< 2 Timotheo 2 >

1 Basi, wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo ndani ya Kristo Yesu.
You then, my child, must be strong in the grace that is in Christ Jesus.
2 Nayo mambo yale uliyonisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu watakaoweza kuwafundisha watu wengine vilevile.
All that you have been taught by me in the hearing of many witnesses, you must hand on to trusty men who shall themselves, in turn, be competent to instruct others also.
3 Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.
As a good soldier of Christ Jesus accept your share of suffering.
4 Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
Every one who serves as a soldier keeps himself from becoming entangled in the world's business--so that he may satisfy the officer who enlisted him.
5 Vivyo hivyo, yeye ashindanaye katika michezo hawezi kupewa tuzo ya ushindi asiposhindana kulingana na kanuni za mashindano.
And if any one takes part in an athletic contest, he gets no prize unless he obeys the rules.
6 Mkulima mwenye bidii ya kazi ndiye anayestahili kuwa wa kwanza kupata fungu la mavuno.
The harvestman who labours in the field must be the first to get a share of the crop.
7 Fikiri sana kuhusu haya nisemayo, kwa maana Bwana atakupa ufahamu katika mambo hayo yote.
Mark well what I am saying: the Lord will give you discernment in everything.
8 Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yeye aliye wa uzao wa Daudi. Hii ndiyo Injili yangu,
Never forget that Jesus Christ has risen from among the dead and is a descendant of David, as is declared in the Good News which I preach.
9 ambayo kwayo ninateseka hata kufikia hatua ya kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi.
For preaching the Good News I suffer, and am even put in chains, as if I were a criminal: yet the word of God is not imprisoned.
10 Kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi wao nao wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios g166)
For this reason I endure all things for the sake of God's own people; so that they also may obtain salvation--even the salvation which is in Christ Jesus--and with it eternal glory. (aiōnios g166)
11 Hili ni neno la kuaminiwa: Kwa maana kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
Faithful is the saying: "If we died with Him, we shall also live with Him;
12 Kama tukistahimili, pia tutatawala pamoja naye. Kama tukimkana yeye, naye atatukana sisi.
"If we patiently endure pain, we shall also share His Kingship; "If we disown Him, He will also disown us;
13 Kama tusipoamini, yeye hudumu kuwa mwaminifu, kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
"And even if our faith fails, He remains true--He cannot prove false to Himself."
14 Endelea kuwakumbusha mambo haya ukiwaonya mbele za Bwana waache kushindana kwa maneno ambayo hayana faida yoyote bali huwaangamiza tu wale wanaoyasikia.
Bring all this to men's remembrances, solemnly charging them in the presence of God not to waste time in wrangling about mere words, a course which is altogether unprofitable and tends only to the ruin of the hearers.
15 Jitahidi kujionyesha kwa Mungu kuwa umekubaliwa naye, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, ukilitumia kwa usahihi neno la kweli.
Earnestly seek to commend yourself to God as a servant who, because of his straightforward dealing with the word of truth, has no reason to feel any shame.
16 Jiepushe na maneno mabaya, yasiyo na maana, yasiyo ya utauwa, kwa maana hayo huzidi kuwatosa watu katika kukosa heshima kwa Mungu.
But from irreligious and frivolous talk hold aloof, for those who indulge in it will proceed from bad to worse in impiety,
17 Mafundisho yao yataenea kama kidonda kisichopona. Miongoni mwao wamo Himenayo na Fileto
and their teaching will spread like a running sore. Hymenaeus and Philetus are men of that stamp.
18 ambao wameiacha kweli, wakisema kwamba ufufuo wa wafu umekwisha kuwako, nao huharibu imani ya baadhi ya watu.
In the matter of the truth they have gone astray, saying that the Resurrection is already past, and so they are overthrowing the faith of some.
19 Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, ukiwa na muhuri wenye maandishi haya: “Bwana anawajua walio wake”; tena, “Kila alitajaye jina la Bwana, na auache uovu.”
Yet God's solid foundation stands unmoved, bearing this inscription, "The Lord knows those who really belong to Him." And this also, "Let every one who names the Name of the Lord renounce all wickedness."
20 Katika nyumba kubwa si kwamba kuna vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali pia vimo vyombo vya miti na vya udongo; vingine kwa matumizi maalum, na vingine kwa matumizi ya kawaida.
Now in a great house there are not only articles of gold and silver, but also others of wood and of earthenware; and some are for specially honourable, and others for common use.
21 Basi ikiwa mtu amejitakasa na kujitenga na hayo niliyoyataja, atakuwa chombo maalum, kilichotengwa na ambacho kinamfaa mwenye nyumba, kimeandaliwa tayari kwa kila kazi njema.
If therefore a man keeps himself clear of these latter, he himself will be for specially honourable use, consecrated, fit for the Master's service, and fully equipped for every good work.
22 Zikimbie tamaa mbaya za ujana, ufuate haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
Keep a strong curb, however, on your youthful cravings; and strive for integrity, good faith, love, peace, in company with all who pray to the Lord with pure hearts.
23 Jiepushe na mabishano ya kipumbavu na yasiyo na maana, kwa kuwa wajua ya kwamba hayo huzaa magomvi.
But avoid foolish discussions with ignorant men, knowing--as you do--that these lead to quarrels;
24 Tena haimpasi mtumishi wa Bwana kuwa mgomvi, bali inampasa awe mwema kwa kila mtu, awezaye kufundisha, tena mvumilivu.
and a bondservant of the Lord must not quarrel, but must be inoffensive towards all men, a skilful teacher, and patient under wrongs.
25 Inampasa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye, kwa matumaini kwamba Mungu atawajalia kutubu na kuijua kweli,
He must speak in a gentle tone when correcting the errors of opponents, in the hope that God will at last give them repentance, for them to come to a full knowledge of the truth
26 ili fahamu zao ziwarudie tena, nao waponyoke katika mtego wa ibilisi ambaye amewateka wapate kufanya mapenzi yake.
and recover sober-mindedness and freedom from the Devil's snare, though they are now entrapped by him to do his will.

< 2 Timotheo 2 >