< Amosi 1 >

1 Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
As palavras de Amós, que era d'entre os pastores de Tecoa, as quaes viu sobre Israel, nos dias de Uzias, rei de Judah, e nos dias de Jeroboão, filho de Joás, rei de Israel, dois annos antes do terremoto.
2 Alisema: “Bwana ananguruma toka Sayuni, pia ananguruma kutoka Yerusalemu; malisho ya wachunga wanyama yanakauka, kilele cha Karmeli kinanyauka.”
E disse: O Senhor bramará de Sião, e de Jerusalem dará a sua voz: as habitações dos pastores prantearão, e seccar-se-ha o cume do Carmelo.
3 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Dameski, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliipura Gileadi kwa vyombo vya chuma vyenye meno.
Assim diz o Senhor: Por tres transgressões de Damasco, e por quatro, não o afastarei, porque trilharam a Gilead com trilhos de ferro.
4 Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.
Por isso porei fogo á casa de Hazael, e consumirá os palacios de Benhadad.
5 Nitalivunja lango la Dameski; nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni, na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni. Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,” asema Bwana.
E quebrarei o ferrolho de Damasco, e exterminarei o morador de Biqueat-aven, e ao que tem o sceptro de Beth-eden; e o povo da Syria será levado em captiveiro a Kir, diz o Senhor.
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima na kuwauza kwa Edomu,
Assim diz o Senhor: Por tres transgressões de Gaza, e por quatro, não o afastarei, porque levaram em captiveiro todos os captivos para os entregarem a Edom.
7 nitatuma moto juu ya kuta za Gaza ambao utateketeza ngome zake.
Por isso porei fogo ao muro de Gaza, que consumirá os seus palacios.
8 Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,” asema Bwana Mwenyezi.
E exterminarei o morador de Asdod, e o que tem o sceptro de Ascalon, e tornarei a minha mão contra Ecron; e o resto dos philisteos perecerá, diz o Senhor Jehovah.
9 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu, na kutokujali mapatano ya undugu,
Assim diz o Senhor: Por tres transgressões de Tyro, e por quatro, não o afastarei, porque entregaram todos os captivos a Edom, e não se lembraram da alliança dos irmãos.
10 Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro ambao utateketeza ngome zake.”
Por isso porei fogo ao muro de Tyro, que consumirá os seus palacios.
11 Hili ndilo Bwana asemalo: “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, alikataa kuonyesha huruma yoyote, kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.
Assim diz o Senhor: Por tres transgressões de Edom, e por quatro, não o afastarei, porque perseguiu a seu irmão á espada, e corrompeu as suas misericordias; e a sua ira despedaça eternamente, e retem a sua indignação para sempre
12 Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”
Por isso porei fogo a Teman, que consumirá os palacios de Bozra.
13 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Amoni, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi ili kuongeza mipaka yake.
Assim diz o Senhor: Por tres transgressões dos filhos de Ammon, e por quatro, não o afastarei, porque fenderam as gravidas de Gilead, para dilatarem os seus termos.
14 Nitatuma moto kwenye kuta za Raba ambao utateketeza ngome zake katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano, katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.
Por isso porei fogo ao muro de Rabba, que consumirá os seus palacios, com alarido no dia da batalha, com tempestade no dia da tormenta.
15 Mfalme wake atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na maafisa wake,” asema Bwana.
E o seu rei irá para o captiveiro, elle e os seus principes juntamente, diz o Senhor.

< Amosi 1 >