< 2 Samweli 6 >

1 Tena Daudi akakusanya watu 30,000 wa Israeli waliochaguliwa.
I Dawid ponownie zebrał wszystkich doborowych [mężczyzn] z Izraela, trzydzieści tysięcy.
2 Yeye na watu wake wote wakatoka Baala ya Yuda kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka huko, linaloitwa kwa Jina, naam, jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, ambaye anaketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi walioko juu ya hilo Sanduku.
Potem Dawid wraz z całym ludem, który z nim był, powstał i wyruszył z Baali judzkiej, aby przenieść stamtąd arkę Boga, która nosi imię PANA zastępów zasiadającego [między] cherubinami.
3 Wakaweka hilo Sanduku la Mungu juu ya gari jipya la kukokotwa na kulileta kutoka nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiongoza hilo gari jipya la kukokotwa
I umieścili arkę Boga na nowym wozie, i wywieźli ją z domu Abinadaba położonego w Gibea. A Uzza i Achio, synowie Abinadaba, prowadzili ten nowy wóz.
4 likiwa na Sanduku la Mungu juu yake, naye Ahio alikuwa anatembea akiwa mbele yake.
I wyprowadzili go z domu Abinadaba położonego w Gibea wraz z arką Boga. A Achio szedł przed arką.
5 Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wanacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, zeze, matari, kayamba na matoazi.
Dawid zaś i cały Izrael grali przed PANEM na wszelkich [instrumentach] z drewna jodłowego: na harfach, cytrach, bębnach, piszczałkach i cymbałach.
6 Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Nakoni, Uza akanyoosha mkono na kulishika Sanduku la Mungu kwa sababu maksai walijikwaa.
A [gdy] przybyli do klepiska Nachona, Uzza wyciągnął [rękę] do arki Boga i pochwycił ją, gdyż woły ją szarpnęły.
7 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza kwa sababu ya kitendo chake cha kukosa heshima, kwa hiyo Mungu akampiga akafia papo hapo kando ya Sanduku la Mungu.
I zapłonął gniew PANA przeciwko Uzzie, i Bóg zabił go za uchybienie. I umarł tam przy arce Boga.
8 Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, hivyo hadi leo mahali hapo panaitwa Peres-Uza.
I Dawid był wielce niezadowolony, że PAN tak srogo poraził Uzzę, i nazwał to miejsce Peres-Uzza, i tak jest do dziś.
9 Daudi akamwogopa Bwana siku ile, akasema, “Ni jinsi gani Sanduku la Bwana litakavyoweza kunijia?”
Dawid zląkł się PANA tego dnia i powiedział: Jakże ma przyjść do mnie arka PANA?
10 Hakuwa radhi kulichukua Sanduku la Bwana kwake katika Mji wa Daudi. Badala yake akalipeleka kwenye nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti.
Dlatego Dawid nie chciał sprowadzić arki PANA do siebie, do swego miasta, lecz wprowadził ją do domu Obed-Edoma, Gittyty.
11 Sanduku la Bwana likabaki katika nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti, kwa miezi mitatu, naye Bwana akambariki pamoja na nyumba yake yote.
I arka PANA pozostała w domu Obed-Edoma, Gittyty, przez trzy miesiące. A PAN błogosławił Obed-Edomowi i całemu jego domowi.
12 Kisha Mfalme Daudi akaambiwa, “Bwana ameibariki nyumba ya Obed-Edomu pamoja na kila alicho nacho, kwa sababu ya Sanduku la Mungu.” Basi Daudi akateremka na kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka nyumba ya Obed-Edomu hadi Mji wa Daudi kwa shangwe.
A doniesiono królowi Dawidowi: PAN błogosławi domowi Obed-Edoma i wszystkiemu, co posiada, ze względu na arkę Boga. Dawid poszedł więc i sprowadził z wielką radością arkę Boga z domu Obed-Edoma do miasta Dawida.
13 Wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Bwana walipokuwa wametembea hatua sita, Daudi alitoa dhabihu fahali na ndama aliyenoneshwa.
A gdy ci, którzy nieśli arkę PANA, zrobili sześć kroków, składał w ofierze woły i tuczne [zwierzęta].
14 Daudi, akiwa amevaa kisibau cha kitani, alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote,
I Dawid tańczył przed PANEM z całych sił; był przepasany lnianym efodem.
15 wakati yeye na nyumba yote ya Israeli walipopandisha Sanduku la Bwana kwa shangwe na sauti za tarumbeta.
Tak Dawid i cały dom Izraela sprowadzili arkę PANA z okrzykami i przy dźwiękach trąby.
16 Ikawa Sanduku la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za Bwana, akamdharau moyoni mwake.
A gdy arka PANA weszła do miasta Dawida, Mikal, córka Saula, wyglądała przez okno i zobaczyła króla Dawida, jak skakał i tańczył przed PANEM, i wzgardziła nim w swoim sercu.
17 Wakaleta Sanduku la Bwana na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
Sprowadzili więc arkę PANA i ustawili ją na swoim miejscu w środku namiotu, który rozpiął dla niej Dawid. I Dawid złożył przed PANEM całopalenia i ofiary pojednawcze.
18 Baada ya kumaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, Daudi akawabariki watu katika jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
A gdy Dawid skończył składać całopalenia i ofiary pojednawcze, błogosławił ludowi w imię PANA zastępów.
19 Kisha akatoa mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu kwa kila mtu katika mkutano wote wa Waisraeli, wanaume kwa wanawake. Nao watu wote wakaenda nyumbani kwao.
I rozdał wśród całego ludu i całego zgromadzenia Izraela, zarówno mężczyznom, jak i kobietom, każdemu po jednym bochenku chleba, po jednym kawałku mięsa i po jednym bukłaku [wina]. Potem cały lud odszedł, każdy do swojego domu.
20 Daudi aliporudi ili kuwabariki watu wa nyumbani mwake, Mikali binti Sauli akatoka nje kumlaki, akamwambia, “Tazama jinsi mfalme wa Israeli alivyojibainisha mwenyewe leo kwa kuvua mavazi yake machoni pa vijakazi wa watumishi wake, kama vile ambavyo mtu asiye na adabu angelifanya!”
Potem Dawid wrócił, aby pobłogosławić swój dom. I Mikal, córka Saula, wyszła naprzeciw Dawidowi, i powiedziała: O jakże wspaniały był dziś król Izraela, który się obnażył dziś na oczach służących swych sług, tak jak się obnaża jakiś niepoważny [człowiek]!
21 Daudi akamwambia Mikali, “Nilifanya hivyo mbele za Bwana ambaye alinichagua mimi badala ya baba yako au mwingine yeyote kutoka nyumba yake wakati aliponiweka niwe mtawala juu ya Israeli, watu wa Bwana. Kwa hiyo nitacheza mbele za Bwana.
Wtedy Dawid powiedział do Mikal: [Grałem] przed PANEM, który wybrał raczej mnie niż twego ojca i niż cały jego dom, aby ustanowić mnie wodzem nad ludem PANA, nad Izraelem. Będę więc grał przed PANEM.
22 Nitakuwa asiye na heshima zaidi kuliko sasa, nami nitajishusha machoni pangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliosema habari zao nitaheshimiwa.”
I poniżę się jeszcze bardziej niż dotąd, i będę jeszcze bardziej godny pogardy w swoich oczach, lecz u służących, o których mi mówiłaś, będę poważany.
23 Naye Mikali binti Sauli hakuwa na watoto mpaka siku ya kufa kwake.
Mikal, córka Saula, nie miała więc dzieci aż do dnia swej śmierci.

< 2 Samweli 6 >