< Wakolosai 3 >

1 Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu.
If however you have risen with Christ, seek the things that are above, where Christ is, enthroned at God's right hand.
2 Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani.
Give your minds to the things that are above, not to the things that are on the earth.
3 Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
For you have died, and your life is hidden with Christ in God.
4 Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
When Christ appears--He is our true Life--then you also will appear with Him in glory.
5 Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu.
Therefore put to death your earthward inclinations--fornication, impurity, sensual passion, unholy desire, and all greed, for that is a form of idolatry.
6 Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja.
It is on account of these very sins that God's anger is coming,
7 Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo.
and you also were once addicted to them, while you were living under their power.
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu.
But now you must rid yourselves of every kind of sin--angry and passionate outbreaks, ill-will, evil speaking, foul-mouthed abuse--so that these may never soil your lips.
9 Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake,
Do not speak falsehoods to one another, for you have stripped off the old self with its doings,
10 nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake.
and have clothed yourselves with the new self which is being remoulded into full knowledge so as to become like Him who created it.
11 Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.
In that new creation there is neither Greek nor Jew, circumcision nor uncircumcision, barbarian, Scythian, slave nor free man, but Christ is everything and is in all of us.
12 Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
Clothe yourselves therefore, as God's own people holy and dearly loved, with tender-heartedness, kindness, lowliness of mind, meekness, long-suffering;
13 Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
bearing with one another and readily forgiving each other, if any one has a grievance against another. Just as the Lord has forgiven you, you also must forgive.
14 Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.
And over all these put on love, which is the perfect bond of union;
15 Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani.
and let the peace which Christ gives settle all questionings in your hearts, to which peace indeed you were called as belonging to His one Body; and be thankful.
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
Let the teaching concerning Christ remain as a rich treasure in your hearts. In all wisdom teach and admonish one another with psalms, hymns, and spiritual songs, and sing with grace in your hearts to God.
17 Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.
And whatever you do, in word or in deed, do everything in the name of the Lord Jesus, and let it be through Him that you give thanks to God the Father.
18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.
Married women, be submissive to your husbands, as is fitting in the Lord.
19 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.
Married men, be affectionate to your wives, and do not treat them harshly.
20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.
Children be obedient to your parents in everything; for that is right for Christians.
21 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
Fathers, do not fret and harass your children, or you may make them sullen and morose.
22 Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana.
Slaves, be obedient in everything to your earthly masters; not in acts of eye service, as aiming only to please men, but with simplicity of purpose, because you fear the Lord.
23 Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu,
Whatever you are doing, let your hearts be in your work, as a thing done for the Lord and not for men.
24 kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia.
For you know that it is from the Lord you will receive the inheritance as your reward. Christ is the Master whose bondservants you are.
25 Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.
The man who perpetrates a wrong will find the wrong repaid to him; and with God there are no merely earthly distinctions.

< Wakolosai 3 >