< Amosi 7 >

1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
To mi ukazał Pan BÓG. Oto tworzył koniki polne na początku odrastania potrawu, a oto [był] to potraw po sianokosach królewskich.
2 Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
A gdy zjadły trawę ziemi, powiedziałem: Panie BOŻE! Przebacz, proszę. Któż zostanie Jakubowi? Jest bowiem malutki.
3 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
I żałował tego PAN. PAN powiedział: To się nie stanie.
4 Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
To mi ukazał Pan BÓG: Oto Pan BÓG wezwał ogień w celu sądu, a wchłonął wielką głębię i strawił dział.
5 Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
Wtedy powiedziałem: Panie BOŻE! Zaniechaj [tego], proszę. Któż zostanie Jakubowi? Jest bowiem malutki.
6 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
I żałował tego PAN. Pan BÓG powiedział: I to się nie stanie.
7 Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
Potem [to] mi ukazał: oto Pan stał na murze [wybudowanym] za pomocą pionu, z pionem w ręku.
8 Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
I PAN powiedział do mnie: Co widzisz, Amosie? Odpowiedziałem: Pion. Wtedy Pan powiedział: Oto przyłożę pion pośród mojego ludu, Izraela. Już mu więcej nie odpuszczę.
9 “Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
Wyżyny Izaaka będą spustoszone i świątynie Izraela zostaną zburzone, i powstanę z mieczem przeciwko domowi Jeroboama.
10 Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
Wtedy Amazjasz, kapłan Betel, posłał do Jeroboama, króla Izraela, taką wiadomość: Amos spiskuje przeciwko tobie pośród domu Izraela, [tak że] ziemia nie może znieść wszystkich jego słów.
11 Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
Tak bowiem mówi Amos: Jeroboam umrze od miecza, a Izrael na pewno zostanie uprowadzony ze swojej ziemi do niewoli.
12 Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
Potem Amazjasz powiedział do Amosa: Widzący, idź, uciekaj do ziemi Judy i tam jedz chleb, i tam prorokuj.
13 Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
A w Betel już więcej nie prorokuj, bo to jest świątynia króla i dom królewski.
14 Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
Wtedy Amos odpowiedział Amazjaszowi: Nie byłem prorokiem ani nawet synem proroka, lecz byłem pasterzem bydła i tym, który zbiera figi sykomory.
15 Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
Ale PAN mnie wziął, gdy [chodziłem] za bydłem, i powiedział do mnie PAN: Idź, prorokuj memu ludowi Izraelowi.
16 Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
Teraz więc słuchaj słowa PANA. Ty mówisz: Nie prorokuj w Izraelu i nie głoś przeciwko domowi Izaaka.
17 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
Dlatego tak mówi PAN: Twoja żona będzie nierządnicą w mieście, twoi synowie i twoje córki padną od miecza, twoja ziemia będzie podzielona sznurem, a ty umrzesz w ziemi nieczystej; Izrael zaś na pewno zostanie uprowadzony do niewoli ze swojej ziemi.

< Amosi 7 >