanie [ktoś] na jego miejsce, kto nadciągnie ze swoim wojskiem, wkroczy do twierdzy króla północy, będzie rządził nimi i zwycięży.
8 Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
Także ich bogów wraz z ich książętami i drogimi naczyniami ze srebra i złota uprowadzi do niewoli [do] Egiptu; i będzie bezpieczny [przez wiele] lat od króla północy.
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
A król południa wtargnie do królestwa i wróci do swojej ziemi.
10 Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
Ale jego synowie będą walczyć i zgromadzą mnóstwo wielkich wojsk. [Jeden z nich] nadciągnie z siłą jak powódź i przejdzie. Potem wróci i wojskiem będzie nacierać aż do jego twierdzy.
11 “Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
Wtedy król południa, będąc rozjuszony, wyruszy i będzie walczył z nim, [to jest] z królem północy. Uszykuje wielkie mnóstwo, ale to mnóstwo zostanie wydane w jego rękę.
12 Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
A gdy to mnóstwo zostanie rozbite, jego serce się wywyższy, a choć powali dziesiątki tysięcy, nie umocni się.
13 Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
Wróci bowiem król północy i uszykuje większe mnóstwo niż poprzednie, i po upływie kilku lat przyjdzie na pewno z wielkim wojskiem i mnóstwem bogactw.
14 “Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
W tych czasach wielu powstanie przeciwko królowi południa. Synowie zbójców spośród twego ludu powstaną, aby utwierdzić widzenie, ale upadną.
15 Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
Nadciągnie więc król północy, usypie wały i zdobędzie miasta warowne, a nie oprą się ramiona południa ani jego lud wybrany, i nie będą mieć siły, by stawić opór.
16 Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
[Ten], który nadciągnie przeciwko niemu, uczyni według swojej woli, i nie [będzie] nikogo, kto by mu się przeciwstawił; stanie też w pięknej ziemi, która zostanie zniszczona przez jego rękę.
17 Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
Potem zwróci swoją twarz, aby przyjść z siłą całego swego królestwa, i będzie wyglądał, jakby [szukał zgody], i uczyni tak: da mu córkę piękną, aby doprowadził go przez nią do zguby. Ale ona nie [będzie] go wspierać ani nie będzie za nim.
18 Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
Potem zwróci swoją twarz ku wyspom i zdobędzie [ich] wiele. Ale [pewien] wódz położy kres jego zniewadze, ponadto odpłaci mu za tę zniewagę.
19 Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
Dlatego zwróci swoją twarz ku twierdzom swojej ziemi, lecz potknie się i upadnie, i nie będzie [już] znaleziony.
20 “Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
I powstanie na jego miejsce [taki], który roześle poborców w chwale królestwa. Ale po niewielu dniach zostanie zniszczony, lecz nie w gniewie ani nie w bitwie.
21 “Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
Potem powstanie na jego miejsce [człowiek] godny pogardy, któremu nie dadzą godności królestwa. Przyjdzie jednak w pokoju i zdobędzie królestwo pochlebstwem.
22 Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
A ramionami, [jakby] powodzią, zostaną porwani sprzed jego oblicza i skruszeni, a także książę przymierza.
23 Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
Po zawarciu przymierza z nim będzie postępował zdradliwie. Nadciągnie bowiem i umocni się z niewielkim ludem.
24 Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
Nieoczekiwanie wkroczy nawet do najbogatszych miejsc prowincji i uczyni to, czego nie czynili jego ojcowie ani ojcowie jego ojców. Łup, zdobycz i bogactwo rozdzieli między nich. Uknuje plany przeciw warowniom, ale do czasu.
25 “Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
Potem pobudzi swoją moc i [swe] serce przeciw królowi południa z wielkim wojskiem. Król południa przygotuje się do walki z wielkim i potężnym wojskiem, ale się nie oprze, gdyż obmyślą przeciwko niemu zdradę.
26 Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
Ci, którzy jedzą jego chleb, zniszczą go, gdy jego wojsko najedzie jak powódź, i padnie wielu zabitych.
27 Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
Obaj królowie w swych sercach [będą mieli] złe zamiary i przy jednym stole będą mówić kłamstwa; ale to się [im] nie uda, gdyż koniec będzie w jeszcze [innym] wyznaczonym czasie.
28 Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
Potem powróci do swojej ziemi z wielkim bogactwem, a jego serce zwróci się przeciwko świętemu przymierzu; tak będzie działał i wróci do swojej ziemi.
29 “Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
W czasie wyznaczonym wróci i skieruje się na południe, ale nie powiedzie [mu] się tak [jak] za pierwszym i drugim [razem].
30 Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
Przeciwko niemu bowiem wyruszą okręty z Kittim, będzie przygnębiony, wróci i rozgniewa się na święte przymierze; tak będzie działał. I znowu wróci, i zawrze porozumienie z tymi, którzy opuścili święte przymierze.
31 “Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
A powstaną przez niego wojska, które zbezczeszczą świątynię-twierdzę i [zniosą] codzienną [ofiarę], a postawią obrzydliwość spustoszenia.
32 Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
A tych, którzy będą postępować niegodziwie przeciwko przymierzu, splugawi pochlebstwem. Ale lud znający swego Boga umocni się i będzie działać.
33 “Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
A rozumni wśród ludu będą nauczać wielu, ale będą padać od miecza, od ognia, od niewoli i od łupu przez wiele dni.
34 Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
Gdy padną, będą mieli niewielką pomoc i wielu przyłączy się do nich pochlebstwem.
35 Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
Spośród tych rozumnych niektórzy padną, aby byli doświadczeni, oczyszczeni i wybieleni aż do czasu ostatecznego, bo to jeszcze potrwa aż do czasu wyznaczonego.
36 “Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
A król uczyni według swojej woli, wyniesie się i wywyższy się ponad każdego boga; będzie mówić dziwne rzeczy przeciwko Bogu bogów i poszczęści mu się, aż dokona się gniew. [To] bowiem, [co] zostało postanowione, dokona się.
37 Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
Nie będzie miał względu ani na boga swoich ojców, ani na pożądanie kobiet, ani na żadnego boga, gdyż wyniesie się ponad wszystko.
38 Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
Zamiast tego będzie czcił boga twierdz; boga, którego nie znali jego ojcowie, będzie czcił złotem, srebrem i drogocennymi kamieniami, i kosztownościami.
39 Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
Tak postąpi w twierdzach obcego boga, a którego uzna i obdarzy sławą. I sprawi, że będą panowali nad wieloma, i rozdzieli [im] ziemię jako zapłatę.
40 “Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
A pod koniec czasu będzie z nim walczył król południa; ale król północy uderzy na niego jak burza z rydwanami, jeźdźcami i licznymi okrętami, wtargnie do krajów, zaleje [je] i przejdzie.
41 Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
Potem wkroczy do pięknej ziemi i wiele [krajów] padnie. Te jednak ujdą z jego rąk: Edom, Moab i pierwsi z synów Ammona.
42 Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
Wyciągnie swą rękę po kraje, a ziemia Egiptu nie zdoła mu ujść.
43 Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
Opanuje skarby złota i srebra oraz wszystkie kosztowności Egiptu, a Libijczycy i Etiopczycy pójdą za nim.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
Ale wieści ze wschodu i z północy przestraszą go. Dlatego wyruszy z wielkim gniewem, aby wielu wygubić i wytępić.
45 Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.
I rozbije namioty swego pałacu między morzami na pięknej górze świętej; ale jego koniec przyjdzie na niego i nikt mu nie pomoże.

< Danieli 11 >