< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
Und David redete vor dem HERRN die Worte dieses Liedes zur Zeit, da ihn der HERR errettet hatte von der Hand aller seiner Feinde und von der Hand Sauls, und sprach:
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
Der HERR ist mein Fels und meine Burg und mein Erretter.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Gott ist mein Hort, auf den ich traue, mein Schild und Horn meines Heils, mein Schutz und meine Zuflucht, mein Heiland, der du mir hilfst vor dem Frevel.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Ich rufe an den HERRN, den Hochgelobten, so werde ich von meinen Feinden erlöst.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Es hatten mich umfangen die Schmerzen des Todes, und die Bäche des Verderbens erschreckten mich.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Der Hölle Bande umfingen mich, und des Todes Stricke überwältigten mich. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
Da mir angst war, rief ich den HERRN an und schrie zu meinem Gott; da erhörte er meine Stimme von seinem Tempel, und mein Schreien kam vor ihn zu seinen Ohren.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Die Erde bebte und ward bewegt; die Grundfesten des Himmels regten sich und bebten, da er zornig war.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Dampf ging auf von seiner Nase und verzehrend Feuer von seinem Munde, daß es davon blitzte.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Er neigte den Himmel und fuhr herab, und Dunkel war unter seinen Füßen.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Und er fuhr auf dem Cherub und flog daher, und er schwebte auf den Fittichen des Windes.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
Sein Gezelt um ihn her war finster und schwarze, dicke Wolken.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Von dem Glanz vor ihm brannte es mit Blitzen.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Der HERR donnerte vom Himmel, und der Höchste ließ seinen Donner aus.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
Er schoß seine Strahlen und zerstreute sie; er ließ blitzen und erschreckte sie.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Da sah man das Bett der Wasser, und des Erdbodens Grund ward aufgedeckt von dem Schelten des HERRN, von dem Odem und Schnauben seiner Nase.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Er streckte seine Hand aus von der Höhe und holte mich und zog mich aus den großen Wassern.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Er errettete mich von meinen starken Feinden, von meinen Hassern, die zu mir mächtig waren,
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
die mich überwältigten zur Zeit meines Unglücks; und der HERR ward meine Zuversicht.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Und er führte mich aus in das Weite, er riß mich heraus; denn er hatte Lust zu mir.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Der HERR tut wohl an mir nach meiner Gerechtigkeit; er vergilt mir nach der Reinigkeit meiner Hände.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Denn ich halte die Wege des HERRN und bin nicht gottlos wider meinen Gott.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Denn alle seine Rechte habe ich vor Augen, und seine Gebote werfe ich nicht von mir;
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
sondern ich bin ohne Tadel vor ihm und hüte mich vor Sünden.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Darum vergilt mir der HERR nach meiner Gerechtigkeit, nach meiner Reinigkeit vor seinen Augen.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Bei den Heiligen bist du heilig, bei den Frommen bist du fromm,
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
bei den Reinen bist du rein, und bei den Verkehrten bist du verkehrt.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Denn du hilfst dem elenden Volk, und mit deinen Augen erniedrigst du die Hohen.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Denn du, HERR, bist meine Leuchte; der HERR macht meine Finsternis licht.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Denn mit dir kann ich Kriegsvolk zerschlagen und mit meinem Gott über die Mauer springen.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Gottes Wege sind vollkommen; des HERRN Reden sind durchläutert. Er ist ein Schild allen, die ihm vertrauen.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Denn wo ist ein Gott außer dem HERRN, und wo ist ein Hort außer unserm Gott?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Gott stärkt mich mit Kraft und weist mir einen Weg ohne Tadel.
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Er macht meine Füße gleich den Hirschen und stellt mich auf meine Höhen.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Er lehrt meine Hände streiten und lehrt meinen Arm den ehernen Bogen spannen.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Du gibst mir den Schild deines Heils; und wenn du mich demütigst, machst du mich groß.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Du machst unter mir Raum zu gehen, daß meine Knöchel nicht wanken.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Ich will meinen Feinden nachjagen und sie vertilgen und will nicht umkehren, bis ich sie umgebracht habe.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Ich will sie umbringen und zerschmettern; sie sollen mir nicht widerstehen und müssen unter meine Füße fallen.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Du kannst mich rüsten mit Stärke zum Streit; du kannst unter mich werfen, die sich wider mich setzen.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Du gibst mir meine Feinde in die Flucht, daß ich verstöre, die mich hassen.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Sie sahen sich um, aber da ist kein Helfer, nach dem HERRN; aber er antwortet ihnen nicht.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Ich will sie zerstoßen wie Staub auf der Erde; wie Kot auf der Gasse will ich sie verstäuben und zerstreuen.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Du hilfst mir von dem zänkischen Volk und behütest mich, daß ich ein Haupt sei unter den Heiden; ein Volk, das ich nicht kannte, dient mir.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Den Kindern der Fremde hat's wider mich gefehlt; sie gehorchen mir mit gehorsamen Ohren.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Die Kinder der Fremde sind verschmachtet und kommen mit Zittern aus ihren Burgen.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Der HERR lebt, und gelobt sei mein Hort; und Gott, der Hort meines Heils, werde erhoben,
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
der Gott, der mir Rache gibt und wirft die Völker unter mich.
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Er hilft mir aus von meinen Feinden. Du erhöhst mich aus denen, die sich wider mich setzen; du hilfst mir von den Frevlern.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Darum will ich dir danken, HERR, unter den Heiden und deinem Namen lobsingen,
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
der seinem Könige großes Heil beweist und wohltut seinem Gesalbten, David und seinem Samen ewiglich.

< 2 Samweli 22 >