< Danieli 1 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja akazingira Yerusalemu kwa jeshi.
In the third year of the reign of Jehoiakim king of Judah, Nebuchadnezzar king of Babylonia came to Jerusalem and surrounded the city to cut off all supplies to it.
2 Bwana akamtia Yehoyakimu mfalme wa Yuda mkononi mwa Nebukadneza, pamoja na baadhi ya vyombo kutoka Hekalu la Mungu. Hivi akavichukua hadi kwenye hekalu la mungu wake huko Shinari, naye akaviweka nyumbani ya hazina ya mungu wake.
The Lord gave Nebuchadnezzar victory over Jehoiakim king of Judah, and he gave him some of the sacred objects from the house of God. He brought them into the land of Babylonia, to the house of his god, and he placed the sacred objects in his god's treasury.
3 Kisha mfalme akamwagiza Ashpenazi, mkuu wa maafisa wa mfalme, kumletea baadhi ya Waisraeli kutoka jamaa ya mfalme na kutoka jamaa kuu,
The king spoke to Ashpenaz, his chief official, to bring in some of the people of Israel, both of the royal family and of the nobility—
4 vijana wanaume wasio na dosari mwilini, wenye sura nzuri, wanaoonyesha kipaji katika kila aina ya elimu, wenye ufahamu mzuri, wepesi kuelewa, na waliofuzu kuhudumu katika jumba la kifalme. Alikuwa awafundishe lugha na maandiko ya Wakaldayo.
young men without blemish, attractive in appearance, skillful in all wisdom, filled with knowledge and understanding, and qualified to serve in the king's palace. He was to teach them the Babylonians' literature and language.
5 Mfalme akawaagizia kiasi cha chakula na divai ya kila siku kutoka meza ya mfalme. Walikuwa wafundishwe kwa miaka mitatu, na hatimaye waingie kwenye utumishi wa mfalme.
The king counted out for them a daily portion of his delicacies and some of the wine that he drank. These young men were to be trained for three years, and after that, they would serve the king.
6 Baadhi ya hawa vijana walitoka Yuda: nao ni Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria.
Among these were Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah, some of the people of Judah.
7 Mkuu wa maafisa akawapa majina mapya: Danieli akamwita Belteshaza, Hanania akamwita Shadraki, Mishaeli akamwita Meshaki, na Azaria akamwita Abednego.
The chief official gave them names: Daniel he called Belteshazzar, Hananiah he called Shadrach, Mishael he called Meshach, and Azariah he called Abednego.
8 Lakini Danieli alikusudia kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme na divai, naye akamwomba mkuu wa maafisa ruhusa ili asijinajisi kwa njia hii.
But Daniel intended in his mind that he would not pollute himself with the king's delicacies or with the wine that he drank. So he asked permission from the chief official that he might not pollute himself.
9 Basi Mungu alikuwa amemfanya huyo mkuu wa maafisa kuonyesha upendeleo na huruma kwa Danieli,
Now God gave Daniel favor and compassion through the respect that the chief official had for him.
10 lakini huyo mkuu wa maafisa akamwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme, aliyeagizia chakula na kinywaji chenu. Kwa nini aone nyuso zenu zikiwa mbaya kuliko za vijana wengine wa rika lenu? Mfalme atakata kichwa changu kwa sababu yenu.”
The chief official said to Daniel, “I am afraid of my master the king. He has commanded what food and drink you should have. Why should he see you looking worse than the other young men of your own age? The king might have my head because of you.”
11 Ndipo Danieli akamwambia mlinzi aliyeteuliwa na huyo mkuu wa maafisa kuwasimamia Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria,
Then Daniel spoke to the steward whom the chief official had assigned over Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah.
12 “Tafadhali wajaribu watumishi wako kwa siku kumi. Usitupe chochote ila nafaka na mboga za majani tule, na maji ya kunywa.
He said, “Please test us, your servants, for ten days. Give us only some vegetables to eat and water to drink.
13 Baadaye ulinganishe sura zetu na vijana wanaokula chakula cha mfalme, ukawatendee watumishi wako kulingana na unachoona.”
Then compare our appearance with the appearance of the young men who eat the king's delicacies, and treat us, your servants, based on what you see.”
14 Basi akakubali jambo hili, akawajaribu kwa siku kumi.
So the steward agreed with him to do this, and he tested them for ten days.
15 Mwisho wa zile siku kumi, walionekana kuwa na afya na kunawiri zaidi kuliko yeyote kati ya wale vijana waliokula chakula cha mfalme.
At the end of ten days their appearance was more healthy, and they were better nourished, than all the young men who ate the king's delicacies.
16 Hivyo mlinzi wao akaondoa chakula chao na divai yao waliopangiwa kula na kunywa, akawapa nafaka na mboga za majani badala yake.
So the steward took away their delicacies and their wine and gave them only vegetables.
17 Mungu akawapa hawa vijana wanne maarifa na ufahamu wa kila aina ya maandiko na elimu. Naye Danieli aliweza kufahamu maono na aina zote za ndoto.
As for these four young men, God gave them knowledge and insight in all literature and wisdom, and Daniel could understand all kinds of visions and dreams.
18 Mwisho wa muda uliowekwa na mfalme kuwaingiza kwake, mkuu wa maafisa akawaleta mbele ya Mfalme Nebukadneza.
At the end of the time set by the king to bring them in, the chief official brought them in before Nebuchadnezzar.
19 Mfalme akazungumza nao, akaona hakuna aliyelingana na Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria. Hivyo wakaingia katika utumishi wa mfalme.
The king spoke with them, and among the whole group there were none to compare with Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah. They stood before the king, ready to serve him.
20 Katika kila jambo la hekima na ufahamu kuhusu kile mfalme alichowauliza, aliwaona bora mara kumi zaidi kuliko waganga na wasihiri wote katika ufalme wake wote.
In every question of wisdom and understanding that the king asked them, he found them ten times better than all the magicians and those who claimed to speak with the dead, who were in his entire kingdom.
21 Naye Danieli akabaki huko mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi.
Daniel was there until the first year of King Cyrus.

< Danieli 1 >